Pepombili
JF-Expert Member
- Dec 20, 2010
- 439
- 58
DIWANI wa Serengeti, Chacha Samwel Gibewa (Chadema) amesalimisha kwa Mkuu wa Mkoa wa Mara, Kanali Enos Mfuru bunduki aina ya AK 47 ambayo amekuwa akimiliki kinyume cha Sheria.
Kiongozi huyo wa wananchi aliwasilisha bunduki hiyo Jumanne jioni baada ya madiwani wenzake kumtuhumu kwa kuchochea ugomvi wa kikabila na kupinga kusajili wa Shule ya Sekondari Machochwe kuwa Shule ya Kidato cha Tano na Sita.
Kabla kukubali kukabidhi bunduki hiyo wakati wa kikao cha bajeti cha baraza la madiwani, Mkuu wa Mkoa alimuonya kuwa atakabiliwa na hatua kali dhidi yake ambazo hatazisahau maishani. Kuwa makini.
Natamani ungefahamu mimi ni mtu wa namna gani. Leo lazima unipe bunduki ama sivyo utakaa jela mpaka utajuta, Kanali Mfuru alimuonya Gibewa ambaye ni Diwani wa Kata ya Machochwe.
Diwani huyo alilazimishwa kuomba msamaha kufuatia tuhuma zilizotolewa na wazungumzaji kadhaa waliosimama kuzungumza katika mkutano huo na kumtaka abadilishe tabia yake.
Napenda kuomba msamaha na kama kuna dalili za ukabila ndani ya moyo wangu nitaacha na kuhusu bunduki nitaitoa kama ninayo, alisema Gibewa ambaye alipigiwa makofi na wajumbe wa baraza.
Mfuru alimshukuru diwani huyo kwa uamuzi wake lakini aliendelea kumshinikiza kutoa bunduki mara moja. Diwani Gibewa alikubaliana na amri hiyo na kukubali kuongozana na Mkuu wa Mkoa bpamoja na Mkuu wa Wilaya Edward Lenga na kwenda kijijini Machachowe ambapo ni kilometa 20 kutoka sehemu ulipokuwa ukifanyika mkutano.
Gibewa alimpeleka mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya hadi shambani kwake ambapo alitoa bunduki kutoka kwenye shimo na kumkabidhi Kanali Mfuru.
Lilikuwa ni shimo refu na alisalimisha na risasi ambazo hazijatumiwa, alisema Lenga.
HAPA NAZIDI KUOGOPA MMMM CHADEMA
source:Habari leo
Kiongozi huyo wa wananchi aliwasilisha bunduki hiyo Jumanne jioni baada ya madiwani wenzake kumtuhumu kwa kuchochea ugomvi wa kikabila na kupinga kusajili wa Shule ya Sekondari Machochwe kuwa Shule ya Kidato cha Tano na Sita.
Kabla kukubali kukabidhi bunduki hiyo wakati wa kikao cha bajeti cha baraza la madiwani, Mkuu wa Mkoa alimuonya kuwa atakabiliwa na hatua kali dhidi yake ambazo hatazisahau maishani. Kuwa makini.
Natamani ungefahamu mimi ni mtu wa namna gani. Leo lazima unipe bunduki ama sivyo utakaa jela mpaka utajuta, Kanali Mfuru alimuonya Gibewa ambaye ni Diwani wa Kata ya Machochwe.
Diwani huyo alilazimishwa kuomba msamaha kufuatia tuhuma zilizotolewa na wazungumzaji kadhaa waliosimama kuzungumza katika mkutano huo na kumtaka abadilishe tabia yake.
Napenda kuomba msamaha na kama kuna dalili za ukabila ndani ya moyo wangu nitaacha na kuhusu bunduki nitaitoa kama ninayo, alisema Gibewa ambaye alipigiwa makofi na wajumbe wa baraza.
Mfuru alimshukuru diwani huyo kwa uamuzi wake lakini aliendelea kumshinikiza kutoa bunduki mara moja. Diwani Gibewa alikubaliana na amri hiyo na kukubali kuongozana na Mkuu wa Mkoa bpamoja na Mkuu wa Wilaya Edward Lenga na kwenda kijijini Machachowe ambapo ni kilometa 20 kutoka sehemu ulipokuwa ukifanyika mkutano.
Gibewa alimpeleka mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya hadi shambani kwake ambapo alitoa bunduki kutoka kwenye shimo na kumkabidhi Kanali Mfuru.
Lilikuwa ni shimo refu na alisalimisha na risasi ambazo hazijatumiwa, alisema Lenga.
HAPA NAZIDI KUOGOPA MMMM CHADEMA
source:Habari leo