venance7
JF-Expert Member
- May 15, 2019
- 554
- 1,637
Msanii Diamond platnumz akihojiwa katika kipindi cha Good morning ya Wasafi FM amesema amenunua hoteli yenye hadhi ya nyota tatu iliyopo Mikocheni, hoteli hiyo amedai ina vyumba zaidi ya 30 pamoja na conference room, pia amedokeza suala la kununua gari ya ndoto yake Rolls Royce ambayo ni ghali zaidi ila bado haijafika nchini na yupo katika hatua za mwisho kuifikisha.
Amezungumzia suala la kukataa kulea watoto wake aliozaa na Zari the bosslady kuwa alimtafuta mzazi mwezie huyo na tayari wamemaliza tofauti zao zilizokuwepo.
Kuhusu hoteli hiyo Diamond ameiomba wizara ya Afya kama ipo tayari waifanye hata karantini kwa ajili ya wagonjwa wa corona kwani kabla ya kuanza kutumika anatarajia kuifanyia marekebisho ya kuiongeza hadhi.
Amezungumzia suala la kukataa kulea watoto wake aliozaa na Zari the bosslady kuwa alimtafuta mzazi mwezie huyo na tayari wamemaliza tofauti zao zilizokuwepo.
Kuhusu hoteli hiyo Diamond ameiomba wizara ya Afya kama ipo tayari waifanye hata karantini kwa ajili ya wagonjwa wa corona kwani kabla ya kuanza kutumika anatarajia kuifanyia marekebisho ya kuiongeza hadhi.