Digrii ya kwanza nchini china

mhalisi

JF-Expert Member
Sep 9, 2011
1,181
320
Wadau naomba kuuliza kama nchini china kuna vyuo vikuu vinavyofundisha degree ya kwanza kwa miaka mitatu na inatambulika? Nauliza kwasababu nimeona vyuo vikuu karibu vyote vya china vinatoa degree za kwanza kwa miaka minne.
 
Kama unataka kusaidiwa toa maelezo yanayojitosheleza, kwa mfano, wewe unataka kusoma fani gani? kwa sababu muda wa masomo haulingani unategeana na aina ya program unayotaka kusoma. Kwa mfano udaktari wa binadamu/wanyama ni miaka 5-7, engineering ni miaka 4 n.k. Ila kwa mfumo wa elimu wa China muda wa chini kabisa kusoma degree ya kwanza ni miaka minne, hii ni kawaida na siyo jambo geni. Hata hapo Tanzania kuna program za shahada ya kwanza za miaka 4 nyingi tu.

Na kwa china kama hujui lugha, kuna mwaka 1-2 wa kujifunza lugha. Labda kama unataka kusoma Hong Kong ambako wanatumia kiingereza vyuo vikuu.

So, what is your problem.
 
mimi nataka kusoma bachelor of business administration, sasa napenda kujua kama vipo vyuo vinatoa bachelor degree kwa miaka mitatu ili nifanye application.
 
mimi nataka kusoma bachelor of business administration, sasa napenda kujua kama vipo vyuo vinatoa bachelor degree kwa miaka mitatu ili nifanye application.

Unayouliza yanaendana na upeo wako wa uelewa na muda ambao umekaa humu jamvini!
 
Usiogope kwenda kukaa miaka minne ndugu, wenzio wengi wanakamua hadi miaka mitano huko. We nenda kama unaogopa si uende vyuo vya hapa hapa bongo au nchi jirani?
 
Back
Top Bottom