Naona hujui nini maaana ya biashsra huru. kama star TV ilikuboa ishia
Hapa hakuna suala la udini ndugu yangu.Kama wangekuwa wametangaza mawaidha ya dini ya Kiislamu kwenye hafla hiyo wala nisingefurahia hata kidogo kwa sababu ningekuwa nafanya ubaguzi wa kidini dhidi ya wale wasiokuwa Waislamu.Nilitaka tu kuonesha jinsi hisia za kidini zisivyofaa kuingizwa katika mambo ya binadamu wote kama vile sherehe za mwaka mpya.Ingekuwa sherehe ya Krismas wala nisingesema kitu maana program ingekuwa ikienda sanjari na siku ya kuzaliwa Yesu.
Kwa mfano huwezi kusherehekea siku ya mapinduzi ya Zanzibar kwa kuimba kaswida na kuandaa mikutano mikubwa ya kumsalia Mtume kama vile ambavyo haiwezekani kusherehekea Pasaka kwa kufanya gwaride la polisi.Kila sherehe inatakiwa kusherehekewa kwa maudhui yake.Pamoja na kwamba mwaka unaosherehekewa ni wa kikristo lakini ndiyo mwaka wa dunia kwa sasa kwa maana ya mataifa mengi yasiyokuwa ya Kikristo yanachukulia huo mwaka kuwa ndiyo mwaka rasmi.nadahani umenielewa ndugu PDiddy.