Clark boots
JF-Expert Member
- Jun 5, 2017
- 6,393
- 5,518
01': Mechi ya Yanga vs Kagera Sugar imeanza hivi punde
04': Haji Mwinyi anarusha mpira kuelekea lango la Kagera baada ya kutolewa, anauchukua Ajib, Ajib anapasia langoni mwa wapinzani, wanaokoa
05': Kagera sasa, anao Atupele Green, pasia pembeni mwa Uwanja, hatariii, Kagera wanakosa nafasi ya wazi
07': Rostand anaanzisha goli kiki, ni baada ya mpira kutoka nje
08: Buswiiiita, namna gani hapa, krosi yake inakwenda nje, ilikuwa ni pasi nzuri ya auta kutoka kwa Ajib
12': Matokeo ni 0-0 mpaka sasa
13': Hatari katika lango la Kagera hapa, Buswiita, anababatizana na mlinda mlango, anaudaka
14': Mpira umesimama baada ya kipa wa Kagera kuumia, Cannavaro naye anapasha nje
15': tayari mpira umeshaanza, kwake Kamusoko, anapiga shuti lakini linatoka nje
16': Offside, Kagare wanaotea, mpira unapigwa kuelekea kwao
18': Kibaya anapata kadi ya njano, ni ya kwanza kwenye mchezo wa leo
19': Faulo, kadi ya pili ya njano inaenda kwa mchezaji wa Kagera, ni baada ya kucheza faulo eneo la hatari, inapigwa langoni mwao
20': Ajib yuko na mpira, anapigaaa, inapiga nyavu za juu
21': Ngonyani naye anapata kadi ya njano baada ya kucheza mazambi, ni ya tatu sasa katika mchezo huu
21': Matokeo ni 0-0
22': Mpira umesimama, Maxime anatoa maelekezo kwa wachezaji wake
23': Fhaki anapiga hapa, hatari langoni mwa Yanga, namna gani mshambuliaji huyu anashindwa kutumia nafasi
25': Kavila anamchezea rafu Chirwa hapa, inakuwa faulo kwenda Kagera
25': Ally Nasoro sasa anaondoka nao kupandisha mashambulizi, anapiga pasi mkaa, anaokoa Yondani
26': Wanaanza Yanga eneo la nyuma, Kessy anampasia Buswita, kwake Kamusoko, Kamusoko anapiga kwake Pato lakini beki wa Kagera anautoa na mpira unakuwa wa kona
28': Mpira anao Kamusoko, anapasia nyuma kwake Yondani, Yanga wanajaribu kutafuta bao hapa
29': Emmanuel Martin, anacheza faulo, mpira unapigwa kuelekea Yanga
30': matokeo ni 0-0, mpaka sasa hakuna timu iliyofanya shambulizi la kutisha kwa mwenzake
31': Goli Kiki upande wa Yanga, unapigwa kuelekea Kagera
32': Kagera waanzisha goli kiki, tayari ushapigwa, faulo, unapigwa kuelekea Kagera
33': Mabadiliko Yanga wanafanya mapema, anatoka Pato na nafasi yake inachukuliwa na Maka
35'; Kagera wanapata kona ya kwanza baada ya Mwinyi Haji kuutoa mpira, inapigwaaa, inapigwa kichwa na mshambuliaji wa Kagera lakini kipa Rostand anadaka
37': Unarushwa sasa kuelekea lango la Kagera, anao Ajib sasa, kwake Martin, unapigwa kwake Buswita, anautuliza kwa njia ya kifua lakini beki wa Kagera anaokoa
39': Anao sasa Ajib, unapigwa langoni, kipa anajitutumua anaupiga na mkono unakuwa wa kurushwa kuelekea langoni kwake, kidogo iwe kona
41': Faulo, Ajib anapiga, anapiga ya chinichini lakini mabeki wanaokoa kwa kichwa
41': Mpira uko mbele sasa upande wa kulia mwa uwanja wanao Yanga, beki wa Kagera anauokoa hapa, unapigwa mbele lakini Maka anautoa nje
Mpira ni mapumziko sasa, Yanga 0-0 Kagera Sugar
45': Kipindi cha pili kimeanza, matokeo ni 0-0
46': Beki wa Kagera anachezewa faulo, mpira unapigwa kuelekea langoni mwa Yanga
47': Hatarii langoni mwa Yanga, Atupele Green anakosa kupiga shuti nje kidogo mwa eneo la hatari, ni faulo,
48': Inapigwaaa, inatoka nje sentimita kadhaa tu, bahati nyingine wanaikosa Kagera Sugar,
50': Yanga wanaanza nyuma taraatibu, beki wa Kagera anautoa nje
51': Penatiiii, Yanga wanapata tuta hapa
51': Ajib ndiyo anapiga tuta, anapigaaa, gooooooli, Yanga wanapata bao la kwanza, sasa ni 1-0
53': Kagera wanaanza upya kati, wanapasiana kuelekea langoni mwa Yanga, inapigwa moja juu, kipa Rostand anaruka kama nyani anaudaka
55': Kagera wamezidi kuamka licha ya kufungwa bao hilo moja, wanamiliki zaidi mpira eneo la kati
57': Ajib sasa na mpira, piga huku pembeni lakini Kagera wanaokoa, inapigwa mbele hukuu, offside
59': Namna gani Kagera wanakosa tena bao hapa, ni nafasi adhimu kabisa hii ndani ya eneo la hatari mwa Yanga, mpira unakwenda nje
61': Kagera wanaanza mashambulizi tena, wanapasiana eneo la nyuma
63': Faulo inapigwa kuelekea Kagera baada ya beki wake kucheza mazambi
64': Yanga wanao mpira hivi sasa, Ajib anajaribu kuzunguka lakini ananyang'anywa mpira, Kamusoko anauwahi
65': Mpira anao Fhaki sasa, pasia kati ya uwanja huku, unarejeshwa kwake Fakhi tena, Kagera bado wanaumiliki, pigwa huku langoni mwa Yanga, offside
68': Kagera wanashindwa kutumia vema nafasi ya kufunga baada ya kupasiana vizuri na kuingia eneo la hatari la Yanga
69': Kona wanapata Yanga, ni ya nne na tano katika mchezo wa leo, Ajib anapiga lakini inaokolewa
70': Chirwaa, anapiga krosi moja ya hewani lakini inatoka nje
71': Mpira umesimaa kidogo, mchezaji wa Kagera ameumia
72': Omary Daga anaingia kuchuka nafasi ya Atupele Green, matokeo bado ni 1-0
75': Yanga wanapata kona, inapigwa na Ajib, pigwa huku Chirwa anapiga kichwa lakini inaenda pembeni, Kagera wanaokoa
75': Emmanuel Martiiiin, anapigaaaa, kipa wa Kagera anakuwa mahiri anaokoa
76': Goooooooli, Martin anaifungia Yanga bao la pili kufuatia krosi nzuri ya Obrey Chirwa, Yanga wana mabao mawili sasa na Kagera 0
79': Yanga wameamka sasa, wanakwenda mbele na mpira, kona! Ajib yu tayari kupiga, anaanza fupi hukuuu, kona nyingine, ni ya 7 sasa, inapigwaaaa, Kagera wanaokoa
81': Kagera wanapata kona pia, inapigwaaa lakini inaokolewa
82': Kagera wanaumiliki mpira tena, wanajaribu kutafuta bao angalau la kufutia machozi
83': Hatari langoni mwa Kagera, kipa anadaka, anaanza taratibu na wenzake nyuma
85': Kagera wanapata kona hapa, inapigwa lakini inatolewa na kuwa kona ya pili, inapigwa tena hukuu, Rostand anadaka na kutulia vizuuri kabisa
87': Yanga wanao sasa, Buswita, kwake Kessy, anarudisha kwa kipa wake
88': Yusuph Mhilu anakwenda na mpira upande wa kulia wa uwanja, anapigaa, gooooooli, Kagera wanajifunga katika harakati za kuokoa, sasa ni 3-0
90': Zimeongezwa dakika tatu pekee mpira umalizike
Full Time, Mwamuzi anapuliza kipyenga kumaliza mpira, Yanga 3-0 Kagera Sugar.