Diwani, Mbunge, Waziri n.k awe na elimu ya level gani katika Katiba Mpya?

Patriote

JF-Expert Member
Jul 13, 2011
1,718
1,047
Nimefuatilia kwa makini mijadala mbali mbali ya Katiba na hata ya kijamii, nimegundea suala la elimu anayopaswa kuwa nayo kiongozi halitajwi sana, hii inaweza kuwa inachangiwa na viongozi wenyewe kutokuwa na elimu ya kulidhisha, hivyo mada ya level ya elimu kwao inakosa mvuto. Lakin ndugu zangu lazma tujue kuwa elimu ina mchango mkubwa katika utendaji wa jamii mbalimbali, sisemi lazma viongozi wawe na PHD, la hasha, ila kuna umuhimu kwa kiongozi kuwa angalau na kiwango fulani cha Elimu kuliko ilivyo sasa ambapo hakuna kiwango chochote kinachotajwa zaidi ya kusema awe Raia anayejua kusoma na kuandika.

Nimepita kwenye CV mbalimbali za waheshimiwa wetu kwa kweli kwa CV zile tusitegemee ya ajabu, Wanachokifanya sasa hivi wanajitahid sana kwa CV zile. CV nyingi zimekaa kiujanjaujanja, hazina mtiririko mzuri na kwa kweli ni aibu kwa Taifa. Mara mtu kasoma hadi O-level then kaunga Degree. Utaratibu wa wapi huu???Au labda zimenakiliwa vibaya??? Kwa sasa nalazimika kuamin waliozinakili wamenakili vibaya kwenye website ya bunge, naomba wahusika wazirekebishe. Sasa hali ipo hivyo kwa Bunge, Je hali ipoje huko chini kwa madiwami na watendaji wa vijiji tunapotegemea maendeleo yafanyike???

Mimi nadhan kuna haja sasa kupose changamoto kwa kuweka kigezo cha elimu, ili anayefikiria kuomba uongozi fulani ajipange kwanza kabla ya kuamua kufanya hivyo. Hii ni sawa kabisa na mtu anayefikiria kuwa mhasibu kujipanga kwanza kwa kwenda chuoni kupata elimu ya uhasibu. Hili suala la kusema raia yeyote ili mradi awe na uwezo wa kujua kusoma na kuandika mimi nadhan kwa karne hii limeshapitwa na wakati. Katiba ya mwanzo ilikuwa na kigezo hicho maana wasomi hawakuwepo, leo miaka 50 ya uhuru bado kigezo ni hicho hicho jaman???Basi kama kigezo cha kiongozi wa nchi hii ni hicho?? basi hata kwa kazi nyingine kigezo kiwe ni hicho hicho. Kwa nini serikali inataka mfanyakazi wa kawaida kama msaidizi wa ofisi au tarishi/mesenja awe na elimu fulani wakati kiongozi wa ngazi ya juu kama Mbunge au Waziri hajawekewa kigezo cha Elimu???Mimi nadhani suala la elimu halihitaji siasa. Kama viongozi wetu hasa watunga sheria hawana elimu ya kutosha ni dhahiri hata sheria zinazotungwa zitakuwa ni za kibabaishaji. Hebu wana JF tulijadili hili.
 
Nimefuatilia kwa makini mijadala mbali mbali ya Katiba na hata ya kijamii, nimegundea suala la elimu anayopaswa kuwa nayo kiongozi halitajwi sana, hii inaweza kuwa inachangiwa na viongozi wenyewe kutokuwa na elimu ya kulidhisha, hivyo mada ya level ya elimu kwao inakosa mvuto. Lakin ndugu zangu lazma tujue kuwa elimu ina mchango mkubwa katika utendaji wa jamii mbalimbali, sisemi lazma viongozi wawe na PHD, la hasha, ila kuna umuhimu kwa kiongozi kuwa angalau na kiwango fulani cha Elimu kuliko ilivyo sasa ambapo hakuna kiwango chochote kinachotajwa zaidi ya kusema awe Raia anayejua kusoma na kuandika.

Nimepita kwenye CV mbalimbali za waheshimiwa wetu kwa kweli kwa CV zile tusitegemee ya ajabu, Wanachokifanya sasa hivi wanajitahid sana kwa CV zile. CV nyingi zimekaa kiujanjaujanja, hazina mtiririko mzuri na kwa kweli ni aibu kwa Taifa. Mara mtu kasoma hadi O-level then kaunga Degree. Utaratibu wa wapi huu???Au labda zimenakiliwa vibaya??? Kwa sasa nalazimika kuamin waliozinakili wamenakili vibaya kwenye website ya bunge, naomba wahusika wazirekebishe. Sasa hali ipo hivyo kwa Bunge, Je hali ipoje huko chini kwa madiwami na watendaji wa vijiji tunapotegemea maendeleo yafanyike???

Mimi nadhan kuna haja sasa kupose changamoto kwa kuweka kigezo cha elimu, ili anayefikiria kuomba uongozi fulani ajipange kwanza kabla ya kuamua kufanya hivyo. Hii ni sawa kabisa na mtu anayefikiria kuwa mhasibu kujipanga kwanza kwa kwenda chuoni kupata elimu ya uhasibu. Hili suala la kusema raia yeyote ili mradi awe na uwezo wa kujua kusoma na kuandika mimi nadhan kwa karne hii limeshapitwa na wakati. Katiba ya mwanzo ilikuwa na kigezo hicho maana wasomi hawakuwepo, leo miaka 50 ya uhuru bado kigezo ni hicho hicho jaman???Basi kama kigezo cha kiongozi wa nchi hii ni hicho?? basi hata kwa kazi nyingine kigezo kiwe ni hicho hicho. Kwa nini serikali inataka mfanyakazi wa kawaida kama msaidizi wa ofisi au tarishi/mesenja awe na elimu fulani wakati kiongozi wa ngazi ya juu kama Mbunge au Waziri hajawekewa kigezo cha Elimu???Mimi nadhani suala la elimu halihitaji siasa. Kama viongozi wetu hasa watunga sheria hawana elimu ya kutosha ni dhahiri hata sheria zinazotungwa zitakuwa ni za kibabaishaji. Hebu wana JF tulijadili hili.

Elimu ni muhimu sana lakini si kila mwenye elimu anaitumia vizuri,kuna watu wanapinga na kutoa mifano kuwa elimu si muhimu sana kwani wanadai kuwa kuna watu (siwataji) walifanya kazi vizuri sana bila elimu,lakini wanasahau kipindi hicho kilikuwaje!!mimi nadhani sababu kubwa ya mtu kupotea hivi mara nyingi utakuta ajaenda shule inayojadiliwa hivyo anahisi kuwa wanamnyanyapaa,ni kujihami tu kihisia,lakini ukiwa umeenda shule utagundua kuwa elimu ni muhimu sana,kwanza unajihamini katika maamuzi yako bila kufikiria kushikwa mkono,mara nyingi mtu akipewa position ambayo kielimu halingani nayo majungu na kujipendekeza ndiyo itakuwa misingi ya kazi.

Kwa maoni yangu mbunge awe na elimu ya kuanzia Advanced diploma/degree na awe ameipata kutoka katika vyuo vinavyotambulika na mitaala inayotambulika pia,udiwani awe na elimu kuanzia elimu ya cheti na kidato cha sita au ordinary diploma,nimeacha kidato cha nne kwa sababu div 4 point 30 ni sawa na bure kwani ndiyo hao waliochaguana sumbawanga kuwa meya akachemsha!!!,kwa upande wa Rais awe na elimu kuanzia Master degree bila kuhusisha phd za heshima.
 
Elimu ni muhimu sana lakini mbona hata Rais wenu kikwete ana Degree tena ya Uchumi lakini hajui kwanini Tanzania Maskini. na akakaa karibia nusu mwaka akaja na jibu ambalo bado sio sahihi. Cha msingi m naamini midahalo ya papo kwa papo muhimu sana maana ikulu wanaamini kila risala lazima aandikiwe
 
Suala la kiongozi aliyekwenda shule ni lazima kama tunataka kufika mahala tukawa tunajadili hoja na wenzetu kwa uzito ulio sawa. Vinginevyo kila siku tutaishia kupiga kelele na hii mikataba mibovu ya Chief Mangungo style.Suala la Kikwete kwenda shule na kushindwa kuperform sio justification ya kuendelea kuwa na viongozi wasiokwenda shule. Sisi tuweke misingi ili hata kama hatutafanikiwa kumaliza tatizo hili basi tulipunguze kwa asilimia kubwa!!
 
Back
Top Bottom