kombaME
JF-Expert Member
- Aug 24, 2015
- 2,115
- 2,807
Nyie watu mnatukosea sana, mmeamua kabisa kuyachosha masikio yetu, hadhi ya Diamond na Wasafi kwasasa ni kubwa sana, kwasasa mpo kwenye wakati wa kutengeneza uniqueness yenye hadhi ya juu, kwanini mnatufanyia hivi??
Hapa katikati mmeanza kutoa nyimbo ambazo hazieleweki, mnapayuka payuka tu mwanzo hadi mwisho halafu mnapeleka youtube then mnatuambia twende tukasikilize, kweli? Masikio yetu yamewakosea nin nyie watu? WCB siku hizi hamtungi kabisa nyimbo, hakuna ubunifu wowote wa kiuwanamuziki kwenye nyimbo zenu, mmeshajiamini sana kiasi cha kuona mnaweza kufanya chochote mnachotaka, Sio Sawa.
Mziki wenu mnatoa leo baada ya wiki umeisha kabisa nguvu yake na wala hausikiliziki tena, hauwezi kukugusa kwa namna yoyote na katika mazingira yoyote, sasa mziki gani huo? Mnatukosea sana nyie watu
Hebu jifunzeni kwa makundi yaliyokuwa serious na muziki, nyimbo zina miaka hadi 20 lakini ikipigwa inakupa ahueni na kuupooza moyo, muziki ni dawa, nyinyi mnatupa sumu, sikilizeni nyimbo za R Kelly, Westlife, Boys2men n.k... ni kitambo mno lakini hadi leo zinaishi mioyoni mwetu.
Tafadhalini, umizen vichwa, kaeni chini mtunge nyimbo na sio kutafuta kaneno kamoja unakataja taja hako tu nyimbo nzima, mnatukosea.
Hapa katikati mmeanza kutoa nyimbo ambazo hazieleweki, mnapayuka payuka tu mwanzo hadi mwisho halafu mnapeleka youtube then mnatuambia twende tukasikilize, kweli? Masikio yetu yamewakosea nin nyie watu? WCB siku hizi hamtungi kabisa nyimbo, hakuna ubunifu wowote wa kiuwanamuziki kwenye nyimbo zenu, mmeshajiamini sana kiasi cha kuona mnaweza kufanya chochote mnachotaka, Sio Sawa.
Mziki wenu mnatoa leo baada ya wiki umeisha kabisa nguvu yake na wala hausikiliziki tena, hauwezi kukugusa kwa namna yoyote na katika mazingira yoyote, sasa mziki gani huo? Mnatukosea sana nyie watu
Hebu jifunzeni kwa makundi yaliyokuwa serious na muziki, nyimbo zina miaka hadi 20 lakini ikipigwa inakupa ahueni na kuupooza moyo, muziki ni dawa, nyinyi mnatupa sumu, sikilizeni nyimbo za R Kelly, Westlife, Boys2men n.k... ni kitambo mno lakini hadi leo zinaishi mioyoni mwetu.
Tafadhalini, umizen vichwa, kaeni chini mtunge nyimbo na sio kutafuta kaneno kamoja unakataja taja hako tu nyimbo nzima, mnatukosea.