JUAN MANUEL
JF-Expert Member
- Nov 26, 2010
- 6,832
- 14,192
Wabongo MNA chuki sana!!Kwa kuwa kaonyesha ukaidi dhidi ya serikali(BASATA) basi iandikwe barua kwenda uhamiaji kuzuia ziara zake zote za kimuziki duniani,paspoti ipigwe pini
Mond kawafanya nini?kwanini mnamchukia kiasi hicho?hizi ni chuki binafsi!!
Kijana kawa milionea,amepata ukwasi ambao vijana wengi na madigrii yao,wanauota tu!!sasa hilo linawaumiza wengi!!
Mbona hamuwachukii mafisadi waliokwapua pesa zetu,na kusababisha huduma za jamii kuwa duni?watoto wanazaliwa wanakufa,mama wajawazito wanakufa,!!hao hamuwachukii???mnamchukia Mond kisa kaimba Nyegezi!!!sababu eti maadili!!!
Mond inabidi atetewe na watz wote wa kada ya chini na kati.
Lakini watu walivyona roho mbaya,wanataka awe fukara kama wao!!ili wasichekane,kinawauma sana wakimuona anapiga pesa,ambazo wao ni ndoto kuzipata,hata wakikusanya Mali zote za ukoo wao.