kibaravumba
JF-Expert Member
- Dec 21, 2012
- 6,635
- 7,005
Nimefuatilia mahojiano ya huyu Mzee Abdul baba yake Diamond katika TV ya Carrymastori. Mzee anajikaza kiume.
Chini katika maoni nimeona comments za visichana na vivulana vya kizazi hiki vikimponda Mzee kuwa anastahili kupitia anayopitia kwa vile alimtelekeza Diamond akiwa mtoto.Inasikitisha!
Katika maisha,wanaume tunakabiliwa na mengi ila wengi huwa hatulii lii hovyo.
Kuna wanawake umezaa naye, unampa pesa ya matumizi huku anakutukana. Una kipato cha kawaida, unampa mzazi mwenzio pesa, ila anakutukana kuwa unatoa pesa gani ya mboga Unapigania umchukue mwanao,anafanya kila awezalo usifanikiwe. Inafika mahali anakuatambia ana bwana mwenye hela hivyo hababaishwi na vihela unavyomtumia.Unajikuta moyo unakufa ganzi. Mtoto anakuwa mkubwa, amelishwa sumu ya kutosha. Anakuona kama kibaka tu
Diamond unatakiwa kumjali sana baba yako. Ukiangalia hata kitambaa alichojifunga kama barakoa,utaona kiuhalisia aina ya maisha aliyonayo.
Mzee mwenye mtoto anayeweza kulipia kodi watu 500, na wakati huo umenunua hoteli ya mamilioni ya pesa, mzazi wako anafanya biashara ya umachinga wa kutembeza Viatu na corona hii! Ni nini hiki?
Wengine wanashindwa kuwajali wazazi kwa sababu ya uwezo mdogo, wewe una sababu gani ya kuruhusu mzazi aishi kwa unyonge jinsi hiyo?
Hivi haya masharti ya illuminat mbona yanakuwa ya ajabu sana? Au mama Diamond kwa nini usimwambie mwanao amjali baba yako kama anavyokujali wewe?
Au ulishamwambia ana baba mwingine?
Chini katika maoni nimeona comments za visichana na vivulana vya kizazi hiki vikimponda Mzee kuwa anastahili kupitia anayopitia kwa vile alimtelekeza Diamond akiwa mtoto.Inasikitisha!
Katika maisha,wanaume tunakabiliwa na mengi ila wengi huwa hatulii lii hovyo.
Kuna wanawake umezaa naye, unampa pesa ya matumizi huku anakutukana. Una kipato cha kawaida, unampa mzazi mwenzio pesa, ila anakutukana kuwa unatoa pesa gani ya mboga Unapigania umchukue mwanao,anafanya kila awezalo usifanikiwe. Inafika mahali anakuatambia ana bwana mwenye hela hivyo hababaishwi na vihela unavyomtumia.Unajikuta moyo unakufa ganzi. Mtoto anakuwa mkubwa, amelishwa sumu ya kutosha. Anakuona kama kibaka tu
Diamond unatakiwa kumjali sana baba yako. Ukiangalia hata kitambaa alichojifunga kama barakoa,utaona kiuhalisia aina ya maisha aliyonayo.
Mzee mwenye mtoto anayeweza kulipia kodi watu 500, na wakati huo umenunua hoteli ya mamilioni ya pesa, mzazi wako anafanya biashara ya umachinga wa kutembeza Viatu na corona hii! Ni nini hiki?
Wengine wanashindwa kuwajali wazazi kwa sababu ya uwezo mdogo, wewe una sababu gani ya kuruhusu mzazi aishi kwa unyonge jinsi hiyo?
Hivi haya masharti ya illuminat mbona yanakuwa ya ajabu sana? Au mama Diamond kwa nini usimwambie mwanao amjali baba yako kama anavyokujali wewe?
Au ulishamwambia ana baba mwingine?