Dili kusoma Bongo au Mbele?!?

Scolari Ndenga

JF-Expert Member
Aug 4, 2008
271
43
Jamani nimekaa sana na kutafakari mno baada ya kusoma thread kadha wa kadha...!

Pia nimeangalia mno kuangalia status ya vyuo vyetu na kucompare na vya mbele...mmmh!!

Pia tuangalie jinsi vijana wengi wakichoropoka kwenda nje kusoma je kweli wanafata elimu bora ama?!?
 
Katika Sekta ya Elimu Tanzania Bado iko nyuma hivyo basi ni Vizuri zaidi kusoma nje kuliko hapa ili mradi tukirudi tuje kupanua wigo wa Elimu.Ama kuhusu Vijana wengi waliopo nje ni kweli wanfata kusoma au La hasha! Nadhani ni vigumu kulizungumzia jambo hilo!!
 
Nafikiri Mtu akisoma nje ya hapa huwa ni nzuri sana maana kuna kitu anajifunza haswa wengi wao upeo wa kufikiri huongezeka....... kuhusu vijana waliopo nje ka wanasoma au la ..... mh hilo linategemeana
 
suala la maana ni kuelimika,nikiwa na maana ya kuitumia elimu uliyoipata katika kuwezesha maendeleo ya jamii yako,sasa hapa hatuangalii kusoma marekani,uk,wala china,wala tz.kwani mafisadi wangapi wamesoma nje na wangapi walisoma tz?jibu ni kwamba wapo wengi tu.kuhusu kama wanaoenda nje wanasoma kweli au ala,hiyo pia mtu binafsi,mfano hapa nilipo mie wapo wanafunzi wameacha kusoma wanafanya shughuli zingine wakati lengo lao la kuja hapa ilikuwa kusoma,mie naona hilo nao ni akili ya mtu tu.
 
kuelimika ni popote pale vitabu ni vilevile ,sema tofauti inayojitokeza ni jinsi wanafunzi wanavyopagawishwa na wahadhili wao.

Mtu anaweza soma nyumbani kwake bila kwenda kokote kule akaelimika zaidi kuliko aliyepaa mwezini.Maana huyu anakua na uwanja mpana wa kuhoji na kudadisi mambo tofauti na aliye pale UDSM ama havard anayelazimishwa kukalili ili apasi mtihani yani ya kwamba hapewi uhuru wa kuhoji ama ku logic
 
Nimehamasishwa Sana Na Maoni Yako, Kusoma Na Kuwa Msomi Kunatofauti Kubwa Sana. Pia Kuelimika. Kuelimika Hakuhitaji Shule Ya Darasani Ni Kuwa Na Busara Inayokuwezeza Kupambana Na Maisha Ya Kila Siku Kwa Haki. Kuhusu Hili Suala Kukariri Mimi Huwa Naliita Akili Karirifu Ambayo Ndio Inategemewa Kwenye Academics Karibu Zote Duniani. Hii Inadumaza Sana Akili Inaziba ,mianya Ya Ubunifu Kwa Vizazi. Inakandamiza Akili Asilia Natural Intelgence. Ukija Kwenye Upande Wa Logic Huu Ni Muhimu Sana Kwani Mlolongo Wake Huwa Na Hitimisho La Haki Na Kweli Kutokana Na Mtizamo Wa Mtiu Binafsi

Ni kweli kabisa ndugu yangu
hiyo filosofia yako ya akili karirifu nimeifurahia,achana ni hiyo akili karirifu kuna watu nimesoma nao hawa wazungu wanameza vidonge yani akili yake inakumbuka mambo yote yani akiyameza kila atakachosoma atakumbuka kila kitu hadi koma,nukta.Ila balaa lake ni baada ya mtihani itabidi asinzie siku nzima.

Kuelimika ni filosofia iliyofichika na saizi kama tungekua kweli tunataka maendeleo tungeanza kufuatilia walio elimika ki kweli kweli.
 
Jamani nimekaa sana na kutafakari mno baada ya kusoma thread kadha wa kadha...!

Pia nimeangalia mno kuangalia status ya vyuo vyetu na kucompare na vya mbele...mmmh!!

Pia tuangalie jinsi vijana wengi wakichoropoka kwenda nje kusoma je kweli wanafata elimu bora ama?!?

Miguu, tafuta kwa bidii fursa ya kwenda kusoma nje hata kama ni semina ya siku mbili. Faida kubwa ni exposure. Kukutana na watu toka mataifa mbalimbali, mkabadilishana mawazo, mkashindana na mkashirikiana ni experience moja nzuri sana. Pili Tanzania tunachofanya ni "catching up" kwa hiyo ni vema ukaenda kuona wale tunaowaiga wamefikia wapi na wanaendesha vipi jamii zao.
 
Inategemea malengo yako kielimu.

Tangu nimeondoka Tanzania kuna vyuo vingi vimeanzishwa na sijapata bahati kutathmini mitaala yao. Mimi nitakupa mawazo yangu kwa kutumia chuo kikuu cha dar es salaam ambako nilisoma na nikapata bahati ya kufundisha.

(a) Kama unataka kupata digrii moja tu na kuingia mzigoni ukiwa mahiri sana wa taaluma yako kiutendaji kulingana na taratibu zilizopo basi ni afadhali ukasome nchi za nje. Kwa mitaala ya chuo kikuu cha Dar es Salaama, wanafunzi pale wanafunduisha kufikiri zaidi ya kutenda kwa mikono yao. Huo ndio ukweli wenyewe, na sitaki kuuficha.

(b) Kama unataka kusoma na kupanda hadi darini (Ph.D) basi ni afadhali uichukulie digrii yako ya kwanza hapo UDSM kusudi utakapoingia kwenye masters huko nje utakuwa na upeo mkubwa kuliko competitors wako wengi na hivyo kuweza kukwea hadi mwisho. Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kiko kama Sharif University cha Iran; kinawajenga vijana kwa nguvu sana katika nyanja ya kuchanganya nadharia ili kufikiria mambo mbali mbali, lakini wengi wa wahitimu wanakuwa ni wafikiriaji katika mazingira ambayo yanahitaji vitendo, na hivyo uwezo wao unakuwa haonekani kwa jamii.
 
Miguu, tafuta kwa bidii fursa ya kwenda kusoma nje hata kama ni semina ya siku mbili. Faida kubwa ni exposure. Kukutana na watu toka mataifa mbalimbali, mkabadilishana mawazo, mkashindana na mkashirikiana ni experience moja nzuri sana. Pili Tanzania tunachofanya ni "catching up" kwa hiyo ni vema ukaenda kuona wale tunaowaiga wamefikia wapi na wanaendesha vipi jamii zao.

Kwani mtu akisoma nyumbani anazuiwa kusafiri nchi nyingine? Exposure sio lazima iwe ni kwenda kusoma tu, inaweza kuwa ni kutembea kwa kutalii tu. Kwa maana hiyo hata aliyesoma nyumbani na akapata nafasi ya kusafiri na kubadilishana mawazo na watu wengine atapata exposure.

Jambo lingine kusom nje inategemea pia ni level gani ya elimu (msingi, sekondari, shahada ya kwanza, shahada ya uzamili, au shahada ya uzamifu). Kwa maoni yangu ni vizuri zaidi mtu kabla hajaenda nje awe kwanza amesoma shahada ya kwanza nyumbani. Hapo atakuwa na msingi mzuri wa uelewa wa mambo na hali halisi ya nchi yake kuliko ambaye atasomea shahada ya kwanza nje. Kwa kawaida katika fani kama sheria wanafundishwa mambo yanayolenga zaidi sheria za nchi husika, sasa kama mtu atasoma shahada ya kwanza ya sheria Marekani itakuwa ni vigumu sana ku-apply elimu hiyo Tanzania. Kwa hiyo kama ni kusoma nje, basi mtu aende huko kusoma kuanzia shahada ya uzamili.
 
Nimehamasishwa Sana Na Maoni Yako, Kusoma Na Kuwa Msomi Kunatofauti Kubwa Sana. Pia Kuelimika. Kuelimika Hakuhitaji Shule Ya Darasani Ni Kuwa Na Busara Inayokuwezeza Kupambana Na Maisha Ya Kila Siku Kwa Haki. Kuhusu Hili Suala Kukariri Mimi Huwa Naliita Akili Karirifu Ambayo Ndio Inategemewa Kwenye Academics Karibu Zote Duniani. Hii Inadumaza Sana Akili Inaziba ,mianya Ya Ubunifu Kwa Vizazi. Inakandamiza Akili Asilia Natural Intelgence. Ukija Kwenye Upande Wa Logic Huu Ni Muhimu Sana Kwani Mlolongo Wake Huwa Na Hitimisho La Haki Na Kweli Kutokana Na Mtizamo Wa Mtiu Binafsi

Ni Bahati Mbaya Sana bila Kukariri Huendi Popote.

Ni Nani Aliyesoma bila Kuweka Ka-element Ka Kukariri? Kama yupo ninaomba anipe Alifanyaje!

Njimba
 
nitumie email yako tuandike mchakato tukagombee nobel prize. maana kule japani walimfanyia uchunguzi nyani wakadai hana akili kama binadamu wakimshinikiza nyani awe na akili karirifu. wakati akili yake ni kwa ajili yake na maisha ya kila siku huko mwituni. Hata panya anakumbukumbu ya kujua pango lake liko wapi akalale, pia atapatawapi kitoweo chake cha kila siku. kumbukumbu ni sehemu ndogo sana ya akili ya viumbe. email yangu ni tgeofrey@gmail.com

mkamap@yahoo.com
 
Ila jamani elimu ya bongo ina bore sana....hasa ya vyuo vikuu.lol
 
Kwani mtu akisoma nyumbani anazuiwa kusafiri nchi nyingine? Exposure sio lazima iwe ni kwenda kusoma tu, inaweza kuwa ni kutembea kwa kutalii tu. Kwa maana hiyo hata aliyesoma nyumbani na akapata nafasi ya kusafiri na kubadilishana mawazo na watu wengine atapata exposure.

Jambo lingine kusom nje inategemea pia ni level gani ya elimu (msingi, sekondari, shahada ya kwanza, shahada ya uzamili, au shahada ya uzamifu). Kwa maoni yangu ni vizuri zaidi mtu kabla hajaenda nje awe kwanza amesoma shahada ya kwanza nyumbani. Hapo atakuwa na msingi mzuri wa uelewa wa mambo na hali halisi ya nchi yake kuliko ambaye atasomea shahada ya kwanza nje. Kwa kawaida katika fani kama sheria wanafundishwa mambo yanayolenga zaidi sheria za nchi husika, sasa kama mtu atasoma shahada ya kwanza ya sheria Marekani itakuwa ni vigumu sana ku-apply elimu hiyo Tanzania. Kwa hiyo kama ni kusoma nje, basi mtu aende huko kusoma kuanzia shahada ya uzamili.

Mtuwamungu ukienda mahali kama mtalii you'll always be an outsider. Utaona majengo n.k. lakini utakuwa na insights kidogo sana kuhusu fikra zinazoendelea. Ila ukienda kama mwanafunzi, au mfanyakazi una fursa kubwa ya kupata ufahamu mkubwa kuhusu kwa nini watu hao wanafanya vitu unavyoviona.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom