Dhana ya Serikali kutokuwa na Dini au Serikali ya Kisekula

wimbi la mbele

JF-Expert Member
Jan 4, 2011
647
266


GREAT THINKERS. Naamimi sisi ni watu ambao tunaupeo mkubwa kuliko vyombo vya habari vilivyojaa proganda na waandishi uchwara ambao hawapendi kuuliza maswali wala kuwa na ma critical thinkers.

Nadhani siko peke yangu ninaliyechoshwa na upuuzi na propaganda toka wa wanasiasa wetu wa CC, CHADEMA na vyama vyote vya siasa kuwa serikali haina dini lakini raia wake wanazo dini.

Dhana hiyo ni maarufu Tanzania. Mara nyingi katika masuala yahusuyo dini, viongozi wa serikali husikika wakisema «serikali haina dini, ila wananchi wake wana dini zao


Hoja ya usekula wa serikali ni ya kihistoria. Ilijengwa kiasi cha miaka miambili iliyopita ikitaka serikali ijiepushe na shughuli za kidini hususan katika masuala ya elimu, mafundisho ya maadili na na ibada.
Japokuwa Tanzania imekuwa ikidai kwamba serikali yake ni ya kisekula, hali halisi haioneshi hivyo. Pamoja na madai hayo, serikali ya Tanzania imewahi kuingia katika msuguano na Waislamu na baadhi ya wasiokuwa waislamu pale Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ilipotaka kuanzisha somo la dini au maadili ya nchi. Kadhia hii ni maarufu kwa jina la “dini mseto”. serikali ya kisekula haiwezi ikaja na mipango ya kusomesha dini kwa jina lolote lile liwe la maadili au vyovyote vile.
Mifano mingine inayotia wasiwasi usekula wa serikali ya Tanzania ni hii ifuatayo:
1. Wimbo wa Taifa – unaomba mungu aibariki nchi

2. Dua ya Bungeni – ina muomba mungu

3. Idara za serikali kutenga mabilionioni kwa ajili ya sherehe za kidini




3. Kuapishwa kwa wanaochukua nafasi za uongozi. Japo wanaoapa huapa kwa dini zao, aneapisha si kiongozi wa dini husika bali wa serikali au wa bunge.




Utaratibu huo hauendani na madai kuwa nchi au serikali ya Tanzania haina dini, bali wananchi wake ndiyo wenye dini.

Swali ni je, tunapomtaja Mungu katika wimbo wa taifa



au katika dua ya bungeni, na kadhalika, tunamkusudia mungu yupi?

1.Mungu wa Waislamu?

2.Wa Wakristo?

3.Wa dini za asili?

Je, kuna mungu wa kitaifa? Mungu huyo wa kitaifa ni yupi na ni wa dini gani?



Je, katika hali hiyo, ni kweli serikali haina dini?


Hivi kwa nini hawa wanasiasa wa CCM, CHADEMA na vyama vingine wanapenda kutufanya sisi wajinga?
 
umetugusa sana mkuu

Lakini hilo la kuwaunganisha CHADEMA na CCM umemaliza maana wote wapo kwa ajili ya kutetea maslahi yao
 
Kuna tofauti kati ya Serikali ya nchi kuwa na dini rasmi (k.m. Jamhuri ya Kiislam ya Iran) na nchi kutowanyima watu wake uhuru wa kuabudu. Watu wako huru kuwa na imani kadri wanavyoona inafaa na serikali haiingilii kuwaelekeza ni imani ipi iliyo bora kuliko zingine. Huko ndiyo serikali kutokuwa na dini. Tanzania inatambua kuwepo kwa dini nyingi lakini haiipi upendeleo dini mojawapo. Kuala kihapo kwa kutumia misahafu na kumtaja Mungu katika wimbo wa taifa siyo sawa na serikali kuwa na dini. Dini nyingi ninazozijua zikiwemo baadhi ya dini zetu za jadi zinamtambua Mungu mmoja. Uislam, Ukristo, Uyahudi, n. k. ni tofauti zilizotokana na mapungufu ya kibinadamu zikiwemo uchu wa madaraka, kiburi, dharau, ubaguzi, tofauti za tamaduni, n.k. Dhana yetu ni tofauti na Ukomunisti ambao unasema wazi kabisa kuwa hauamini kuwepo kwa Mungu.
 
Kuna tofauti kati ya Serikali ya nchi kuwa na dini rasmi (k.m. Jamhuri ya Kiislam ya Iran) na nchi kutowanyima watu wake uhuru wa kuabudu. Watu wako huru kuwa na imani kadri wanavyoona inafaa na serikali haiingilii kuwaelekeza ni imani ipi iliyo bora kuliko zingine. Huko ndiyo serikali kutokuwa na dini. Tanzania inatambua kuwepo kwa dini nyingi lakini haiipi upendeleo dini mojawapo. Kuala kihapo kwa kutumia misahafu na kumtaja Mungu katika wimbo wa taifa siyo sawa na serikali kuwa na dini. Dini nyingi ninazozijua zikiwemo baadhi ya dini zetu za jadi zinamtambua Mungu mmoja. Uislam, Ukristo, Uyahudi, n. k. ni tofauti zilizotokana na mapungufu ya kibinadamu zikiwemo uchu wa madaraka, kiburi, dharau, ubaguzi, tofauti za tamaduni, n.k. Dhana yetu ni tofauti na Ukomunisti ambao unasema wazi kabisa kuwa hauamini kuwepo kwa Mungu.

Nadhani kuna umuhimu wa separation ya haya mambo

lakini sio kuongopeana
 
Ndipo Waislamu wakatetea uwepo na utambulikanaji wao ndani ya Katiba wakiwa na madai yenye msingi ,kwani wamechoka kuambiwa serikali haina dini ,vipi serikali haina dini inawahukumu wenye dini na kusema huna dini ni dini vilevile.
 
Ni kweli kabisa na nivizuri yukaeleweshwa kwa sababu Mungu wa Wakristo na mungu wa waislam ni tofauti, sasa inapofika bunge linaomba kwa mungu na wimbo wa taifa unamtaja mungu ni mungu yupi?

Nathubutu kusema ndo maana nchi inazidi kuchanganyikiwa kwa sabubu haijui inamuomba mungu yupi
 
Ulichosema ni sawia kabisa. Mungu anayetajwa katika wimbo wa Taifa wenu ni Mungu Gani?
 
Wanasiasa huwa na propoganda nyingi ili watawale kwa urahisi.
 
Back
Top Bottom