Dini zetu ni sehemu ya shida zetu za kiuchumi tulizonazo Afrika.

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
13,622
14,069
Dini zetu hizi mbili zilikuja na wakoloni (watesi) wetu. Viongozi wa dini waliishi nyumba na mtaa mmoja na wakoloni (watesi) wetu, walisali pamoja, walikula na kunywa pamoja na wakoloni. Waliwabariki kwenye kazi zao za utesi na uporaji wa rasilimali zetu, kuwaombea mema na afya tele na kubatiza watoto wao. Wakoloni na dini ilikuwa ni kitu kimoja kilekile.
Viongozi wa dini walibaki wakati wenzao wakoloni wanaondoka shingo upande kurudi ulaya ili sisi tupate Uhuru.
Maswali ni mengi, lakini Yale machache ni haya:
1. Je, viongozi wa dini walifurahi au kuchukia wakati wakoloni wanaondoka?
2. Je, viongozi wa dini walifurahi Waafrika kujitawala?
3. Uhusiano kati ya dini hizi na wakoloni uliisha baada ya uhuru?
4. Viongozi wa dini waliomba msamaha kwa Waafrika kwa kishirikiana na wakoloni waliopora mali, kuua watu wetu, tamaduni zetu, na kudumaza maendeleo yetu?

View: https://youtu.be/BpswhiyKqpg?si=3vx7bzuU2k5j-Uys
 
Dini zetu hizi mbili zilikuja na wakoloni (watesi) wetu. Viongozi wa dini waliishi nyumba na mtaa mmoja na wakoloni (watesi) wetu, walisali pamoja, walikula na kunywa pamoja na wakoloni. Waliwabariki kwenye kazi zao za utesi na uporaji wa rasilimali zetu, kuwaombea mema na afya tele na kubatiza watoto wao. Wakoloni na dini ilikuwa ni kitu kimoja kilekile.
Viongozi wa dini walibaki wakati wenzao wakoloni wanaondoka shingo upande kurudi ulaya ili sisi tupate Uhuru.
Maswali ni mengi, lakini Yale machache ni haya:
1. Je, viongozi wa dini walifurahi au kuchukia wakati wakoloni wanaondoka?
2. Je, viongozi wa dini walifurahi Waafrika kujitawala?
3. Uhusiano kati ya dini hizi na wakoloni uliisha baada ya uhuru?
4. Viongozi wa dini waliomba msamaha kwa Waafrika kwa kishirikiana na wakoloni waliopora mali, kuua watu wetu, tamaduni zetu, na kudumaza maendeleo yetu?

View: https://youtu.be/BpswhiyKqpg?si=3vx7bzuU2k5j-Uys

Ukifananisha mali iliyoporwa na wakoloni Tanzania na mali inayoporwa na serkali ya CCM tangu tulipopata uhuru ni kama vile wakoloni walitunza mali yetu. Wangefanya kama CCM miaka yote ya ukoloni tusingekuta kitu hata kimoja.
Kwa upande wa Imani, asilimia 99.9% ni unafiki tu. Imani imekuwa kama lifestyle tu. Kama kweli tungekuwa tunafuata mafundisho ya imani zetu, wote tungekuwa tunaipambania haki kama Gen z.
 
Ukifananisha mali iliyoporwa na wakoloni Tanzania na mali inayoporwa na serkali ya CCM tangu tulipopata uhuru ni kama vile wakoloni walitunza mali yetu. Wangefanya kama CCM miaka yote ya ukoloni tusingekuta kitu hata kimoja.
Kwa upande wa Imani, asilimia 99.9% ni unafiki tu. Imani imekuwa kama lifestyle tu. Kama kweli tungekuwa tunafuata mafundisho ya imani zetu, wote tungekuwa tunaipambania haki kama Gen z.
Gen Z wamefanya vile kwa kuwa wamefikishwa mwisho, wamebanwa hadi shimo la mwisho la mkanda wa suruali zao. Sisi hapa bado kidogo kufikia levels za Gen Z kwa kuwa Bado vijana wanazo bado njia mbadala za kupumulia kwenye ardhi vijijini kwao, uvuvi, bodaboda, migodini, umachinga horera na biashara holela popote na chochote. Siku ardhi ya wazi ikiisha, sehemu za kuvua zikijaa, sehemu ya kuegesha bodaboda ikijaa na migodini, bamdarini na umachinga ukawa na utaratibu maalum na ajira kukosekana utaona kivumbi zaidi ya Gen Z.
 
Back
Top Bottom