Leslie Mbena
JF-Expert Member
- Nov 24, 2019
- 207
- 677
DHANA YA "MKONO MTUPU HAULAMBWI" YAENDELEA KUONEKANA KATIKA KURA ZA MAONI.
Leo 20:45pm 21/07/2020
Nimeamini aliyevaa kiatu ndie mwenye kujua kiatu kinabana wapi,nimeshiriki katika kura za maoni juzi nikiwa na mapenzi tu ya Jimbo langu la Morogoro kichwani nikijua sasa naenda kuwaeleza wana Morogoro kinachowasibu hadi Mkoa wa Morogoro unadumaa kiuchumi,na wakinielewa basi wanipe kura,cha ajabu nimepata kura 1.
Nilianza kujinadi kwa kuwashukuru wajumbe wote wa mkutano kwa kunilea nikiwa mdogo,sisi tuliozaliwa miaka ya 1980 tulilelewa na kila mtu mtaani enzi za Ujamaa,ni fahari na heshima kuwashukuru,nimesoma na kukulia Morogoro niliwaambia sasa nina kazi na nitawalea,
Licha ya kuwashukuru nikawaambia matatizo ya Morogoro ni Ajira na mzunguko duni wa fedha,Ndio maana hivi leo watoto wote wa Morogoro wanafanya kazi Dar es Salaam na wamelowea uko tatizo likiwa Viwanda vinavyotoa ajira Morogoro vimekufa,vilibinafsishwa na aliyenunua kaviua ndiye Mbunge wa mioyo yao.
Nikawaambia kura yenu ni hatma ya watoto na wajukuu zenu,kesho watamaliza Shule watakosa ajira,ni vyema wakaonyesha kwa vitendo kumkataa aliyeua Viwanda na kumchagua mtu mwingine Mzalendo ili ajenge msingi wa kuanzisha Viwanda vipya,kwa ajili ya ajira kwa watoto,wajukuu na kizazi kijacho,
Niliwaambia kwa miaka mingi Morogoro ni kama kidonda kilichokosa dawa,naomba mnipe kura nikawe dawa,kweli niliongea kwa uchungu na watu walinyamaza na kuniangalia tu,sikujua walikuwa wanawaza nini,hadi mwisho nilipopata kura moja ndio nilijua kuwa wajumbe walikuwa wananionea huruma tu wao tayari walikuwa wakijua nini wanakwenda kufanya,
Asikwambie mtu wajumbe wanaopiga kura wenyewe hawajui cha huyu ni Mzalendo anatuambia kitu cha maana tumpe kura atusaidie kuiponya Morogoro ndipo nilipojua mkono mtupu haulambwi,uwezi amini kuna wajumbe wengine hawajui kama kuna mtu anaitwa Magufuli wala Majaliwa nikimaanisha zama za Wito na Uzalendo na si pesa ndio uwe kiongozi katika hii nchi,wao wapo kulamba mkono wako tu.
Niliulizwa na baadhi ya wajumbe "Mjomba mbona hujatutembelea" nikawaambia nilijua tunakutana hapa ukumbini na kufahamiana wakati wa kujieleza,cv yangu ipo kwenye form,mnanifahamu mimi kijana wenu nimekulia kichangani,na screening nimefanyiwa,wakaniambia Mjomba ungezungukia wajumbe wote,nikagundua ili ushinde kura za maoni lazima uzunguke wakulambe mkono,ni lazima uwe na hela na uwape wale viongozi wao kisha wao ndio watawapa hela watu wao,
-Tathmini yangu,live kabisa.
Matokeo ya kura za maoni maeneo mengi hasa Morogoro yameonyesha kuwa harakati za Rais Magufuli za Chama kuwa cha Wakulima na Wafanyakazi bado hazijafika wilayani,kata na matawini,ndio maana Katibu Mwenezi atapanda Jukwaani na kusema "mnaniona Mimi,Mimi nalelewa na Wazee wa Morogoro,mimi nakula vizuri,
Hili ni gamba la ile CCM ya zamani kwa maana ya mkono mtupu haulambwi,mwenye pesa ndio atawatunza na kuwalea kwa hiyo Wazalendo wa kweli hatuna nafasi kuleta mabadiliko na mawazo mbadala kwa ajili ya kuleta chachu ya Maendeleo Mkoani Morogoro,naungana na Mwenyekiti kukata kila aliyepata kura nyingi kwa pesa na bahati nzuri wanajulikana hata kwa historia zao za nyuma,japo historia za nyuma haziwezi kumfunga mtu.
Matumaini pekee ya kuibadilisha CCM ya Wilayani,Kata na tawi na kuwa ccm mpya itakayoendelea kujali maslahi ya nchi kama enzi za Mwalimu Julius Nyerere na Wakati huu wa Rais John Magufuli yamebakia mikononi mwake Rais na Mwenyekiti John Magufuli mwenyewe.
Kinyume na hapo matokeo ya ubunge na udiwani maeneo mengi yakibakia kama yalivyotoka kwenye kura za maoni kwa maana ya wa kwanza ndio wa kwanza kweli hadi wakati wa uchaguzi mkuu basi CCM itabakia na sura ileile na matendo yaleyale hatari kwa uhai wa CCM ya baada ya Mwalimu Julius Nyerere na kabla ya Rais John Magufuli.
-Hatma ya CCM
Kama ccm itarudi kulekule kwenye Azimio la Zanzibar yaani CCM ya wafanyabiashara baada ya Rais John Magufuli kuondoka,hali hii itasababisha kuibuka kwa makundi makubwa mawili ndani ya CCM kwa maana ya CCM mpya safi ya watu wenye mtazamo wa Mwalimu Julius Nyerere na Rais John Magufuli,
Kundi lingine likiwa la ile CCM chukua chako mapema iliyokuja baada ya Mwalimu Julius Nyerere na kabla ya Rais John Magufuli na kudumu kwa miaka 30 ikitapanya rasilimali za nchi yetu hadi ikawaudhi wananchi kiasi cha kuwa tayari hata kuchagua jiwe badala ya CCM,tujihadhari na kurudi huku.
Matendo yale baada ya Azimio la Zanzibar ya Wafanyabiashara kuhodhi Madaraka ndani ya CCM na Serikali ni hatari kwa uhai wa chama na Taifa.
Nimalizie kwa kijembe iki nilichopigwa na mjumbe mmoja pengine ndiye aliyenipa kura moja,"Umeifanyia nini Morogoro wewe,
Sikutegemea mtu kama wewe unaejitambua kwa kiasi kikubwa kujipeleka tu hujawahi hata kukutana na wajumbe wa mkutano mkuu wa kata unaenda tu kwa vile unafikiri ukiongea kwa dakika moja utaweza kupindua meza ya mbunge mwenye mabus anayetoaga kwenda kuzikia,uwaconvince watu wakuchague"
Tatizo wengi mliokuja kuchukua fomu mnawaza kama wagombea na sio kama wapiga kura,wapiga kura ni wajumbe,wengi la saba,hawana mshahara wao uchaguzi ndio mavuno yao,wewe unakuja,umeongea kitu kimewachoma hadi ukumbi ukanyamaza lakini mwisho ukaambulia kura 1"
Kwa maisha hayo ya kutaka kula bila kuliwa uliyochagua uwezi kushinda kura za maoni ila endelea kuishi maisha ya furaha sana,usiwe kinyongo aisee,Hongera pia huna hasira ni mtu wa kucheka na kuchukulia powa kila jambo, wenye kuyaweza maisha hayo Ni wale tu wanaoamwamini Mungu,Mungu akubariki na karibu Morogoro.
Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854
-Bachelor of Business Administration in International Business.
-Master's in Leadership and Management.
-Research; Assessing Effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.
Leo 20:45pm 21/07/2020
Nimeamini aliyevaa kiatu ndie mwenye kujua kiatu kinabana wapi,nimeshiriki katika kura za maoni juzi nikiwa na mapenzi tu ya Jimbo langu la Morogoro kichwani nikijua sasa naenda kuwaeleza wana Morogoro kinachowasibu hadi Mkoa wa Morogoro unadumaa kiuchumi,na wakinielewa basi wanipe kura,cha ajabu nimepata kura 1.
Nilianza kujinadi kwa kuwashukuru wajumbe wote wa mkutano kwa kunilea nikiwa mdogo,sisi tuliozaliwa miaka ya 1980 tulilelewa na kila mtu mtaani enzi za Ujamaa,ni fahari na heshima kuwashukuru,nimesoma na kukulia Morogoro niliwaambia sasa nina kazi na nitawalea,
Licha ya kuwashukuru nikawaambia matatizo ya Morogoro ni Ajira na mzunguko duni wa fedha,Ndio maana hivi leo watoto wote wa Morogoro wanafanya kazi Dar es Salaam na wamelowea uko tatizo likiwa Viwanda vinavyotoa ajira Morogoro vimekufa,vilibinafsishwa na aliyenunua kaviua ndiye Mbunge wa mioyo yao.
Nikawaambia kura yenu ni hatma ya watoto na wajukuu zenu,kesho watamaliza Shule watakosa ajira,ni vyema wakaonyesha kwa vitendo kumkataa aliyeua Viwanda na kumchagua mtu mwingine Mzalendo ili ajenge msingi wa kuanzisha Viwanda vipya,kwa ajili ya ajira kwa watoto,wajukuu na kizazi kijacho,
Niliwaambia kwa miaka mingi Morogoro ni kama kidonda kilichokosa dawa,naomba mnipe kura nikawe dawa,kweli niliongea kwa uchungu na watu walinyamaza na kuniangalia tu,sikujua walikuwa wanawaza nini,hadi mwisho nilipopata kura moja ndio nilijua kuwa wajumbe walikuwa wananionea huruma tu wao tayari walikuwa wakijua nini wanakwenda kufanya,
Asikwambie mtu wajumbe wanaopiga kura wenyewe hawajui cha huyu ni Mzalendo anatuambia kitu cha maana tumpe kura atusaidie kuiponya Morogoro ndipo nilipojua mkono mtupu haulambwi,uwezi amini kuna wajumbe wengine hawajui kama kuna mtu anaitwa Magufuli wala Majaliwa nikimaanisha zama za Wito na Uzalendo na si pesa ndio uwe kiongozi katika hii nchi,wao wapo kulamba mkono wako tu.
Niliulizwa na baadhi ya wajumbe "Mjomba mbona hujatutembelea" nikawaambia nilijua tunakutana hapa ukumbini na kufahamiana wakati wa kujieleza,cv yangu ipo kwenye form,mnanifahamu mimi kijana wenu nimekulia kichangani,na screening nimefanyiwa,wakaniambia Mjomba ungezungukia wajumbe wote,nikagundua ili ushinde kura za maoni lazima uzunguke wakulambe mkono,ni lazima uwe na hela na uwape wale viongozi wao kisha wao ndio watawapa hela watu wao,
-Tathmini yangu,live kabisa.
Matokeo ya kura za maoni maeneo mengi hasa Morogoro yameonyesha kuwa harakati za Rais Magufuli za Chama kuwa cha Wakulima na Wafanyakazi bado hazijafika wilayani,kata na matawini,ndio maana Katibu Mwenezi atapanda Jukwaani na kusema "mnaniona Mimi,Mimi nalelewa na Wazee wa Morogoro,mimi nakula vizuri,
Hili ni gamba la ile CCM ya zamani kwa maana ya mkono mtupu haulambwi,mwenye pesa ndio atawatunza na kuwalea kwa hiyo Wazalendo wa kweli hatuna nafasi kuleta mabadiliko na mawazo mbadala kwa ajili ya kuleta chachu ya Maendeleo Mkoani Morogoro,naungana na Mwenyekiti kukata kila aliyepata kura nyingi kwa pesa na bahati nzuri wanajulikana hata kwa historia zao za nyuma,japo historia za nyuma haziwezi kumfunga mtu.
Matumaini pekee ya kuibadilisha CCM ya Wilayani,Kata na tawi na kuwa ccm mpya itakayoendelea kujali maslahi ya nchi kama enzi za Mwalimu Julius Nyerere na Wakati huu wa Rais John Magufuli yamebakia mikononi mwake Rais na Mwenyekiti John Magufuli mwenyewe.
Kinyume na hapo matokeo ya ubunge na udiwani maeneo mengi yakibakia kama yalivyotoka kwenye kura za maoni kwa maana ya wa kwanza ndio wa kwanza kweli hadi wakati wa uchaguzi mkuu basi CCM itabakia na sura ileile na matendo yaleyale hatari kwa uhai wa CCM ya baada ya Mwalimu Julius Nyerere na kabla ya Rais John Magufuli.
-Hatma ya CCM
Kama ccm itarudi kulekule kwenye Azimio la Zanzibar yaani CCM ya wafanyabiashara baada ya Rais John Magufuli kuondoka,hali hii itasababisha kuibuka kwa makundi makubwa mawili ndani ya CCM kwa maana ya CCM mpya safi ya watu wenye mtazamo wa Mwalimu Julius Nyerere na Rais John Magufuli,
Kundi lingine likiwa la ile CCM chukua chako mapema iliyokuja baada ya Mwalimu Julius Nyerere na kabla ya Rais John Magufuli na kudumu kwa miaka 30 ikitapanya rasilimali za nchi yetu hadi ikawaudhi wananchi kiasi cha kuwa tayari hata kuchagua jiwe badala ya CCM,tujihadhari na kurudi huku.
Matendo yale baada ya Azimio la Zanzibar ya Wafanyabiashara kuhodhi Madaraka ndani ya CCM na Serikali ni hatari kwa uhai wa chama na Taifa.
Nimalizie kwa kijembe iki nilichopigwa na mjumbe mmoja pengine ndiye aliyenipa kura moja,"Umeifanyia nini Morogoro wewe,
Sikutegemea mtu kama wewe unaejitambua kwa kiasi kikubwa kujipeleka tu hujawahi hata kukutana na wajumbe wa mkutano mkuu wa kata unaenda tu kwa vile unafikiri ukiongea kwa dakika moja utaweza kupindua meza ya mbunge mwenye mabus anayetoaga kwenda kuzikia,uwaconvince watu wakuchague"
Tatizo wengi mliokuja kuchukua fomu mnawaza kama wagombea na sio kama wapiga kura,wapiga kura ni wajumbe,wengi la saba,hawana mshahara wao uchaguzi ndio mavuno yao,wewe unakuja,umeongea kitu kimewachoma hadi ukumbi ukanyamaza lakini mwisho ukaambulia kura 1"
Kwa maisha hayo ya kutaka kula bila kuliwa uliyochagua uwezi kushinda kura za maoni ila endelea kuishi maisha ya furaha sana,usiwe kinyongo aisee,Hongera pia huna hasira ni mtu wa kucheka na kuchukulia powa kila jambo, wenye kuyaweza maisha hayo Ni wale tu wanaoamwamini Mungu,Mungu akubariki na karibu Morogoro.
Nikiishia hapa,Mimi ni
Msemakweli Chakubanga,
Dar es Salaam.
0755078854
-Bachelor of Business Administration in International Business.
-Master's in Leadership and Management.
-Research; Assessing Effects of Micro-Financing on Poverty Reduction.