Dini na Siasa: Kuna tofauti kubwa kati ya Maaskofu wa Katoliki na akina Kakobe

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,840
141,763
Leo nimejifunza kitu kikubwa katika kuhusanisha dini na siasa kupitia maaskofu wa Kanisa Katoliki. Askofu Ruwaichi katika mahubiri yake kuanzia mwanzo hadi mwisho hakuzungumza hata sentensi moja iliyohusu siasa bali alijikita kwenye Injili.

Baada ya misa takatifu kukamilika wakati wa kusoma risala kwa mgeni wa heshima ndipo walau siasa kidogo ilionekana. Ninakumbuka wakati wa ule mgongano wa Kakobe na TRA siku ya ibada katikati ya mahubiri askofu Kakobe akaanza kuwashambulia maofisa wa TRA. Kadhalika wakati wa mgogoro wa Gwajima na Makonda ilikuwa ni katikati ya mahubiri askofu Gwajima alipoanza kumshambulia Makonda na karatasi aliyoiita ni cheti na kuanza kukisoma. Nawashauri hawa maaskofu wa Huduma za kiroho wajifunze kutoka Katoliki ibada ni lazima iheshimiwe na mambo ya siasa wayafanye baada ya ibada.

Kwa namna mahubiri ya Askofu Ruwaichi yalivyojaa hekima ya Mungu yalipelekea hata mgeni rasmi ambaye ni mwanasiasa kutumia zaidi maandiko ya Biblia katika salamu zake. Ahsante!
 
Leo nimejifunza kitu kikubwa katika kuhusanisha dini na siasa kupitia maaskofu wa Kanisa Katoliki. Askofu Luaichi katika mahubiri yake kuanzia mwanzo hadi mwisho hakuzungumza hata sentensi moja iliyohusu siasa bali alijikita kwenye Injili. Baada ya misa takatifu kukamilika wakati wa kusoma risala kwa mgeni wa heshima ndipo walau siasa kidogo ilionekana. Ninakumbuka wakati wa ule mgongano wa Kakobe na TRA siku ya ibada katikati ya mahubiri askofu Kakobe akaanza kuwashambulia maofisa wa TRA. Kadhalika wakati wa mgogoro wa Gwajima na Makonda ilikuwa ni katikati ya mahubiri askofu Gwajima alipoanza kumshambulia Makonda na karatasi aliyoiita ni cheti na kuanza kukisoma. Nawashauri hawa maaskofu wa Huduma za kiroho wajifunze kutoka Katoliki ibada ni lazima iheshimiwe na mambo ya siasa wayafanye baada ya ibada. Kwa namna mahubiri ya Askofu Luaichi yalivyojaa hekima ya Mungu yalipelekea hata mgeni rasmi ambaye ni mwanasiasa kutumia zaidi maandiko ya Biblia katika salamu zake. Ahsante!


Kila mtu Ana Uhuru wa kutoa maoni yake! Kwahiyo maoni yako yanaheahimiwa pia, lakini hiyo haaanishi kwamba Uko sahihi! Kila mahali Kuna taratibu zake, kwahiyo usilazimishe katoliki Na wengine waliookoka eti wafanane!
 
Mkuu ili Uwe askofu wa catholic kuna process nyingi za kupitia kuanzia elimu ya darasani, elimu ya dini, uwezo wa kupambanua na kufikiri mambo. Catholic huwi askofu kwa kujipa mwenyewe Kama wanavyojipa kina gwajima. Catholic wana process zao za kupata maaskofu
Nimekuelewa mkuu!
 
Back
Top Bottom