TANZIA Ukiwaona Ditopile afariki dunia

6404.JPG

Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Yusuph Makamba ( wa tatu kulia ) na viongozi wengine wakiwa wamezunguka jeneza lenye mwili wa marehemu Ditopile Mzuzuri katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro jana, kabla ya kusafirishwa kwenda Dar es Salaam kwa mazishi. Wa pili kulia ni Kamanda mstaafu wa Jeshi la Polisi nchini, Bw. Omari Mahita ( Picha na Ramadhan Libenanga)
 
Mungu ametoa na Mungu ametwaa Jina la Bwana Lihimidiwe.
Natoa Pole kwa familia ya Mzee Dito na wanae kina Ramadhan.
Tukutane Msibani baadaye!
 
View attachment 1449
Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Yusuph Makamba ( wa tatu kulia ) na viongozi wengine wakiwa wamezunguka jeneza lenye mwili wa marehemu Ditopile Mzuzuri katika Hospitali ya Mkoa wa Morogoro jana, kabla ya kusafirishwa kwenda Dar es Salaam kwa mazishi. Wa pili kulia ni Kamanda mstaafu wa Jeshi la Polisi nchini, Bw. Omari Mahita ( Picha na Ramadhan Libenanga)

Mafisadi wakiwa wamemzunguka mwenzao.
Hapo ndo wanapaswa kujua kuwa ubabe na ubaradhuli haulipi,wakati wao wanajidai kulia sisi wengine ni sherehe na furaha tu kwenda mbele.Dunia hii imeshuhudia wababe,mabedui na mafedhuli wengine katika historia,kuanzia kina Hitler,Mussolini,Bokassa,Idd Amini,Napoleon Bonaparte,na wengine wengi tu,wote hawa walitembea juu ya uso wa duni na kufikiri madraka na utajiri,ufisadi vingewafanya wadumu milele wakiwakandamiza binadamu wenzao,on the other hand watu wema wameacha historia na duni itawakumbuka milele:Nyerere,Nkurumah,Gandhi,martin Luther King Jr.Jesus Christ,Mtume Muhamad,Mother Theresa,Pope John Paul II,Che Guevara etc...

Mimi kwangu ni kuwa finally justice has been done,Muumba ndo atamuamuli but personally I wish Ditopile suffer in eternally in hell.
 
Linapokuja suala la hukumu nje ya dunia hii, sipo tayari kumpiga yeyote mawe.
Ni wauwaji wangapi hatuwajui?
RIP Ditto!
 
Chenge kubwaga manyanga yamkini ni shinikizo la Kaka Jakaya maana jeuri aliyonayo haiashirii kuwa hili limetoka moyoni mwake.

Ila hakika hili lilikuwa jigogo.

THANX TO GOD "KILIO CHA WA TANZANIA AMEKISIKIA".

Mamilioni ya ankara yaitwa vijisent DAH? inhali mama wajawazito na watoto wanakufa kwa kukosa huduma ndogo kama ya oxygen baada ya umeme kukatika na jenereta kukosekana?

I just wonder how many standby generators and oxygen facilities could by purchased to save lives by the said "VIJISENTI".
 
Unafiki juu ya kifo cha Ditto sitaki kabisa.Naamini kila mwanadamu atayaonja mauti na hili sina wasiwasi nalo.Nadhani Mungu sasa yuko upande wa watanzania wanaodhulumiwa haki za na baadhi ya watu wenye mamlaka ha TZ.

Kesi ya mauaji iliyokua ikimkabili mheshimiwa huyu ilipindishwa na watu wasiokua na akili mpaka kudiliki kupindisha sheria na kuanzisha vitu ambavyo havipo kabisa.Kimsingi kwa taaluma ya sheria ninayoijua mimi,hakuna kosa la kuua bila kukusudia lakini watu wasiomtanguliza Mungu wakaona ni vyema wawadanganye waTZ ili mtu wao muuaji atoke jela.Kuua bila kukusudia ni pale Jaji anpotoa hukumu ndio anaweza kuona kwamba kutokana na ushahidi uliotolewa mtuhumiwa aliuua bila kukusudia na sio katika process au ktk mwenendo wa mashitaka mtu anakurupuka eti huyu aliuua bila kukusudia how mwanasheria huyu alikula rushwa.

Kufa kwa JK sorry kufa kwa Ditto,ni majibu ya Mungu kwa kilio cha watanzani na mahabusu walioko magerezani kwa miaka dahari tena walioua kwa bahati mbaya kweli kuliko hata hii ya Ditto.

Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu.Mliojua mnajua sheria mtajiju,mliokula njama za kumtoa Ditto mmeula wachuya,Yaani mambo yamewaendea kombo mbwa nyie.

Mimi siamini na sitaki kuamini kwamba mtu akifa na maovu yake yanakwisha huu ni UNAFIKI.Ditto ni mdhambi tu,kwa killing ya makusudi.

JK hili ni fundisho kubwa sana kwako,uliambiwa Lowasa hafai ukalazimisha lakini Mungu amekuchapa Kiboko,Ukasimamia uharamia wa Ditto Mungu amekuchapa kiboko kingine,Ukaambiwa Chenge hafai amejiuzulu hicho nancho ni kiboko kingine.Kuwa msikivu kwa vilio vya wananchi wako.Wewe sio mbabe hata kidogo,kumbukeni Mungu ndio yuko mbele yenu,fanyeni kazi kwa kumpendeza yeye na sio vinginevyo.
 
Ktk dunia hii yetu hakuna aliyemkamilifu, mwenyezi mungu ampe pumziko lake kwa amani.
 
Unajua tuseme ukweli hiki kifo cha huyu "mtoto wa mjini" wengi tumekipokea kwa furaha sana.Hasa tukimkumbuka marehemu Mbonde.....Rest Not In Peace Ditto
 
Unajua tuseme ukweli hiki kifo cha huyu "mtoto wa mjini" wengi tumekipokea kwa furaha sana.Hasa tukimkumbuka marehemu Mbonde.....Rest Not In Peace Ditto

Afadhali wewe umesema kweli. Sisi wabongo unafiki umetuzidi.

Halafu suala la maisha baada ya kifo, hii ni imani ya mtu binafsi.
 
Dito alizidiwa akiwa kwenye tendo la ndoa hadi kufia kifuani kwa mkewe.

maji ya moto,
Tumefika huku??Mod ondoa hii please,hata kama ni muuaji ila jambo la kifo tusilifanyie mdhaha wa namna hii..
 
Pole kwa familia na jamaa wa marehemu. Safari ya Ditopile hapa dunia imefika mwisho na mwisho imefika!

Nakubaliana na wote wanaosema kuwa hakuna haja ya kuwa walafi hapa dunia kwa vile hatuondoki na kitu ila maua yanayowekwa juu ya makaburi yetu iliyakauke kwa kasi kubwa zaidi ya aliyekwa chini yake!

Naamini mafisadi wamenipata!

... jina la bwana lihimidiwe!
 
Blessed are the dead who die in the Lord from now on."that they may rest from their labors, for their deeds follow them!"
 
RIP Braza Dito,

Fundisho kwa wengine:

Kifo hakina cha "utoto wa mjini", kujua kula chapati na wala hakitishiwi bastola...
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom