Diwani CCM Dotto Mtawa ashikiliwa na polisi kwa wizi wa gari

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,883
DIWANI wa Kata ya Kigamboni jijini Dar es Salaam, Dotto Mtawa (CCM), anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Morogoro kwa tuhuma za wizi wa gari.

Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima imezipata zilisema diwani huyo alikamatwa juzi jioni, katika viwanja vya Tuamoyo katika eneo la Kigamboni kwenye sherehe za mkesha wa Mwenge wa Uhuru na kwenda kuhojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam kabla ya kupelekwa mkoani Morogoro.....

Mbunge wa Kigamboni, Dk. Faustine Ndugulile, alikiri kupata taarifa hizo na kusema kwamba wanalishughulikia kujua sababu zilizomfanya diwani huyo achukuliwe na polisi.....

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Adolphina Chialo, alizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu ya kiganjani na kukiri kufikishwa kwa mtuhumiwa huyo kutoka jijini Dar es Salaam, akisema anahusishwa na wizi wa gari aina ya Toyota Coaster lenye namba T 615 BUL.

Chialo alisema tukio hilo lilitokea Agosti 18 mwaka huu, katika eneo la Msamvu Nane Nane mkoani Morogoro kwa watuhumiwa kumnywesha dawa za kulevya dereva aliyekuwa akiendesha gari hilo. Aliwataja watuhumiwa wengine wanaoshikiliwa kuwa ni Christopher Nyakiaga na mwingine aliyemtaja kwa jina moja la Kileo, na kwamba Mtawa anashikiliwa kwa kuwa inadaiwa kulinunua gari hilo.


Source: Tanzania daima
 
Kosa lake ni ndogo tu. Anatakiwa kudhibitisha tu kuwa hakujua kwamba gari hilo ni mali ya wizi. Sana sana yeye atakuwa ni shahidi namba moja dhidi ya hao wezi.
 
DIWANI wa Kata ya Kigamboni jijini Dar es Salaam, Dotto Mtawa (CCM), anashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani Morogoro kwa tuhuma za wizi wa gari. Habari za uhakika ambazo Tanzania Daima imezipata zilisema diwani huyo alikamatwa juzi jioni, katika viwanja vya Tuamoyo katika eneo la Kigamboni kwenye sherehe za mkesha wa Mwenge wa Uhuru na kwenda kuhojiwa katika Kituo Kikuu cha Polisi jijini Dar es Salaam kabla ya kupelekwa mkoani Morogoro.....

Mbunge wa Kigamboni, Dk. Faustine Ndugulile, alikiri kupata taarifa hizo na kusema kwamba wanalishughulikia kujua sababu zilizomfanya diwani huyo achukuliwe na polisi.....

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro, Adolphina Chialo, alizungumza na Tanzania Daima kwa njia ya simu ya kiganjani na kukiri kufikishwa kwa mtuhumiwa huyo kutoka jijini Dar es Salaam, akisema anahusishwa na wizi wa gari aina ya Toyota Coaster lenye namba T 615 BUL. Chialo alisema tukio hilo lilitokea Agosti 18 mwaka huu, katika eneo la Msamvu Nane Nane mkoani Morogoro kwa watuhumiwa kumnywesha dawa za kulevya dereva aliyekuwa akiendesha gari hilo. Aliwataja watuhumiwa wengine wanaoshikiliwa kuwa ni Christopher Nyakiaga na mwingine aliyemtaja kwa jina moja la Kileo, na kwamba Mtawa anashikiliwa kwa kuwa inadaiwa kulinunua gari hilo.

Source: Tanzania daima

TBC itangaze hili kama Zombe alivyomshikilia bango mpiganaji Lema.
Magamba wapo wauza unga wakuu, majambazi wakuu, wauaji wakuu, in fact Magamba ni Mafia wanaoshikilia serikali kama columbia na vinchi vya latin amerika
 
Ni Dotto Masawani, diwani wa kata ya Kigamboni, hata kabla ya kugombea kuliwahi kuibuka tuhuma za yeye kushiriki katika wizi wa gari la mkuu wa majeshi katika moja ya nchi za eac,

yote kwa yote, kaipendezesha kigamboni hasa eneo la ferry
 
CCM wamejaa vibaka na majambazi, yupo diwani wao mmoja anatokea sijui kule Unga Mwingi, lihalifu la kutupwa!
 
CCM wamejaa vibaka na majambazi, yupo diwani wao mmoja anatokea sijui kule Unga Mwingi, lihalifu la kutupwa!

Mkuu kwani hawa jamaa wana matatizo gani?unamkumbuka yule mwenzao alikuwa wa uenezi hapa dar,wanamwita sijui Haj'i Manar!naye alikutwa na magari ya wizi!!
 
Kinacho ingia kwenye taka ni taka! Kama wakuu wanatuhumiwa kwa wizi na ubadhirifu wadogo nao hawata acha.
 
Angekuwa wa CDM magazeti yote na radio fulani fulani wangefanya talk of the day
 
Nasubiri ngongo aje kuchangia maana hakawii kusema ni rafiki'ake Lema!
 
Kosa lake ni ndogo tu. Anatakiwa kudhibitisha tu kuwa hakujua kwamba gari hilo ni mali ya wizi. Sana sana yeye atakuwa ni shahidi namba moja dhidi ya hao wezi.

Nasita kuunga mkono hoja yako kwa maana kwamba gari ya wizi utaitambua tu kutokana na kukosekana kwa baadhi ya vielelezo, nyaraka na mengineyo. Mnunuzi makini wa gari anahakikisha gari ina viambatanisho vya kisheria vya mmiliki anayeuza.
 
Kuna dalili nyingi tu za zile tuhuma za vyombo vya habari kununuliwa na CCM na serikali, kwani kashfa nyingi za viongozi wa CCM na srikli vyombo vya habari haviandiki, na kuna kila jitihada za kuficha mengi yanayoendelea ambayo ni uzembe wa waziwazi.

  • Ustaadhi Alhaji Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kunywa pombe hadharani wakati wa wakiwa ziarani mkuani Rukwa, vyombo vyote vya habari vimefunika kombe mwanaharamu apite.
  • Wizi huu wa diwani wa CCM mambo yanaendeshwa kimya kimya wakati yametokea kwenye mikondo iliyojaa vyombo vya habari.
Mambo hayo yangefanywa na wapinzani ungekuwa wimbo usioisha kwa mwezi mzima na mahabusu kujaa watuhumiwa.
 
Nanukuu "..........Ustaadhi Alhaji Makamu wa Rais na Waziri Mkuu kunywa pombe hadharani wakati wa wakiwa ziarani mkuani Rukwa, vyombo vyote vya habari vimefunika kombe mwanaharamu apite......" mwisho wa kunukuu

Hawakua mkoani Rukwa na Makamu wa raisi hakunywa pombe ila alikua anapata maelekezo kutoka kwa waziri mkuu kuhusu hiyo pombe ya asili ya Wafipa. shughuli hiyo ilikua ni maalum kwa ajili ya kabila hilo pale Kijiji cha Makumbusho Dar es Salaam!
 
Kosa lake ni ndogo tu. Anatakiwa kudhibitisha tu kuwa hakujua kwamba gari hilo ni mali ya wizi. Sana sana yeye atakuwa ni shahidi namba moja dhidi ya hao wezi.

Huyu ni mwizi tu, IGNORANCE IS NO EXCUSE IN A COURT OF LAW. He should have done some due diligence before buying the vehicle!!
 
Huyu jamaa ilikuwa kazi yake kabla ya kuwa Diwani. SAsa kumbe ukila nyama ya mtu hutaacha. NAsikia alikingiwa kifua na prince ili jina lake lirudi kwenye udiwani.
 
Kosa lake ni ndogo tu. Anatakiwa kudhibitisha tu kuwa hakujua kwamba gari hilo ni mali ya wizi. Sana sana yeye atakuwa ni shahidi namba moja dhidi ya hao wezi.
mh! kukutwa na mali ya wizi na wewe unahesabika kama mwizi. kwamba hukujua kwua hiyo si mali ya wizi wakati unanunua, si utetezi unaokubalika
 
Jamaa huyu ni jambazi maarufu Kigamboni hata wapiga kura wake wanajua hilo na wakati wa kuomba kura wananchi walihoji kwanini bwana Dotto alifungwa jela kama yeye sio jambazi? Dotto aliwajibu wapiga kura wake kuwa mahakama alimuachia huru baada ya kudhibitisha kuwa sie jambazi na hakuwa amefungwa bali alikua ni mahabusu kwa miezi sita.

Katika kesi iyo ya awali yapata miaka mitatu iliyopita Dotto kabla hajawa diwani alikamatwa na gari la UN lililoibiwa kwa mama flani na kuswekwa miezi sita mahabusu na kesi ikamalizwa kimjini chini ya usimamizi wa Alex Massawe ambaye anamtumia bwana Dotto kama kijana wake wa shuhuli zake za mjini.

Diwani huyu anamatukio kadhaa ya wizi wa magari ila huwa zinamalizwa juu kwa juu na Alex Massawe.
Mmoja kati ya wapiga kura wake ambaye ni jirani yake anasema huyu Dotto anatambulika kwa uwizi na ubabe ivyo huogopewa sana na majirani na ameshinda kiti hicho cha udiwani kwa kusaidiwa na wazee na makada wa CCM kwa kushawishi wananchi kuwa Dotto sio jambazi na na kuzidi kumtetea hakuwa mfungwa bali alikua ni mahabusu lakini leo hii ndo ivyo tena amekua mahabusu tena kwa kesi ya gari kama awali kabla hajawa mbunge.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom