Dini Dini Dini Dini.....Sasa miye nimeanza kuboreka na hizi threads za dini, Je wewe?

Je, Sehemu ya Dini/Imani Ifungwe au Isifungwe hapa JF?!

  • Isifungwe

    Votes: 14 43.8%
  • Ifungwe

    Votes: 8 25.0%
  • Irekebishwe

    Votes: 10 31.3%

  • Total voters
    32
  • Poll closed .
Status
Not open for further replies.

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Wana JF, hivi imekuwaje, kila nikiamka threads za dini zinazidi kumiminika tu... na ingekuwa bora kweli kama hizi threads zingekuwa si za kukashifiana katika mambo haya ya imani kama inavyoonekana hivi sasa, maana kuna wengine katika mambo haya wanamisimamo mikali usiombe, kujadiliana nao ni kama kupoteza muda haswaa. Hivi sasa, mengi ninayo yasoma ni kuwa dini hii bora zaidi ya hii, dini hii ina mtume bora kuliko dini ile, sherehe hii haina maana kuliko sherehe ile, tukio hilo ni la uongo na hili ni la kweli... mimi nimeanza kuchoshwa na haya mambo. Hivi hawa watu ni WAUMINI wa dini kweli ambazo nyingi naamini zinataka uvumilivu, kusameheana na kufundishana yaliyo mema?!

Unajua nini, kama dini ndizo ziko hivi mimi bora nirudi kwenye dini za makwetu tu, dini za Kibantu kabla Afrika yetu haija vamiwa na wageni na kututawala. Mfano wa dini zile za akina Kinjeketile na akina Mwanamalundi... maana hizi ambazo naziona hazina asili ya Kibantu zinazidi kuandamana kila moja zidi ya nyingine katika kutafuta IMANI YA KWELI.

Kwa kweli ningependa kabisa forum ya dini iwepo kwa ajili ya kubadilishana mawaidha, kutafakari na kupashana habari kuhusiana na imani tulizo nazo, na wale wasio amini kitu basi kusoma habari za imani hizi na wao kuwa na maoni yao BILA KUTUKANANA.

Lakini kwa sasa hiyo sehemu ya dini imebadilika ghafla na kufanywa uwanja wa kugombania waumini. Kwa kweli miye naona hili si jema hapa JF. Hivyo basi naomba ushauri wenu kwa kupiga kura;

JE, SEHEMU YA DINI IFUNGWE ISIFUNGWE au Ifanyiwe marekebisho?!

Ukichagua IREKEBISHWE, naomba uendelee kutoa mawazo yako kwenye thread hii namna ya kufanya marekebisho hayo.

Nitamwomba Admin atengeneze Poll, ili tupige kura zetu kama hili linafaa.

Naomba kutoa hoja. Ahsanteni.

SteveD.
 
SteveD,

Kwa nini na wewe usimwage utirio wako? Kuhusu dini au lack of dini yako?
 
SteveD,

Kwa nini na wewe usimwage utirio wako? Kuhusu dini au lack of dini yako?

Pundit, ahsante kwa ombi lako. Ila linanifedhehesha kidogo maana sina 'utirio' wowote kuhusu dini, maana naamini dini ni imani na wengi wetu tunarithi au kufata dini kutokana na pahala tulipozaliwa. Sasa nikiwa naamini hiki halafu mwingine anakuja kuniambia yeye anaamini kile na chake ni bora zaidi, huu si ndiyo mwanzo wa mifarakano. Waliosema fahari wawili hawaishi zizi moja labda waliliona hili mapema.

Usinielewe vibaya Pundit, kwani naamini pia kufundishana kuhusu imani ya mtu au mtu kutoa habari kuhusu dini yake ni kitu ambacho naweza kusikiliza na nina kikubali pia. Lakini kilicho nipelekea mimi kusema labda sehemu ya dini ifungwe ni ule uelekeo wa mtu kuelezea dini yake unapotea haraka, badala yake Waumini hawa wanaanza kukashifu dini za wenzao katika kutetea zao, au basi tu kukashifu bila uelekeo wowote hali kila kilicho katika dini NAAMINI ni VITU VYA KUAMINIKA TU. Basi, hatuna budi kuonyesha kuwa tunaheshimu dini za wenzetu na wale ambao hawana dini hata kama tunaamini kutokana na mafundisho ya dini zetu kuwa WAKO KATIKA UPANDE WA MAKOSA au DINI YA MAKOSA.

SteveD.
 
SteveD,

You raise a very important point kuhusu kuheshimu didni za watu wengine. Heshima ni kitu cha bure an nisingependa kuona distractions kutokana na malumbano yasiyo na msingi.

Kuna msuguano mkali kati ya kuheshimu dini za watu na uhuru wa kujieleza.Kwa mfano, mimi ni "apatheist", siamini mungu wa "Judeo-Christian" religions, in fact kuamini hakuko katika msamiati wangu, you either know or you dont. And as far as I know there is no god.Nikiona watu wanatiana mchanga machoni kwa kulumbana kuhusu kitu ambacho mimi as far as I know hakipo, naona kuwakataza kuongea siyo solution kwa sababu kuongea ndiyo maana ya forum, mimi naona huu ni wakati mzuri na mimi kuchangia kuhusu my lack of belief.

Kwa hiyo ndiyo maana nikakwambia mwaga nondo zako.Ila tunataka facts tu, nimenotice kuweka jazba na unazi ni rahisi sana katika mambo ya dini na nafikiri hii ndiyo concern yako kubwa.Tunaweza kuwa na matatizo haya katika topic tofauti, hata siasa pia kwa hiyo kufungia topic za dini halitakuwa jambo la maana.Jambo la maana ni kukubaliana kuwa na standards za hali ya juu katika presentation za ideas zetu.They say the best government is no government, we should all learn to practice that.
 
Wana JF, hivi imekuwaje, kila nikiamka threads za dini zinazidi kumiminika tu... na ingekuwa bora kweli kama hizi threads zingekuwa si za kukashifiana katika mambo haya ya imani kama inavyoonekana hivi sasa, maana kuna wengine katika mambo haya wanamisimamo mikali usiombe, kujadiliana nao ni kama kupoteza muda haswaa. Hivi sasa, mengi ninayo yasoma ni kuwa dini hii bora zaidi ya hii, dini hii ina mtume bora kuliko dini ile, sherehe hii haina maana kuliko sherehe ile, tukio hilo ni la uongo na hili ni la kweli... mimi nimeanza kuchoshwa na haya mambo. Hivi hawa watu ni WAUMINI wa dini kweli ambazo nyingi naamini zinataka uvumilivu, kusameheana na kufundishana yaliyo mema?!

Unajua nini, kama dini ndizo ziko hivi mimi bora nirudi kwenye dini za makwetu tu, dini za Kibantu kabla Afrika yetu haija vamiwa na wageni na kututawala. Mfano wa dini zile za akina Kinjeketile na akina Mwanamalundi... maana hizi ambazo naziona hazina asili ya Kibantu zinazidi kuandamana kila moja zidi ya nyingine katika kutafuta IMANI YA KWELI.

Kwa kweli ningependa kabisa forum ya dini iwepo kwa ajili ya kubadilishana mawaidha, kutafakari na kupashana habari kuhusiana na imani tulizo nazo, na wale wasio amini kitu basi kusoma habari za imani hizi na wao kuwa na maoni yao BILA KUTUKANANA.

Lakini kwa sasa hiyo sehemu ya dini imebadilika ghafla na kufanywa uwanja wa kugombania waumini. Kwa kweli miye naona hili si jema hapa JF. Hivyo basi naomba ushauri wenu kwa kupiga kura;

JE, SEHEMU YA DINI IFUNGWE ISIFUNGWE au Ifanyiwe marekebisho?!

Ukichagua IREKEBISHWE, naomba uendelee kutoa mawazo yako kwenye thread hii namna ya kufanya marekebisho hayo.

Nitamwomba Admin atengeneze Poll, ili tupige kura zetu kama hili linafaa.

Naomba kutoa hoja. Ahsanteni.

SteveD.


Steve, thanks for this thread. Ninachopenda kukwambia ni kuwa pamoja na kashfa na matusi yanayomiminwa bado kuna elimu wasomaji wanapata kitu ambacho ni muhimu zaidi kuliko matusi. Pia moto ya JF inasema its where we dare to talk openly (bila shaka ndo maana kuna wachangiaji hulipuka kwa matusi ya nguoni dhidi wa watoa hoja).

Mwisho ni kuwa kuchangia au kutochangia ni uamuzi wa mtu mwenyewe kwa hiyo its up to you; unaweza ukapitia tu kusoma na kupata ufahamu na hekima za wenye hekima pia kujia characters za ufuasi wa Imani.
 
SteveD,

As a side "smrtazz" comment, "kuboreka" katika kiswahili cha lahaja ya KiMkapa at least ni "to get better" from the root "bora"

Kwa hiyo the irony is one can actually spin your topic heading to mean you are being educated by these threads :)
 
SteveD,

As a side "smrtazz" comment, "kuboreka" katika kiswahili cha lahaja ya KiMkapa at least ni "to get better" from the root "bora"

Kwa hiyo the irony is one can actually spin your topic heading to mean you are being educated by these threads :)

Duuh, hiyo mbona itakuwa spin positive, lakini tu iwapo hakutakuwa na kashifa ndani yake! Ahsante kwa ku point hili.

SteveD
 
Wana JF, hivi imekuwaje, kila nikiamka threads za dini zinazidi kumiminika tu... na ingekuwa bora kweli kama hizi threads zingekuwa si za kukashifiana katika mambo haya ya imani kama inavyoonekana hivi sasa, maana kuna wengine katika mambo haya wanamisimamo mikali usiombe, kujadiliana nao ni kama kupoteza muda haswaa. Hivi sasa, mengi ninayo yasoma ni kuwa dini hii bora zaidi ya hii, dini hii ina mtume bora kuliko dini ile, sherehe hii haina maana kuliko sherehe ile, tukio hilo ni la uongo na hili ni la kweli... mimi nimeanza kuchoshwa na haya mambo. Hivi hawa watu ni WAUMINI wa dini kweli ambazo nyingi naamini zinataka uvumilivu, kusameheana na kufundishana yaliyo mema?!

Unajua nini, kama dini ndizo ziko hivi mimi bora nirudi kwenye dini za makwetu tu, dini za Kibantu kabla Afrika yetu haija vamiwa na wageni na kututawala. Mfano wa dini zile za akina Kinjeketile na akina Mwanamalundi... maana hizi ambazo naziona hazina asili ya Kibantu zinazidi kuandamana kila moja zidi ya nyingine katika kutafuta IMANI YA KWELI.

Kwa kweli ningependa kabisa forum ya dini iwepo kwa ajili ya kubadilishana mawaidha, kutafakari na kupashana habari kuhusiana na imani tulizo nazo, na wale wasio amini kitu basi kusoma habari za imani hizi na wao kuwa na maoni yao BILA KUTUKANANA.

Lakini kwa sasa hiyo sehemu ya dini imebadilika ghafla na kufanywa uwanja wa kugombania waumini. Kwa kweli miye naona hili si jema hapa JF. Hivyo basi naomba ushauri wenu kwa kupiga kura;

JE, SEHEMU YA DINI IFUNGWE ISIFUNGWE au Ifanyiwe marekebisho?!

Ukichagua IREKEBISHWE, naomba uendelee kutoa mawazo yako kwenye thread hii namna ya kufanya marekebisho hayo.

Nitamwomba Admin atengeneze Poll, ili tupige kura zetu kama hili linafaa.

Naomba kutoa hoja. Ahsanteni.

SteveD.

Kuna tetesi nimezisikia kuwa kuna watu wanapeleka matusi kule kwenye thread za dini ili thread ifungwe... Nadhani kampeni zao kama zinataka kufanikiwa vile...! Mhh ni tetesi tu...!

Lakini kwani lazima usome thread za dini weyeee, un'tafuta nini kule...weyeee, uwachi mambo yako?!

Kila siku siasa... siasa... siasa...! Hamchoki na siasa zenu za Kiafrika... mbona hatuoni uadirifu wowote ule... Vyama vyote vina kashfa... ubadhirifu wa mali za chama, viongozi wanakula ruzuku, ufisadi, uzinifu tena kwa viongozi wakuu, yaani wenyeviti na makatibu wao... Aaah yaani mi nimichoka kabisa na siasa, kwa wanachama ndo usiseme kila siku ugofi... i mean UGOMVI... Mhhh mi chichemi chana...!

Dawa si kufunga thread, utakuwa umewanyima Haki yao wanachama wa JF. Kinacho takiwa ni kuanisha tu kile ambacho ni matusi, kisiwepo na atakaye tukana basi aonywe na kama hakusikia afungiwe yeye na si Thread usika...! Kashfa? Mmmh kashfa lazima ziwepo.. Oooh! Ndio kwani kashfa maana yake ni ukweli uliofichwa, Ukisema X-Paster nimekukashifu ina maana nimetoa kweli yako ulioificha, kweli ambayo hutaki watu waijue...! That's Kashfa kwa kiswahili... Wengine wanasema scandal...!

Kwa Waislam ukisema kuwa Yesu ni Mwana wa mungu, ni matusi si kashfa kwao. Unakuwa umemkosea Mungu wao... Lakini hawawezi kulalamika kwenye vyombo vya habari kuwa wametukaniwa Mungu wao kuwa ana mtoto. Kwani wamefundishwa kuwa wavumilifu na dini na watu wa imani nyingine. Lakini kwa wakristo Wakisikia kuwa Yesu si Mwana wala si mungu kwao ni kashfa kubwa na watataka mpaka serikali iingilie kati...! Watalalamika weeee! Mkapa thread..o Ohoo!, yaani wata-la-la-mi-ka mpaka thread ifungwe roho ziwe kwatu...!
Kwani unafikiri Ukisema kuwa Mungu Hayupo watu wa dini hawaumii... wanaumia kama vile watu wasio amini kuwepo kwa M'Mungu wanavyo waona kuwa kuamaini Mungu ni Kasumba...!

Ngoja nikunong'oneze kidogo... ila usiseme kwa ntu yoyote...
"Nimisikia tetesi ku- ku-kuwa-kuwa ete eti kule kwenye mambo mambo yenu yale, yale ya chumbani kule, Mambo Ya Kikubwa uelewi tu... sasa kuna kukuna watu wan'taka yafungiwe yale pia, eti eti ni kinyume na maadili ya Taifa letu changa... si Unajuwa Taifa la Bongo bado ntoto n'dogo tu. Sasa unafikiri raia watakuwaje. Ndo mana maakili yao bado... Yaani ngono, ngono tu. Wakiona mwana'nke tu wanafikiria chumbani, tena basi chitandani kabsaaaa....! Mi nimichoka kabisa..." uchicheme wakakuchikia Oooh!

Tuwe wavumilifu, tutumie Hikma na Busara... Jazba Hazisaidii wala hazitatusaidia kitu zaidi ya kueneza chuki miongoni mwetu...

Nawomba kuwakirisha mahoja ya kwangu...

Wafungiwe tu wenye mitusi wasiotaka kuheshimu Dini na imani za watu wengine. Ahsantu
 
XP you have a point. Migongano na kashfa inaweza kutokea kwenye thread yoyote, kwa hiyo tusiweke mtego wa panya utakaonasa waliokuwamo na wasiokuwamo.Kama kuna mtu analeta matusi aonywe na kufungiwa mwenyewe. Kuna watu wengine wana-enjoy discussion za kila level na topic watanyimwa uwanja wa ku-discuss matters of faith.
 
Mr steve umeongea kitu cha msingi ni lazima ukumbuke kuwa hukuna kitu cha kuongelea kwa makini katika jamii kama dini. Unaweza ukakusanya dunia yote ikafika Tosamaganga.. Weka kichwani dini ni pombe ya roho!!!!!!!!
Lenin asawahi kusema 'religion is the opium of the oppressed'
 
Duuh, hiyo mbona itakuwa spin positive, lakini tu iwapo hakutakuwa na kashifa ndani yake! Ahsante kwa ku point hili.

SteveD

StevenD,

Hapa kuna tatizo lingine umeli-raise. Unajua kuwa hata huku mitaani yanatokea malumbano ya dini. Na upande mmoja ukielemewa, wkt mwingine hukimbilia mahakamani kwa madai kuwa wamekashifiwa dini yao. Sasa, wafikapo huko, wanashindwa kutoa definition ya kisheria khs "kashfa", na hivyo kushindwa kuyatetea madai yao. Labda, ndugu SteveD, unaweza kutufafanulia khs kashfa, as far as JF rules are concerned.

Sishabikii matusi na lugha chafu. La hasha! Ni kuwekeana tu utaratibu mzuri ili mwisho wa siku tusisahau kuwa Mungu "wetu" ndiye Aliyewaumba na wengine wasiokuwa "sisi". O/wise huyo si "Mungu" wa kweli.
 
Steve naungana na wewe,
Mtu anapofungua kusoma thread ya dini anatarajia kuelimishwa/kuelimika juu ya jambo fulani,
kitu lilinichosha kwenye hizi thread za dini, wanazungumzia Ukristu VS Uislam tuuuuuu, na nyingi kati ya hizo thread ni za chuki na matusi, kwa wale ambao familia ni mchanganyiko, baba mkristu Vs Mama mwislamu na vice versa, hii inakwaza kidogo.

Na utakuta mtu anapost thread ile ile kuibadilisha heading zaidi ya mara tatu (mfano siku ya christmas), anamaanisha nini??
Sioni kama imani aka dini nyingine zinazungumziwa hapa, bahai, budha, etc.

.
 
Nafikiri si vema watu kama wana NIA ya kuwaita wengine ktk DINI yao basi watumie Lugha nzuri. na kama ingalikuwa tunaonana Face to face basi Hata SURA zetu zilihitaji kuonesha bashasha.

Wengi wanaojadili mambo ya DINI si wasomi wa mambo ya DINI ila wachache, na wanavutwa na HISIA au walivyorithi au alivyopokea. Ni ukweli kwa mtu yoyote ukimuonesha anacho-AMINI sicho sahihi ataanza kuwa na HASIRA na kama anauwezo wa KIMAMLAKA anaweza chukua hatua kali ili tu asiendelee kusikia hayo maneno. MFANO leo hi china hawataki kusikia DINI yoyote. na wengine utasikia DINI moja ina fanya kila iwezalo kustopisha growth ya DINI ingine.

Hawa mitume tunaowafuata wote walikuwa na approach nzuri. Sisi wa sasa tumekosa methodology ya kufikisha ujumbe. Hata kama ni kweli unachozungumza lkn hutoweza kuwavuta wengine. na Ndio maana baadhi ya watu wanaamua hata kanisani au msikitini wasiende kutokana na aproach....Zipo Hadithi za mitume ambazo zinaonesha namna gani wao walivyoweza fikisha ujumbe ktk Jamii iliyokuwa INAABUDU MASANAMU...
KTK BIBLIA na QURAN imefahamishwa kuwa watu wawaite wengine ktk DINI yao kwa LUGHA LAINI. Mtume MUSSA alipkwenda kwa FIRAUNI akaambiwa nenda kwa farao ukazungumze nao lugha laini huenda akakusikiliza...au akaingiwa na KHOFU/WOGA
 
Sasaaaa.. hii thread si ihamishiwe kule kwenye mambo ya dini... huku mbona kama imejificha, nadhani itakuwa busara ikiunganishwa kule na waumini na wasio waumini wakapata nafasi nzuri ya kuchangia, maana si wote wenye kuperuzi kurasa za JF. Kuna watu wakiingia humu yaani break ya kwanza kwenye kurasa za Dini, kama ilivyo wengine kwenye siasa.

Wahusika tafadharini... kama inawezekana basi ipelekwe kunako husika na wahusika wakaweza kutoa maoni yao.
Ahsante
 
Sasaaaa.. hii thread si ihamishiwe kule kwenye mambo ya dini... huku mbona kama imejificha, nadhani itakuwa busara ikiunganishwa kule na waumini na wasio waumini wakapata nafasi nzuri ya kuchangia, maana si wote wenye kuperuzi kurasa za JF. Kuna watu wakiingia humu yaani break ya kwanza kwenye kurasa za Dini, kama ilivyo wengine kwenye siasa.

Wahusika tafadharini... kama inawezekana basi ipelekwe kunako husika na wahusika wakaweza kutoa maoni yao.
Ahsante

X-PASTER,
Ahsante kwa wazo lako, ila naona kama kuhamishwa ni bora ipelekwe kwenye sehemu ya mapendekezo/maoni maana ni thread ya maoni na siyo ya dini kama jinsi nilivyo ianzisha. Pia ilibidi kuiweka hapa kutokana na forum ya polls kuwepo hapa.
Labda kuweka link tu kule kwenye dini ili watu watembelee..

SteveD.
 
Wana JF, hivi imekuwaje, kila nikiamka threads za dini zinazidi kumiminika tu... na ingekuwa bora kweli kama hizi threads zingekuwa si za kukashifiana katika mambo haya ya imani kama inavyoonekana hivi sasa, maana kuna wengine katika mambo haya wanamisimamo mikali usiombe, kujadiliana nao ni kama kupoteza muda haswaa. Hivi sasa, mengi ninayo yasoma ni kuwa dini hii bora zaidi ya hii, dini hii ina mtume bora kuliko dini ile, sherehe hii haina maana kuliko sherehe ile, tukio hilo ni la uongo na hili ni la kweli... mimi nimeanza kuchoshwa na haya mambo. Hivi hawa watu ni WAUMINI wa dini kweli ambazo nyingi naamini zinataka uvumilivu, kusameheana na kufundishana yaliyo mema?!

Unajua nini, kama dini ndizo ziko hivi mimi bora nirudi kwenye dini za makwetu tu, dini za Kibantu kabla Afrika yetu haija vamiwa na wageni na kututawala. Mfano wa dini zile za akina Kinjeketile na akina Mwanamalundi... maana hizi ambazo naziona hazina asili ya Kibantu zinazidi kuandamana kila moja zidi ya nyingine katika kutafuta IMANI YA KWELI.

Kwa kweli ningependa kabisa forum ya dini iwepo kwa ajili ya kubadilishana mawaidha, kutafakari na kupashana habari kuhusiana na imani tulizo nazo, na wale wasio amini kitu basi kusoma habari za imani hizi na wao kuwa na maoni yao BILA KUTUKANANA.

Lakini kwa sasa hiyo sehemu ya dini imebadilika ghafla na kufanywa uwanja wa kugombania waumini. Kwa kweli miye naona hili si jema hapa JF. Hivyo basi naomba ushauri wenu kwa kupiga kura;

JE, SEHEMU YA DINI IFUNGWE ISIFUNGWE au Ifanyiwe marekebisho?!

Ukichagua IREKEBISHWE, naomba uendelee kutoa mawazo yako kwenye thread hii namna ya kufanya marekebisho hayo.

Nitamwomba Admin atengeneze Poll, ili tupige kura zetu kama hili linafaa.

Naomba kutoa hoja. Ahsanteni.

SteveD.

steve d, ukiangalia kiundani hapa jf utaona hakuna sehemu inayokashifu kama ukumbi wa siasa, watu wanaongelea mpaka private life za viongozi aidha wa vyama fulani ama serikali.na pia kuna vita vikali baina ya chadema na ccm. elewa kwamba sometime msimamo wako ni kashfa kwa mwenzio.kitu kizuri ni kwamba katika kashfa hizo (kutofautiana kimsimamo) kuna wale neutral au wale ambao wamefuata mkumbo bila kuelewa, huwa wanaelimika na kubadilika kutoka fiction na kwenda kwenye real aspect ya msimamo wao mpya.hilo nililoongea hapo juu ni porojo
in short sidhani kama ni solution kuufunga ukumbi wa dini, the only solution ni admin kufanya kazi ya kubann kila anaevuka maadili ya forum hii. hata miskitini na makanisani wanaokwenda sio wote ni waumini wengine ni wababaishaji tu lakini solution sio kufunga msikiti wala kanisa , solution ni kuwafahamisha.hakuna alokamilika isipokuwa mmoja tu(kwa mimi ninaeamini mungu)
shukran
 
Tatizo kubwa kwenye Dini ni kashfa kati ya dini moja na ingine

wengine wanasema siasa kuna kashfa ni kweli lakini dini ni kitu tofauti na siasa ndio maana utasikia mrema leo yupo hapa kesho kule. Lakini hutasikia akihama dini kila wakati y?

1. Rule of laws zinaanzia kwenye dini maana kama unamwamini Mungu na kushika amri zake bila kufuatwa na polisi, Atashindwaje sheria za nchi....

2. Dini gives life meaning (respect of life) maana Mungu ndio mwenye uhai na ukitenda vinginevyo basi kuna hukumu so watu wanaheshimu (maana ipo kwenye dini zote) ingawa hawajui fate yake.

3 N.K
Ninachotaka kusema ukidharau au kukashfu dini ya mtu mwingine madhara yake ni makubwa kuliko chama au individual therefore Moderotors wanaohusika na dini wawe makini zaidi kwenye kuhakikisha kashfa haziwepo.

Kutofautiana kiitikadi za kidini sio kashfa, lakini kutusi, kukejeli, na maneno ya kukashfu ndio tatizo hapa
 
StevenD,

Hapa kuna tatizo lingine umeli-raise. Unajua kuwa hata huku mitaani yanatokea malumbano ya dini. Na upande mmoja ukielemewa, wkt mwingine hukimbilia mahakamani kwa madai kuwa wamekashifiwa dini yao. Sasa, wafikapo huko, wanashindwa kutoa definition ya kisheria khs "kashfa", na hivyo kushindwa kuyatetea madai yao. Labda, ndugu SteveD, unaweza kutufafanulia khs kashfa, as far as JF rules are concerned.

Sishabikii matusi na lugha chafu. La hasha! Ni kuwekeana tu utaratibu mzuri ili mwisho wa siku tusisahau kuwa Mungu "wetu" ndiye Aliyewaumba na wengine wasiokuwa "sisi". O/wise huyo si "Mungu" wa kweli.

Niliomba kupewa tafsiri ya "kashfa", lilikuwa ni direct swali kwa SteveD, lkn haikuwa na maana kuwa wengine wasingeweza kuchangia! Vinginevyo tutakuwa tukijadili kitu tusichokijua.
 
Kuna jambo moja ambalo naona linaangaliwa tofauti. Kufikiria dini inajengwa kwenye misingi ya imani tu sio sahihi. Ni kweli imani ni moja wapo ya sababu za msingi, lakini kufiri/tafakari (reasoning) pia ni muhimu sana. It is a mixture of reasoning and faith ndio inatufanya tusima huku au kule, tuhamie huku au kule. Watu tumezaliwa na kukuta labda tuko kwenye dini hii au ile. Lakini hili halituzuii sisi kama binadamu kutafuta na kujua ukweli, machimbuko na sababu za imani zetu. Imani bila reasoning ndio haswa unavyotakiwa kuwa uhusiano na Mungu (hii ni ngumu sana hasa katika changamoto mbali mbali za siku hzi). Lakini kwa wengi wetu kwa kutumia reasoning tunaweza kuelewa zaidi na hivyo kukazia imani zetu.

Kwa upande wangu thread za dini nizamuhimu sana hapa JF, hasa zile zinazojenga utambuzi wa sababu za kuwa katika dini tulizopo, na zinazo tusaidia katika reasoning. Ni vuziri sana tukakumbushwa mara kwa mara sababu hizo ili tusipoteze imani zetu. Kama tunavyo kumbushana kuhusu nini maana ya kuwa Mtanzania na kupigania ili Utanzania wetu usipotee, sioni kwa nini tushindwe kufanya hivyo kuhusu dini zetu.

Kwa namna moja au nyingine uelewa wetu wa kimaadili umejengeka sana katika misingi ya dini zetu (hata za mababu zetu). ambazo zinajega msingi kwa jamii iliyo bora na ambayo kwa kiasi fulani kuna kipimo kinachokubalika (yard stick) cha mema na mabaya. Kwa hiyo nashauri tena Threads za dini zenye malengo ya kutukuza kiimani, kutuhabarisha kuhusu dini na kutufufua kiimani zina nasafi kubwa sana JF kama tunataka Tanzania yenye maadili. Tanzania ya watanzania ambao kwa imani (dini) zao tafauti wanajali maslahi ya taifa letu

Waliyosema wengine kuhusu kashfa zinazoingiza mambo ya dini au kashfa kwa dini nyingine hizo hazitakiwi kabisa kuwa na nafasi JF.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom