MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,213
- 22,277
Hivi karibuni kuna tukio limetokea huko Marekani ambalo kwa upande wangu limenifanya nifikiri tofauti kabisa. Msanii Kanye West alishambuliwa sana kwa maneno toka kwa Black Americans kisa kikiwa yeye kusema WHITE LIVES MATTER. Ikumbukwe weusi wengi wana harakati zao za BLACK LIVES MATTER. Miongoni mwa waliomshambulia kwa maneno ni msanii maarufu Sean Combs (Diddy).
Binafsi nawaunga mkono weusi wote kwenye harakati zao ila siwaungi mkono kutaka kuminya haki za wengine kwasababu ni weupe. Wakifanya hivyo hawatakuwa tofauti na hao weupe wanaowalalamikia daily. Pia kuingilia uhuru binafsi wa Kanye sio sawa. Kanye yuko sahihi kabisa kusema White lives matter kwasababu kila binadamu bila kujali rangi ana haki ya kuishi. Kina Didy wanakosea sana kutengeneza chuki dhidi ya weupe. Hii itaendelea kuwafanya black Americans kujiona wako chini ya weupe na kuwaondolea kujiamini.
Black Americans wanatakiwa wapambane sana hasa kwenye elimu ili kuweza kujikomboa na sio kila black awe anawaza muziki, basketball na filamu wakati kwenye vyombo vya maamuzi nyeti wakiwa wachache. Anachofanya Didy ni kuzidi kujinufaisha yeye tu. Kina Didy na wenzake wenye mtazamo unaofanana hawana tofauti na makada wa CHADEMA wanaotaka uhuru wa kutoa maoni wakati wao wanaongoza kwa blocks mitandaoni huku wakiwa vinara wa matusi.
Binafsi nawaunga mkono weusi wote kwenye harakati zao ila siwaungi mkono kutaka kuminya haki za wengine kwasababu ni weupe. Wakifanya hivyo hawatakuwa tofauti na hao weupe wanaowalalamikia daily. Pia kuingilia uhuru binafsi wa Kanye sio sawa. Kanye yuko sahihi kabisa kusema White lives matter kwasababu kila binadamu bila kujali rangi ana haki ya kuishi. Kina Didy wanakosea sana kutengeneza chuki dhidi ya weupe. Hii itaendelea kuwafanya black Americans kujiona wako chini ya weupe na kuwaondolea kujiamini.
Black Americans wanatakiwa wapambane sana hasa kwenye elimu ili kuweza kujikomboa na sio kila black awe anawaza muziki, basketball na filamu wakati kwenye vyombo vya maamuzi nyeti wakiwa wachache. Anachofanya Didy ni kuzidi kujinufaisha yeye tu. Kina Didy na wenzake wenye mtazamo unaofanana hawana tofauti na makada wa CHADEMA wanaotaka uhuru wa kutoa maoni wakati wao wanaongoza kwa blocks mitandaoni huku wakiwa vinara wa matusi.