Dharau za Ndugai kwa Watanzania zimepitiliza

mcoloo

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
918
1,401
Tuta sema ukweli hata kama ni mchungu.

Huyu Ndugai anayedai kuwa anajua maana ya kufundwa mbona wakati wa kampeni za 2015 alimpiga fimbo ya kichwani mgombea mwenza hadi akazimia na kulazwa hospitali.

Kitendo hicho cha kishenzi kilitosha kumnyima nafasi ya kuwa spika.

Ndugai lazima afahamu kuwa CHADEMA Ina mamilioni ya wafuasi na kama zitafanywa takwimu huwenda kwa sasa CHADEMA ndicho chama chenye wanachama wengi kuliko chama chochote cha siasa hapa nchini ukiwa ni pamoja na hilo liCCM lake linalomtia kiburi.

Ndugai anamshambulia Mbowe kana kwamba maamuzi ya kuwafurumsha uanachama COVID 19 ulikuwa wa Mbowe na wala sio wa CC ya CHADEMA.

Leo ndo Ndugai ajifanya kuwaonea huruma wanawake kwa sababu tu ameshiriki nao kufanya uharamia wa kisiasa.

Nchi imefikia kuwa sasa inaongozwa kwa matakwa tu ya kakikundi fulani tena bila kujali kuwa tuna Sheria mama inayostahili kuwa mwongozo wetu kama taifa.

Kwa hili la kudharau Sheria za nchi linafaa kukemewa na kila mzalendo wa nchi hii, kwani kwa kuinajisi katiba sio tu kuwa ni kwa kuikomoa CHADEMA Bali Ni dharau kwa Watanzania wote awe CCM au hata chama kingine chochote cha siasa.

Nchi imefikia kuwa kila kiongozi aliye kada wa CCM kuanzia kwa mabalozi wa nyumba kumi hadi Mwenyekiti wa chama Taifa kuwa wao ndio katiba kila wanalo lilisema ndio Sheria ya nchi hii kweli?

Kwa ushauri tu ni kwamba Ndugai atoke hadharani na kuomba msamaha kwa Watanzania kwa yale aliyo yatamka, pia ajue kuwa amekuwa na vijikauli vya hovyo hovyo vingi ambavyo vina ishi ndani ya mioyo ya Watanzania.
 
Wewe na wenzako Mlijiandaa kwanza tupigane sisi kwa sisi, nalo halijatokea, sasa mlijiandaa ili nchi isitawalike nalo halijatokea, sasa mnataka kumalizia hasira zenu kwa akina Halima nalo limeshindikana
 
ndiyo shida za nchi ilipo. Hamuoni tatizo analolifanya ndugai ?!. Wamejitungia sheria ya kutokushtakiwa mnaona poa tu !!. Elimu ya shule za kata imeleta majanga . Unakuwa na wananchi hawaoni viongozi wanapofanya madudu kama ndugai & co

Ndugai amevunja katiba
 
Awamu hii , katiba inategemea wanavyotafsiri hawa viongozi wa awamu ya tano.

Yoote haya wanayafanya kwa kujua mahakama zetu haziko huru .
Mzembe mkuu katika nchi ni rais, Rais wa nchi huwezi kuwaacha watu wanabagaza katiba katika level hii. Rais tangu ameapishwa yupo kimya mno. Watueleze ni Mgonjwa au alisha wahi mbele ya haki. nchi inapoteza mwelekeo
 
Me nawaambia kila siku,bila bunduki hao watu hawatakuwa na heshima.Bunduki zichezwe hata miaka 3 heshima itarudi.This time ni wafalme hao watu
 
Aina yenu ndiyo shida za nchi ilipo. Hamuoni tatizo analolifanya ndugai ?!. Wamejitungia sheria ya kutokushtakiwa mnaona poa tu !!. Elimu ya shule za kata imeleta majanga . Unakuwa na wananchi hawaoni viongozi wanapofanya madudu kama ndugai & co

Ndugai amevunja katiba

Kwani Tanzania ndo ncho pekee ambayo ina sheria ya kutoshtakiwa? umesema chadema ina wanachama wangap eti?
 
Aina yenu ndiyo shida za nchi ilipo. Hamuoni tatizo analolifanya ndugai ?!. Wamejitungia sheria ya kutokushtakiwa mnaona poa tu !!. Elimu ya shule za kata imeleta majanga . Unakuwa na wananchi hawaoni viongozi wanapofanya madudu kama ndugai & co

Ndugai amevunja katiba

Elimu yetu ndiyo chanzo cha yote! Umemaliza! Utashangaa ukienda NEC kuna Dr. anafanya mambo ya hovyo hovyo!!
Jiwe nae ana PhD daaaah!!
Ana timu ya watu wanajiita maDr.
Bungeni kuna Dr. wasiopungungua 10 na mapropesa wasiopungua watano! Wanapigia makofi haya matendo!!

Elimu ya Mtanzania bado ni janga! Wasomi ndiyo wanaongoza kubananga katiba, bora kurudisha wenye elimu ya kawaida wana akili ya maamuzi kuendana na katiba na sheria!

Wakati huu ndiyo naelewa kwanini katika wapigania uhuru wote Africa hakukuwa na Daktari hata mmoja (wengine walipata PhD baadae sana)! Nimeanza kuelewa sasa
 
Mzembe mkuu katika nchi ni rais, Rais wa nchi huwezi kuwaacha watu wanabagaza katiba katika level hii. Rais tangu ameapishwa yupo kimya mno. Watueleze ni Mgonjwa au alisha wahi mbele ya haki. nchi inapoteza mwelekeo
Jiwe anapenda aina za kina Ndugai kwani yeye nae ni mvunja katiba tena kwa kukejeli watu.
 
Back
Top Bottom