Hassan J. Mosoka
JF-Expert Member
- Oct 26, 2010
- 682
- 323
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, Diwani wa Kata ya Bumera kwa tiketi ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tengera Marwa jana alitolewa gerezani kwa muda na kwenda kuapishwa wakati wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime na baadaye alirudishwa gerezani.
Diwani huyo yuko rumande tangu mwanzoni mwa mwaka huu akituhumiwa kwa mauaji na hata fomu za kugombea udiwani alipelekewa rumande na kufanikiwa kumshinda Katibu Uenezi na Siasa wa CCM wilaya ya Tarime, James Nokwe katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 31 mwaka huu.
Diwani huyo yuko rumande tangu mwanzoni mwa mwaka huu akituhumiwa kwa mauaji na hata fomu za kugombea udiwani alipelekewa rumande na kufanikiwa kumshinda Katibu Uenezi na Siasa wa CCM wilaya ya Tarime, James Nokwe katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 31 mwaka huu.