Shujaa Mwendazake
JF-Expert Member
- Jul 11, 2015
- 3,735
- 6,280
Nikimnukuu mwanajamvi Pythagoras ktk comment yake:
[Askofu Emmaus B. Mwamakula alikamatwa wiki ya mwisho ya mwezi Februari. Mapolisi wa Jiwe wakamdhihaki eti "Yule anayejiita Askofu" tunamhoji. Niliposikia vile nikajua sasa Meko ame cross red line. Meko Hakumaliza hata wiki mbili tena.
Alipotoka askofu aliandika ujumbe mzito akamaliza na Mwanakondoo ameshinda Tumfuate!
Baada ya hapo Jiwe akatoa mashambulizi dhidi ya Maaskofu pale St Peters kuhusu uvaaji wa barakoa na hii ni baada ya Niwemugizi Kutangaza orodha ya watawa waliokufa kwa corona ndani ya muda mfupi. Zile zilikuwa ni kejeli dhidi ya maaskofu wa Kikatoliki siku aliposimama pale madhabahuni St Peters Oysterbay mbele ya waumini na wafuasi wa kanisa na taifa kwa ujumla.
Tuliosoma definition ya History tunakumbuka kuwa ni study of past events, lakini pia tunaambiwa tunajifunza history ili tuweze kupredict the future lakin pia kujifunza failures na mafanikio ya tunaowasoma.
Hili la ubabe, dharau na kejeli kwa viongozi au taasis za kidini tunashauri Serikali chini ya mama iliangalie sana maana hata Kongo anguko la kabila lilianza kwenye vita na taasis za kidini. Dola za kidini ni dola imara sana, zipo karne na karne, ni kongwe kuliko dola za kisecular. Na tunajifunza pia dola hizi zimepitia changamoto nyingi sana lakin hazikufa na ziliendelea kuwa imara. Tunashauri serikali hii sikivu ijifunze kitu hapa kuhusu kuheshimu taasisi za kidini na viongozi wao.
Inapotokea kiongozi amekosea awajibishwe kwa sheria zilizopo, lakini si kwa dhihaka,kisasi au ubambikiwaji wa mashtaka. Huwezi jua yupi ana connection ya kiroho na muumba wake. Askofu Mwamakula alisimikwa wakfu mwaka 2016 na kuwa askofu , anaongoza kanisa na ana waumini wake anaowaongoza hapa nchini, alishakuwa mkuu wa chuo St John.
Ile kauli ya anayejiita askofu ni kejeli na dharau sana kwa wafuasi na kanisa lake, zile sarakasi za Gwajima pale Central na makosa yasiyoeleweka toka kwa Bashite na kauli ya Jiwe kuwa "I wish I could be IGP" BADO NI DHARAU KWA WALE WAUMIN WALIOKUJA KUJUA HATMA YA KIONGOZI WAO. Sijamuongelea Sheikh Ponda bado, Askofu Kakobe na TRA kufukua akaunti za kanisa lake na kutaja hadharani kiasi kilichopo benki, Askofu aliyetaka kupewa kesi ya Uraia na wengineo.
[Askofu Emmaus B. Mwamakula alikamatwa wiki ya mwisho ya mwezi Februari. Mapolisi wa Jiwe wakamdhihaki eti "Yule anayejiita Askofu" tunamhoji. Niliposikia vile nikajua sasa Meko ame cross red line. Meko Hakumaliza hata wiki mbili tena.
Alipotoka askofu aliandika ujumbe mzito akamaliza na Mwanakondoo ameshinda Tumfuate!
Baada ya hapo Jiwe akatoa mashambulizi dhidi ya Maaskofu pale St Peters kuhusu uvaaji wa barakoa na hii ni baada ya Niwemugizi Kutangaza orodha ya watawa waliokufa kwa corona ndani ya muda mfupi. Zile zilikuwa ni kejeli dhidi ya maaskofu wa Kikatoliki siku aliposimama pale madhabahuni St Peters Oysterbay mbele ya waumini na wafuasi wa kanisa na taifa kwa ujumla.
Tuliosoma definition ya History tunakumbuka kuwa ni study of past events, lakini pia tunaambiwa tunajifunza history ili tuweze kupredict the future lakin pia kujifunza failures na mafanikio ya tunaowasoma.
Hili la ubabe, dharau na kejeli kwa viongozi au taasis za kidini tunashauri Serikali chini ya mama iliangalie sana maana hata Kongo anguko la kabila lilianza kwenye vita na taasis za kidini. Dola za kidini ni dola imara sana, zipo karne na karne, ni kongwe kuliko dola za kisecular. Na tunajifunza pia dola hizi zimepitia changamoto nyingi sana lakin hazikufa na ziliendelea kuwa imara. Tunashauri serikali hii sikivu ijifunze kitu hapa kuhusu kuheshimu taasisi za kidini na viongozi wao.
Inapotokea kiongozi amekosea awajibishwe kwa sheria zilizopo, lakini si kwa dhihaka,kisasi au ubambikiwaji wa mashtaka. Huwezi jua yupi ana connection ya kiroho na muumba wake. Askofu Mwamakula alisimikwa wakfu mwaka 2016 na kuwa askofu , anaongoza kanisa na ana waumini wake anaowaongoza hapa nchini, alishakuwa mkuu wa chuo St John.
Ile kauli ya anayejiita askofu ni kejeli na dharau sana kwa wafuasi na kanisa lake, zile sarakasi za Gwajima pale Central na makosa yasiyoeleweka toka kwa Bashite na kauli ya Jiwe kuwa "I wish I could be IGP" BADO NI DHARAU KWA WALE WAUMIN WALIOKUJA KUJUA HATMA YA KIONGOZI WAO. Sijamuongelea Sheikh Ponda bado, Askofu Kakobe na TRA kufukua akaunti za kanisa lake na kutaja hadharani kiasi kilichopo benki, Askofu aliyetaka kupewa kesi ya Uraia na wengineo.