Steve Dii
JF-Expert Member
- Jun 25, 2007
- 6,403
- 1,241
Wana JF, hivi imekuwaje, kila nikiamka threads za dini zinazidi kumiminika tu... na ingekuwa bora kweli kama hizi threads zingekuwa si za kukashifiana katika mambo haya ya imani kama inavyoonekana hivi sasa, maana kuna wengine katika mambo haya wanamisimamo mikali usiombe, kujadiliana nao ni kama kupoteza muda haswaa. Hivi sasa, mengi ninayo yasoma ni kuwa dini hii bora zaidi ya hii, dini hii ina mtume bora kuliko dini ile, sherehe hii haina maana kuliko sherehe ile, tukio hilo ni la uongo na hili ni la kweli... mimi nimeanza kuchoshwa na haya mambo. Hivi hawa watu ni WAUMINI wa dini kweli ambazo nyingi naamini zinataka uvumilivu, kusameheana na kufundishana yaliyo mema?!
Unajua nini, kama dini ndizo ziko hivi mimi bora nirudi kwenye dini za makwetu tu, dini za Kibantu kabla Afrika yetu haija vamiwa na wageni na kututawala. Mfano wa dini zile za akina Kinjeketile na akina Mwanamalundi... maana hizi ambazo naziona hazina asili ya Kibantu zinazidi kuandamana kila moja zidi ya nyingine katika kutafuta IMANI YA KWELI.
Kwa kweli ningependa kabisa forum ya dini iwepo kwa ajili ya kubadilishana mawaidha, kutafakari na kupashana habari kuhusiana na imani tulizo nazo, na wale wasio amini kitu basi kusoma habari za imani hizi na wao kuwa na maoni yao BILA KUTUKANANA.
Lakini kwa sasa hiyo sehemu ya dini imebadilika ghafla na kufanywa uwanja wa kugombania waumini. Kwa kweli miye naona hili si jema hapa JF. Hivyo basi naomba ushauri wenu kwa kupiga kura;
JE, SEHEMU YA DINI IFUNGWE ISIFUNGWE au Ifanyiwe marekebisho?!
Ukichagua IREKEBISHWE, naomba uendelee kutoa mawazo yako kwenye thread hii namna ya kufanya marekebisho hayo.
Nitamwomba Admin atengeneze Poll, ili tupige kura zetu kama hili linafaa.
Naomba kutoa hoja. Ahsanteni.
SteveD.
Unajua nini, kama dini ndizo ziko hivi mimi bora nirudi kwenye dini za makwetu tu, dini za Kibantu kabla Afrika yetu haija vamiwa na wageni na kututawala. Mfano wa dini zile za akina Kinjeketile na akina Mwanamalundi... maana hizi ambazo naziona hazina asili ya Kibantu zinazidi kuandamana kila moja zidi ya nyingine katika kutafuta IMANI YA KWELI.
Kwa kweli ningependa kabisa forum ya dini iwepo kwa ajili ya kubadilishana mawaidha, kutafakari na kupashana habari kuhusiana na imani tulizo nazo, na wale wasio amini kitu basi kusoma habari za imani hizi na wao kuwa na maoni yao BILA KUTUKANANA.
Lakini kwa sasa hiyo sehemu ya dini imebadilika ghafla na kufanywa uwanja wa kugombania waumini. Kwa kweli miye naona hili si jema hapa JF. Hivyo basi naomba ushauri wenu kwa kupiga kura;
JE, SEHEMU YA DINI IFUNGWE ISIFUNGWE au Ifanyiwe marekebisho?!
Ukichagua IREKEBISHWE, naomba uendelee kutoa mawazo yako kwenye thread hii namna ya kufanya marekebisho hayo.
Nitamwomba Admin atengeneze Poll, ili tupige kura zetu kama hili linafaa.
Naomba kutoa hoja. Ahsanteni.
SteveD.