MWITONGO MAARIFA
JF-Expert Member
- Aug 11, 2018
- 276
- 1,428
Sasa hivi kila mtu ni mtakatishaji fedha na muhujumu uchumi na hakuna dhamana kwao. Ukijiuliza haya makosa yanatokea wapi unagundua DPP ndizo kesi anazofungua baada ya kujua akifika mahakamani anakwenda kukataa wahusika wasipewe dhamana.
Leo hii hata ukipewa maelekezo haramu ukayakataa kitakachofuata ni kufunguliwa uhujumu uchumi ukose dhamana na ndugu zako pamoja na familia wakae meza moja na wakubwa wajadiliane.
Uhujumu uchumi imekuwa ni kigezo Cha serikali kudai rushwa kwa wananchi na wakaazi wa Tanzania na kibaya zaidi wanaoomba fedha wamehalalisha mtindo kwa kusaidiwa na mahakama.
Ifike mahali mawakili wasomi wakaona ni namna gani wanazipitia sheria zinazowanyima watu ambao ni watuhumiwa dhamana kuepusha kazia hii.
Sheria hizi Leo zinaonekana ni tamu kwa watawala na baadhi ya watendaji mahakamani hawazioni kama ni tatizo hadi pale watakapokamatwa na kutundikiwa dripu ya uhujumu uchumi ndo watatambua madhara yake.
Ni vyema tukaandaa mazingira ya kisheria yaliyosafi Sasa kabla hatujaumizwa na sheria tunazoona leo si kandamizi.
Sent using Jamii Forums mobile app
Leo hii hata ukipewa maelekezo haramu ukayakataa kitakachofuata ni kufunguliwa uhujumu uchumi ukose dhamana na ndugu zako pamoja na familia wakae meza moja na wakubwa wajadiliane.
Uhujumu uchumi imekuwa ni kigezo Cha serikali kudai rushwa kwa wananchi na wakaazi wa Tanzania na kibaya zaidi wanaoomba fedha wamehalalisha mtindo kwa kusaidiwa na mahakama.
Ifike mahali mawakili wasomi wakaona ni namna gani wanazipitia sheria zinazowanyima watu ambao ni watuhumiwa dhamana kuepusha kazia hii.
Sheria hizi Leo zinaonekana ni tamu kwa watawala na baadhi ya watendaji mahakamani hawazioni kama ni tatizo hadi pale watakapokamatwa na kutundikiwa dripu ya uhujumu uchumi ndo watatambua madhara yake.
Ni vyema tukaandaa mazingira ya kisheria yaliyosafi Sasa kabla hatujaumizwa na sheria tunazoona leo si kandamizi.
Sent using Jamii Forums mobile app