Diamond usiwapuuze wanaokuandama sasa, hao sio shilawadu au Konde Gang. Chukua hoja zao

Wanaharakati wamefikia wapi mpk sa hiz jamani?
Au kura hazijatosha kuwashawish BET
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣.

HII NCHI KUNA MUDA INA MAMBO YA KIWEHUUUU.
 
Na amekaa kimya basi haters napo wanaumia kweli..walitegemea angeongea...yuko bize anapost shoo zake
Kaaaama sio yeye aliyekuwa anawekewa link na votes zikafika ngapi sijui.

🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
Dogo shule hajaenda ila akili aliyonayo kwenye biashara hii ya muziki hakuna anayeweza kumuangusha kirahisi.
 
DIAMOND USIWAPUUZE KINA KIGOGO NA WANAMTANDAO, HAO SIO KINA KONDE NA SHILAWADU

Na, Robert Heriel

Diamond hapaswi kupuuza hii movement ya Wanaharakati wa kimtandao na wanasiasa, asije akafikiri kundi hili nila Wale Wasanii wenzake ambao hata shule hawajaenda.

Diamond anapaswa Ajue kuwa Wanaharakati wa mtandaoni ni wasomi tena sio wakubahatisha, wana-exposure ya hali ya juu kumshinda hata yeye mwenyewe.

Kama ningeambuwa nimshauri Diamond kuhusiana na kile kinachoendelea mtandaoni ningemwambia aombe radhi hata ya kinafiki kwani yote anayotuhumiwa ni kweli.

Diamond anapaswa Ajue kuwa kundi hili ndilo lile lile lililokuwa linamshambulia Mwendazake bila kukoma mpaka dakika ya mwisho kabisa bila kujali athari zozote. Ikiwa kundi hili lilimudu kumkabili Mkuu. WA nchi lazima Diamond afikiri mara mbili mbili asifikiri Kama mtoto mdogo.

Simtishi Ila namtahadharisha ili achukue hatua zinazostahili. Nafikiri Diamond Kama atazichukua hoja za hawa wanamtandao akazifanyia kazi atakuwa msanii Bora zaidi kuliko akizipuuza.

Ni kweli kabisa Diamond hakuweza kuzungumzia uonevu na ukiukwaji wa haki za binadamu uliofanyika miaka ya 2016 - 2019 zaidi ya yote alitoa kibao kisemacho ACHA NIKAE KIMYA.

Diamond asije akadhani hawa wanamtandao ni Wale kina Konde na shilawadu

Diamond lazima aangalie hili kundi linaloongozwa na #Kigigo_kigogo, na wenzake halijawahi kushindwa katika movement wazifanyazo.

Hilo kundi asilipuuze na Kama atalipuuza basi Ajue anafanya makosa makubwa yatakayo mgharimu pakubwa mno.

Diamond asilione kundi hilo Kama watafuta Kick Kama yeye na wenzake kwani kundi hilo halitegemei kick.

Management ya Diamond na washabiki wake ambao kimsingi nafahamu wengi wao wanafikiri kuwa kila anayemkosoa Diamond ni haters wabadilishe huo mtazamo.

Hakuna anayemchukia Diamond labda Wasanii wenzake huko.

Diamond unachopaswa kufanyia KAZI ni madai ya hao Wanaharakati wa mitandaoni.

Wanamtandao hawakatai Diamond kuwa CCM hiyo ni Haki yake Kama apendavyo, lakini tatizo ni diamond kushindwa kutetea maslahi na haki ya jamii yake pale zinaposiginwa.

Diamond Kama anaakili aichukue hii Kama changamoto na ajifunze ili wakati mwingine aweze kutetea maslahi na haki za jamii yake wakiwemo Wasanii.

Lakini Kama atashupaza shingo yake Nina uhakika Diamond huu unaweza kuwa mwanzo wa mwisho wake.

Diamond akileta mawazo ya mwendazake akidhani kila anayemshauri na kumkosoa ni hater basi anguko lake halipo mbali.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kashapigwa huko na mnigeria hahahaaa
 
Hiyo ilikuwa wazi kabisa
Ilikua ni swala la kusimama kama Taifa kuhakikisha tuzo inakuja nyumbani, bt kwa manyaunyau ya wasafi tumegawanyika sana na tunawapa gape wapinzani, WCB wanatakiwa wajirekebishe na wawe pamoja na wenzao wakiendelea kujiona matawi ipo siku hata KTMA ikirudi watatoka patupu...NAWASILISHA
 
Back
Top Bottom