Diallo TV na Ulokole kwenye sherehe ya mwaka mpya

Alnadaby

JF-Expert Member
Sep 28, 2006
505
41
Mheshimiwa waziri na rafiki yangu Diallo.Najua fika kuwa wewe ni mwanasiasa mwenye juhudi kubwa katika masuala ya haki na maendeleo kitaifa.Tv yako ya Star una kila aina ya power of influence kwa wafanyakazi wako kutangaza kile unachodhani kuwa ni sahihi na kina manufaa kwa nchi na raia.

Nataka nikushauri kuwa kama unataka injili ihubiriwe vema basi tumia hiyo Tv yako kama chombo kila siku ya mwaka 2008 na ubadlilishe jina kutoka STAR kuwa kitu kama CROSS TV ili utangaze neno la bwana kwa wale ambao una wa target.

Kama unataka kuwa kama ITV,BBC,TVT au CNN basi nakushauri usichague dhehebu moja likaiteka Tv na kuharibu kabisa maana ya sherehe ya mwaka mpya.Star Tv haikutakiwa kuchanganya mambo siku ya mwaka mpya na kuwa kama kitengo cha dhehebu la dini.Mheshimiwa TV yako inawafikia Watanzania wote wote si walokole tu na haifurahishi hata kidogo inapokuwwa ni chombo cha uenezaji injili badala ya chombo cha upashaji habari na kutoa burudani kwa wote.
 
Anadaby tunarudi tena kenye mabishano ya udini,,sioni ajabu kwa star tv kutangaza ibada ya walokole,,mbona ujaandika ATN ambao wallionyesha toka ssaa moja,,,labda kwa ushauri tusiwape watu kushindanisha mijadala ya udini kwenye formus else tutarudi kenya
 
Alnadaby, ITV TVT hazijakuridhisha, star tv unaona miyeyusho, basi nunua decoder ya GTV nayo ujaribu.
 
Anadaby tunarudi tena kenye mabishano ya udini,,sioni ajabu kwa star tv kutangaza ibada ya walokole,,mbona ujaandika ATN ambao wallionyesha toka ssaa moja,,,labda kwa ushauri tusiwape watu kushindanisha mijadala ya udini kwenye formus else tutarudi kenya

Hapa hakuna suala la udini ndugu yangu.Kama wangekuwa wametangaza mawaidha ya dini ya Kiislamu kwenye hafla hiyo wala nisingefurahia hata kidogo kwa sababu ningekuwa nafanya ubaguzi wa kidini dhidi ya wale wasiokuwa Waislamu.Nilitaka tu kuonesha jinsi hisia za kidini zisivyofaa kuingizwa katika mambo ya binadamu wote kama vile sherehe za mwaka mpya.Ingekuwa sherehe ya Krismas wala nisingesema kitu maana program ingekuwa ikienda sanjari na siku ya kuzaliwa Yesu.
Kwa mfano huwezi kusherehekea siku ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kuimba kaswida na kuandaa mikutano mikubwa ya kumsalia Mtume kama vile ambavyo haiwezekani kusherehekea Pasaka kwa kufanya gwaride la polisi.Kila sherehe inatakiwa kusherehekewa kwa maudhui yake.Pamoja na kwamba mwaka unaosherehekewa ni wa kikristo lakini ndiyo mwaka wa dunia kwa sasa kwa maana ya mataifa mengi yasiyokuwa ya Kikristo yanachukulia huo mwaka kuwa ndiyo mwaka rasmi.nadahani umenielewa ndugu PDiddy.
 
Sasa wewe shida iko wapi?
ungebadili station kama hiyo ilikuwa inakukera!
Au siku hizi STAR TV ni ya taifa?(public) mambo ya soko huria!
Channel 5 etv walivyokuwa wanarusha nyimbo za dini kila siku asubuhi ilikuwa sawa?

Ukiona channel mmoja inabore wewe zungusha antena.
 
Sijaona tatizo kwa star TV, kwanza ilikuwa ni kuombea Taifa. Kwa nini hukuangalia ngwasuma TVT? kila mtu ana uhuru kuangalia au kutoangalia. Ni kiasi cha kubadilisha channell tu ndugu yangu.
 
Mi siono ubaya wowote hapo, isitoshe walikuwa wanaombea taifa si dini ya kilokole. hebu tuwe tunaangalia mambo ya kukosoa. hata hivyo naheshimu maoni yako, kama walivyosema wengine hapo juu ungebadilisha tu channel n hold your peace.
 
Sijaona tatizo kwa star TV, kwanza ilikuwa ni kuombea Taifa. Kwa nini hukuangalia ngwasuma TVT? kila mtu ana uhuru kuangalia au kutoangalia. Ni kiasi cha kubadilisha channell tu ndugu yangu.

Loi, nakubaliana na wewe kabisa, maadam star tv sio ya serikali, wana uhuru wa kuonyesha wanachotaka kwa muda wao wanaotaka..na pia mtazamaji anao uhuru wa kuamua aaangalie ama asiangalie! sasa hivi si tuna channel nyingi tu kwa nini usitafute nyingine chap chap badala ya kulalamika?
 
Nadhani mnakwenda beyond my point.Kama wewe ni mlokole I can understand your concern.Sina tatizo kabisa na wale wanaosema ningebadili chanel.Kusema kweli nilibadili channel lakini hebu fikiria wewe ni mlokole na TV uipenadyo ikusomee quran kwa masaa 2 tu.Ofcourse utabadili kabla ya dakika 2.Lakini je hao Star Tv wanafurahia kukimbiwa na watazamaji?Ijadili hiyo kwa mtazamo huu.Kama Dialo na star Tv wana maslahi ya kibiashara its fine lakini kama walikuwa wanatafuta kutangaza dini ilikuwa watayarishe kipindi katika siku maalum za kidini.Labda ingekuwa vema watu wa Star Tv wakatupa majibu muafaka.
 
Alnadaby, hizo pumba! usitafute ngongoti wa kupagawisha ngoma kwa uzezeta wa manju. umeanzisha mada sasa mzee nyala unataka wa nini tena. s***zi type!
 
If STAR TV is using public funds then there could be an issue because not every John Doe is down with gospel music.

Otherwise, it may be an alienating business decision but as a private operator you can pretty much flip the channel.More opportunity to start a neutral TV and capture the portion of viewers who will be irritated by STAR TV.
 
Alnadaby, hizo pumba! usitafute ngongoti wa kupagawisha ngoma kwa uzezeta wa manju. umeanzisha mada sasa mzee nyala unataka wa nini tena. shenzi type!

Nyala huyo ndiye anaweza kutoa jibu lakini wewe hulka yako haifanani kabisa na ustaarabu wa kilokole.Jibu lako halilipi pressure kabisa.
 
If STAR TV is using public funds then there could be an issue because not every John Doe is down with gospel music.

Otherwise, it may be an alienating business decision but as a private operator you can pretty much flip the channel.More opportunity to start a neutral TV and capture the portion of viewers who will be irritated by STAR TV.

Now that's a very good reply.The owner chooses what he wishes to show.The audience will move according to what they want to see.
 
nadhani sasa watu wamekuwa wavivu wa kufikiria. Ni juzi tu hata pale bungeni Malima alitoa pumba kuwa ITV wanampendelea Mengi bila kujua kuwa ni chombo chake imradi havunji sheria yoyote ya nchi. Tupigie kelele tuonapo TVT/RTD vinapotumiwa vibaya kwani vyatumia kodi zetu. Lakini vikitumiwa na CCM kwa shughuli zao wote kimya.

Unajuaje kama waandaji wa sherehe ze mwaka mpya 2008 walilipia Star TV???? kumbuka kile ni chombo cha kibiashara wala siyo cha hiduma kwa jamii.

Tuache kutoa pumba bali tufikirie zaidi
 
Nsololi katoa jibu tosha,hamna haja ya kupiga kelele ya kwanini hiki na kile hakuna Nyota TV.

Mfungua thread kama kuna kitu kingine unataka kujua behind the scene
 
alnaby kumbuka hiki ni chombo cha biashara,,kubwa zaidi ni chombo binafsi chenye uhuru wa kufanya mambo yake.....hivyo napenda tu kukujulisha weka hayo mambo kichwani then utajua hawakuwa na makosa,,,STAR TV aitegemei kodi yako kama TVT,,,kasanal,loi judy tumwelimishe tu jamani..amekosea ama anaitaji msaada hakuna haja ya kumt*****a,,

2))Alikuwa na haki ya kuuliza ama maana kuna sehemu nyingine jamani haikamati zaidi ya station moja ,,labda uko aliko inakamata star tv pekee,,angebadilishaje na mnajua gairo,kulivyo na matatizo ya network,,,,ALNABY KARIBU TENA RUKSA KUELIMISHWA
 
Tusiharibu mjadala kwa kurusha matusi.Matusi nimepata na kuelimishwa pia.Sasa nakumbuka pia kuwa CCM na JK mnamo 2005 walipata coverage about 90% kwenye Star TV na matokeo yake ndiyo hayo tuliyoyaona.Athari yake
wapinzani walipondwa na Mwenye TV kaukwaa uwaziri.Nimeelimika wakuu sasa sina hoja tena.Mwenye nacho ndiye bwana mkubwa,asiyekuwa nacho atulie.
 
Naona unataka kutuletea mambo ya Kenya, HATUTAKI. Kwanza pale walikuwa wanaombe Taifa na kwa taarifa yako mgeni rasmi alikuwa Mh. Rais na alimutuma waziri wake kumuwakilisha Mh Batilda Buriani inamaana na wenyewe ni walokole? Hukulazimishwa kuangalia hiyo channel hata Al-jezira walikuwa hewan ungeangalia huko
 
Mkuu Alnaby Natumaini Sasa Utaiitwa Chrisnaby Baada Ya Kuelewa
Bwana Yesu Asifiwe Nilikuwa Nimekuwaka Kwenye Maombi Kwa Muda Upate Ufahamu Wa Hili,,,pia Sikutukana Nilichoandika Mkuu Waache Ku.......a(kutukana),,napenda Hoja Juu Ya Hoja,ubarikiwe Na Bwana Karibu Kwa Mama Yetu Rwakatare Kama Uko Bongo..ntafurahi Jumapili Nikikuona
Ubarikiwe Na Bwana
 
..Mheshimiwa TV yako inawafikia Watanzania wote wote si walokole tu na haifurahishi hata kidogo inapokuwwa ni chombo cha uenezaji injili badala ya chombo cha upashaji habari na kutoa burudani kwa wote.

Unaonekana kuwa u mwepesi sana kubisha kuliko kuelewa..Kwa taarifa tu, hata INJILI ni HABARI, ni habari tena NJEMA iwapo ungeonja japo kidogo maana yake ni nini..Labda tuseme kwamba una matatizo ya kimsingi na huyo aliyoleta hiyo habari (Authority wa injili) maybe tutakuelewa..otherwise your posting is simply BS.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom