Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 52,206
- 42,067
Wanajamvi Habari.
Hivi karibuni baada ya msanii Diamond Platnumz kuchaguliwa kuwania tuzo za BET kumeibuka makundi mbalimbali hasa baadhi ya wasanii na wanasiasa kulazimisha wasanii na wadau wote wa muziki na wasio wadau wa muziki kumuunga mkono Diamond.
Lazima tuseme ukweli kuwa hata Diamond mwenyewe huwa haungi mkono wasanii wote kwenye kazi zao na wadau wote kwenye kazi zao hivyo tusiwalaumu au kuwalazimisha watanzania wote kumuunga mkono Diamond.
Lazima tukubali Diamond ana makundi na yanajulikana na ndiyo yanayo mgharimu sasa kwa hiyo watu waache nature/asili ichukue nafasi.
Nakumbuka kipindi kile cha Paul Makonda alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-salaam alizuia kufanyika kwa tamasha la Fiesta na Diamond na kundi lake ndio waliongoza kuchekelea na kuwabeza Clouds....
Diamond alikuwa anajua fika kipindi kile wasanii wenzie wengi walikuwa wanapata kula kupitia lile tamasha lakini alichekelea kufungiwa kwa hilo tamasha hadi kukwaruzana na wakina Fid Q ... Kwa hiyo watu waache wachague cha kufanya wasilazimishwe uzalendo maana Diamond sio mzalendo.
Wasanii wanampost tu kwakuwa wasionekane wabaya na wengine wanafanya hivyo kwakuwa ni mmiliki wa radio lakini si kwamba wanapenda maana ukweli ni kwamba Diamond huwa hatoi support kwa wasanii wenzie....
Watu waache wawe huru kabisa maana Diamond atavuna alichopanda watu wasilazimishwe kumuunga mkono.
Hivi karibuni baada ya msanii Diamond Platnumz kuchaguliwa kuwania tuzo za BET kumeibuka makundi mbalimbali hasa baadhi ya wasanii na wanasiasa kulazimisha wasanii na wadau wote wa muziki na wasio wadau wa muziki kumuunga mkono Diamond.
Lazima tuseme ukweli kuwa hata Diamond mwenyewe huwa haungi mkono wasanii wote kwenye kazi zao na wadau wote kwenye kazi zao hivyo tusiwalaumu au kuwalazimisha watanzania wote kumuunga mkono Diamond.
Lazima tukubali Diamond ana makundi na yanajulikana na ndiyo yanayo mgharimu sasa kwa hiyo watu waache nature/asili ichukue nafasi.
Nakumbuka kipindi kile cha Paul Makonda alipokuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-salaam alizuia kufanyika kwa tamasha la Fiesta na Diamond na kundi lake ndio waliongoza kuchekelea na kuwabeza Clouds....
Diamond alikuwa anajua fika kipindi kile wasanii wenzie wengi walikuwa wanapata kula kupitia lile tamasha lakini alichekelea kufungiwa kwa hilo tamasha hadi kukwaruzana na wakina Fid Q ... Kwa hiyo watu waache wachague cha kufanya wasilazimishwe uzalendo maana Diamond sio mzalendo.
Wasanii wanampost tu kwakuwa wasionekane wabaya na wengine wanafanya hivyo kwakuwa ni mmiliki wa radio lakini si kwamba wanapenda maana ukweli ni kwamba Diamond huwa hatoi support kwa wasanii wenzie....
Watu waache wawe huru kabisa maana Diamond atavuna alichopanda watu wasilazimishwe kumuunga mkono.