Mphamvu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 10,702
- 3,288
Diwani mteule wa kata ya Kijitonyama kwa Ali Maua, Mhe. Juma Athumani Ulole Ulole anashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma za kutaka kumbaka binti mmoja kwa ahadi ya kumtafutia kazi huko Mashariki ya Kati.
Ulole Ulole ni diwani mteule wa kata hiyo kwa tiketi ya CHADEMA ingawa matokeo ya uchaguzi huo yalibatilishwa na mahakama hivyo kubatilisha ushindi wake.
Kwa mujibu wa binti aliyedaiwa kutaka kubakwa, diwani huyo alimuita katika guest house moja na kufanya jaribio la kufanya nae mapenzi ambapo binti huyo aligoma na baadae kwenda kutoa taaarifa kituo sha polisi.
Chanzo: ITV
Kwa mtazamo wangu, kuna jambo linataka kutendeka hapa, maelezo ya polisi yanadai kuwa, diwani ali-attempt kumuingilia binti kwa nguvu, wakati ibinti mwenyewe anadai kuwa diwani aliomba penzi, na si kulazimisha kama taarifa ya polisi inavyodai. Na kama ni kweli aliyoyasema binti kwenye chombo cha habari, kwanini kesi ya msingi isiwe ni ya kuomba rushwa ya ngono badala ya jaribio la kubaka?
Kuna kila dalili ya huyu binti kutumiwa na watu fulani, hasa aliyekuwa mgombea udiwani wa kata hiyo kwa tiketi ya CCM, Ndugu Said Bulembo aliyeshindwa katika uchaguzi huo licha ya kutumia fedha kuhonga wapiga kura pamoja na chakula. Wasiwasi unakuwa mwingi kutokana na mazingira husika, kuna jaribio la kubaka linalofanyika gesti wajameni?
Ulole Ulole ni diwani mteule wa kata hiyo kwa tiketi ya CHADEMA ingawa matokeo ya uchaguzi huo yalibatilishwa na mahakama hivyo kubatilisha ushindi wake.
Kwa mujibu wa binti aliyedaiwa kutaka kubakwa, diwani huyo alimuita katika guest house moja na kufanya jaribio la kufanya nae mapenzi ambapo binti huyo aligoma na baadae kwenda kutoa taaarifa kituo sha polisi.
Chanzo: ITV
Kwa mtazamo wangu, kuna jambo linataka kutendeka hapa, maelezo ya polisi yanadai kuwa, diwani ali-attempt kumuingilia binti kwa nguvu, wakati ibinti mwenyewe anadai kuwa diwani aliomba penzi, na si kulazimisha kama taarifa ya polisi inavyodai. Na kama ni kweli aliyoyasema binti kwenye chombo cha habari, kwanini kesi ya msingi isiwe ni ya kuomba rushwa ya ngono badala ya jaribio la kubaka?
Kuna kila dalili ya huyu binti kutumiwa na watu fulani, hasa aliyekuwa mgombea udiwani wa kata hiyo kwa tiketi ya CCM, Ndugu Said Bulembo aliyeshindwa katika uchaguzi huo licha ya kutumia fedha kuhonga wapiga kura pamoja na chakula. Wasiwasi unakuwa mwingi kutokana na mazingira husika, kuna jaribio la kubaka linalofanyika gesti wajameni?