Diplomasia ni dhana pana. Hata hivyo, huwezi kujigamba kwamba wewe ni Gwiji la Diplomasia usipozifahamu Diplomasia za Kinafiki na jinsi Diplomasia za Kinafiki zinavyofanya kazi!
Miaka kadhaa iliyopita hapa JF niliunga mkono serikali ya Tanzania kuwaachia Misri kutumia maji ya Mto Nile. Uungaji mkono huu ulimaanisha pia kuwakaripia Ethiopia waachane na mpango wao wa kujenga libwawa likuuuuubwa along Mto Nile wakati wenzao Misri hawana chanzo chochote cha maji cha maana zaidi ya Mto Nile!
Mbele ya jicho la kimataifa, ingeonekana Tanzania inataka Misri watumie Mto Nile "kadri wapendavyo" kwa sababu za kibinadamu!
Huo ndio unafiki wenyewe. Hiyo ndiyo Diplomasia ya Kinafiki yenyewe!
Hata hivyo, watu hawakunielewa na hivyo wakanipinga kweli kweli! Hawakunielewa kwa sababu watu hawafahamu Diplomasia za Kinafiki na jinsi zinavyofanya kazi!
Lakini wakati nilitaka jicho la kimataifa liamini kwamba Tanzania ingefanya hivyo kwa sababu za kibinadamu kv Misri hawana chanzo chochote cha maji cha maana zaidi ya Mto Nile, kumbe lengo langu ilikuwa ni kuibua mgogoro wa matumizi ya maji kati ya Misri ya Ethiopia!
Ndiyo, nilitaka tuibue mgogoro kati ya mataifa hayo mawili ambayo yanautegemea sana Mto Nile kuliko sisi tulio na vyanzo lukuki vya maji.
Nilikuwa naogopa sana mpango wa Ethiopia wa kujenga bwawa kubwa kwa ajili ya kuzalisha umeme. Hapa nazungumzia The Grand Ethiopian Renaissance Dam.
Enzi zile Tanzania ilikuwa kwenye amsha amsha ya hali na ari ya juu ya kugundulika kwa matrilioni ya mita za ujazo za Gesi Asilia kule Kusini mwa Tanzania.
Gesi ile niliiona na bado naiona ingeifanya Tanzania kuwa Giant katika uzalishaji na uuzaji wa umeme ukanda wa Afrika Mashariki. Tungekuwa na visionary leaders, gesi ile ingetufanya tuwe giant energy supplier in East Africa!!
Kwa Ethiopia kujenga libwawa likubwa kama lile, litakalokuwa na uwezo wa kuzalisha zaidi ya 6000MW za umeme; hilo ni tishio kubwa sana kwetu kwa biashara tarajiwa ya nishati ukanda huu!!!
Sikuona njia muafaka zaidi ya kuwachonganisha Wamisri na Waethiopia katika matumizi ya maji ya Mto Nile ili hatimae Ethiopia wasijenge bwawa!
HISTORIA imejirudia.
OKW BOBAN SUNZU ameleta hii thread kuhusu uwezekano wa Wachina kuipokonya Bandari ya Mombasa kama walivyofanya kule Sri Lanka!!! Habari inasema:
Chonde chonde... Kenya ni ndugu zetu! Kenya ni majirani zetu! Tusimame nao pamoja na tusimamame imara kupingana na Wachina kwa jaribio lolote la kutaka kuwanyang'anya ndugu zetu Bandari ya Mombasa!
Najua nyie Watanzania mlivyo na roho ya korosho! Najua mnavyopenda kuwatakia mabaya ndugu zetu Wakenya, lakini kwa hili, chonde chonde tusimame nao pamoja!!
Tutapigiwa makofi Afrika mzima na duniani kwa ujumla kwa sisi kusimama imara kuwapigania ndugu zetu Wakenya! Hata Wazungu wa nchi za Magharibi watatupigia makofi (Diplomasia ya Kinafiki) kwa sababu wasingependa kuona Mchina ana-take over!!
Au mnataka kuona Bandari ya Mombasa inayokuwa operated na Wachina at full efficiency huku ikipambana na Bandari ya Dar es salaam inayoendeshwa na Wamatumbi wenzetu ambao efficiency kwao ni msamiati mgumu?!
Tafakari!!
Miaka kadhaa iliyopita hapa JF niliunga mkono serikali ya Tanzania kuwaachia Misri kutumia maji ya Mto Nile. Uungaji mkono huu ulimaanisha pia kuwakaripia Ethiopia waachane na mpango wao wa kujenga libwawa likuuuuubwa along Mto Nile wakati wenzao Misri hawana chanzo chochote cha maji cha maana zaidi ya Mto Nile!
Mbele ya jicho la kimataifa, ingeonekana Tanzania inataka Misri watumie Mto Nile "kadri wapendavyo" kwa sababu za kibinadamu!
Huo ndio unafiki wenyewe. Hiyo ndiyo Diplomasia ya Kinafiki yenyewe!
Hata hivyo, watu hawakunielewa na hivyo wakanipinga kweli kweli! Hawakunielewa kwa sababu watu hawafahamu Diplomasia za Kinafiki na jinsi zinavyofanya kazi!
Lakini wakati nilitaka jicho la kimataifa liamini kwamba Tanzania ingefanya hivyo kwa sababu za kibinadamu kv Misri hawana chanzo chochote cha maji cha maana zaidi ya Mto Nile, kumbe lengo langu ilikuwa ni kuibua mgogoro wa matumizi ya maji kati ya Misri ya Ethiopia!
Ndiyo, nilitaka tuibue mgogoro kati ya mataifa hayo mawili ambayo yanautegemea sana Mto Nile kuliko sisi tulio na vyanzo lukuki vya maji.
Nilikuwa naogopa sana mpango wa Ethiopia wa kujenga bwawa kubwa kwa ajili ya kuzalisha umeme. Hapa nazungumzia The Grand Ethiopian Renaissance Dam.
Enzi zile Tanzania ilikuwa kwenye amsha amsha ya hali na ari ya juu ya kugundulika kwa matrilioni ya mita za ujazo za Gesi Asilia kule Kusini mwa Tanzania.
Gesi ile niliiona na bado naiona ingeifanya Tanzania kuwa Giant katika uzalishaji na uuzaji wa umeme ukanda wa Afrika Mashariki. Tungekuwa na visionary leaders, gesi ile ingetufanya tuwe giant energy supplier in East Africa!!
Kwa Ethiopia kujenga libwawa likubwa kama lile, litakalokuwa na uwezo wa kuzalisha zaidi ya 6000MW za umeme; hilo ni tishio kubwa sana kwetu kwa biashara tarajiwa ya nishati ukanda huu!!!
Sikuona njia muafaka zaidi ya kuwachonganisha Wamisri na Waethiopia katika matumizi ya maji ya Mto Nile ili hatimae Ethiopia wasijenge bwawa!
HISTORIA imejirudia.
OKW BOBAN SUNZU ameleta hii thread kuhusu uwezekano wa Wachina kuipokonya Bandari ya Mombasa kama walivyofanya kule Sri Lanka!!! Habari inasema:
Several other countries, from Argentina to Namibia to Laos, have been ensnared in a Chinese debt trap, forcing them to confront agonizing choices in order to stave off default. Kenya’s crushing debt to China now threatens to turn its busy port of Mombasa – the gateway to East Africa – into another Hambantota.
Chonde chonde... Kenya ni ndugu zetu! Kenya ni majirani zetu! Tusimame nao pamoja na tusimamame imara kupingana na Wachina kwa jaribio lolote la kutaka kuwanyang'anya ndugu zetu Bandari ya Mombasa!
Najua nyie Watanzania mlivyo na roho ya korosho! Najua mnavyopenda kuwatakia mabaya ndugu zetu Wakenya, lakini kwa hili, chonde chonde tusimame nao pamoja!!
Tutapigiwa makofi Afrika mzima na duniani kwa ujumla kwa sisi kusimama imara kuwapigania ndugu zetu Wakenya! Hata Wazungu wa nchi za Magharibi watatupigia makofi (Diplomasia ya Kinafiki) kwa sababu wasingependa kuona Mchina ana-take over!!
Au mnataka kuona Bandari ya Mombasa inayokuwa operated na Wachina at full efficiency huku ikipambana na Bandari ya Dar es salaam inayoendeshwa na Wamatumbi wenzetu ambao efficiency kwao ni msamiati mgumu?!
Tafakari!!