Dhana ya Kuinuana Kiuchumi baina ya Wanafamilia; Kuna haja unapompa ndugu yako Mtaji wa biashara umtoze riba ili kuongeza uwajibikaji?

Binafsi naamini kwenye familia, mmoja anaweza kuinuliwa ili aweze kuwainua wengine. Ndiyo maana kwenye maandiko Kitabu cha Mwanzo 42:25-28 unaona Yusufu alivyoinuliwa ili kuwasaidia ndugu zake. Kuna mtu anaweza kujiuliza kwani ni lazima kuwasaidia ndugu zako, Jibu sio lazima (Sijui kama kuna sheria inayolazimisha ndugu kusaidiwa hata Baba/Mama sio lazima) kuwasaidia lakini unajiuliza ni faida kiasi gani unapata kuona ndugu zako wakihangaika mitaani bila mafanikio wakati wewe ukiwa na nafuu?

Binafsi nimejaribu mara kadhaa kuwainua ndugu zangu (Tumbo moja) bila mafanikio mwisho wa siku najikuta napoteza mitaji tu. Natolea mfano, mwaka fulani nilimpa brother angu mtaji wa kumwezesha afanye biashara fulani iliyonigharimu kiasi. Bahati mbaya biashara akaiua/akala mtaji. Next time, nikampa mtaji mdogo wangu afanye biashara fulani aliyoitaka. Bahati mbaya naye akapoteza mtaji bila kufanikiwa. Simu za brother zikawa nyingi kuomba assistance huku akinishtakia kwa Wazee. Baada ya mivutano kidogo nikampa mtaji mwingine. Shida inakuja kwenye suala la kuikuza biashara na kuiendeleza, brother anafail, Kwahiyo baada ya muda mtaji huu pia ukafa.

Sasa nimempa mtaji wa mwisho wa biashara, akipoteza na huu Potelea mbali. Sitajali lawama za Walimwengu, hata Mungu anaona nilivyojitolea.

Swali, Je, kuna haja ya tunapowapa mitaji ndugu zetu(tuandikishiane) na tuanze kutoza riba ili kuongeza uwajibikaji (accountability)?? Jambo hili litakuwa na athari zozote kwa ustawi na mahusiano ya familia?
Naogopa kusema kuwa kama siyo wewe ni wakufaa kulaumiwa kwenye mkwamo wake basi wewe haukuwa msaada sahihi wa tatizo lake .

Nikama natamani kukuuliza maswali matatu madogo yahusuyo chanzo cha mafanikio yako na weredi wa uliyemsaidia :-

1.
(a) Mafanikio yako yametokana na (ELIMU) bila kujali ukubwa wa mshahara wako (ninachotaka kusema hapa nikuwa ,wenda uwelimu yako imekusaidia kujitambua na kukuongezea umakini .

(b) Au ulifanikiwa tu kwa kudra za Mwenyezi Mungu plus ujanja ujanja?

2.
(a) Msaidiwa anakiwango gani cha elimu ,anaujuzi wowote?

(b) Ulimsaidia kwa kumuwekezea kwenye kile alicho na ujuzi nacho , wewe ndiye uliyempangia chakufanya au ulimsaidia fedha kisha yeye asonge zake tu kwa kudra za Mungu?

3.
(a) Baada ya kumsaidia fedha /mali ulimsaidia ,pia kumpa usimamizi wa karibu juu ya kumfanikishia kuzifikia ndoto zake ? Au ulimpa ili tu uondoe lawama kwa family ?

Sitaki kusema watu wengi hasa tunaojiita watoa msaada wa family zetu ndiyo haswa huwa vyanzo vikuu vya kudumaza ndoto na ustawi wa family zetu .

Wengi wetu hasa waafrika tunahulka za UBINAFSI ,wengi huwa tunataka kuonekana miungu watu kwenye family zetu kutokana na aidha vyeo au mali tulizonazo na hata pale tunapotakiwa au tunapowasaidia wengine huwa tunafanya hivyo lakini siyo kwa dhamira zetu za ndani ,lengo kubwa ni washindwe ili tujidhihirishe kwao na kwakuokoo kuwa Mafanikio siyo lelemama

NAOGOPA KUHITIMISHA KWA KUSEMA MTOA MADA HUWA HAITOI MISAADA YAKE KWA LENGO LA DHATI LA KUMSAIDIA MWWNAFAMILY WAKE AFANIKIWE BALI NI KWA LENGO LA KUTAKA KUJIONDOA KWENYE KUNDI LA LAWAMA .

Binafsi ninamfano wangu kwa mdogo wangu wa kike aliyekuwa ameishia form four wakati ule , na kupachikwa mimba ,kwababhati mbaya aliyempa mimba alipoteza mvuto nae ndani ya muda mfupi Baada ya kujifungia na akahamishia mahaba kwa mschana mwingine ,kwetu halikuwa kosa , tatizo lilianzia pale mdogo wetu alipoomba apewe mtaji , sisi tukamwambia kwa sasa hana sifa ya kupewa mtaji hadi hapo atakapotimiza vigezo , na kigezo No 1 akubali kuendelea na shule au arudi nyumbani na kukaa miaka miwili ili achunguzwe ili tuone kama atakuwa na sifa zitakazomfanya apewe msaada .

Alikubali kurudi shule na kuendelea na form five na six na hata chuo .

Wakati yupo chuo alichagua kuwa mtabibu ,hii ilimfanya boom lake la kwanza aliwekeze kwenye duka la madawa baridi na Baada ya muda kidogo akatushawishi tumuongezee nguvu kwenye biashara yake hiyo ,Baada ya maswali mawili matatu tulijiridhisha nakumsaidia kutimiza hitaji lake huku tukimsaidia kumpa mbinu kadhaa za kiushindani zikiwemo kuweka record za wagonjwa anaowahudumia ,anuani za wanakotoka pamoja na history za magonjwa yanayowasumbua .

Pia tulimsaidia gari ndogo ili awe anawatembelea kwenye makazi yao walau maramoja kwa wiki sambamba na kuwapelekea walau dawa za kupunguza maumivu na juice za na maji madogo sambamba na kuwapa ushauri wa kitaalamu uhusuyo matatizo yanayowahusu .

Hii ilimjengea jina sana kiasi cha kuongeza idadi ya wateja (wagonjwa) hivyo kulazimika kuongeza eneo la kuwapokea sambamba na kuandaa eneo la kuwapumzisha kwa muda wale ambao wanakuna wakiwa hawako kwenye hali ya kuweza kukaa na sasa anamiliki hospital Arusha na hajawahi kuhangaikia ajira tena serikalini na tatizo lake KIUCHUMI nikama limekwisha kusovika kwa zaidi ya 85% .

Mtoa mada wenda ukawa na chakujifunza , samahanini kwa maelezo MAREFU
 
Binafsi naamini kwenye familia, mmoja anaweza kuinuliwa ili aweze kuwainua wengine. Ndiyo maana kwenye maandiko Kitabu cha Mwanzo 42:25-28 unaona Yusufu alivyoinuliwa ili kuwasaidia ndugu zake. Kuna mtu anaweza kujiuliza kwani ni lazima kuwasaidia ndugu zako, Jibu sio lazima (Sijui kama kuna sheria inayolazimisha ndugu kusaidiwa hata Baba/Mama sio lazima) kuwasaidia lakini unajiuliza ni faida kiasi gani unapata kuona ndugu zako wakihangaika mitaani bila mafanikio wakati wewe ukiwa na nafuu?

Binafsi nimejaribu mara kadhaa kuwainua ndugu zangu (Tumbo moja) bila mafanikio mwisho wa siku najikuta napoteza mitaji tu. Natolea mfano, mwaka fulani nilimpa brother angu mtaji wa kumwezesha afanye biashara fulani iliyonigharimu kiasi. Bahati mbaya biashara akaiua/akala mtaji. Next time, nikampa mtaji mdogo wangu afanye biashara fulani aliyoitaka. Bahati mbaya naye akapoteza mtaji bila kufanikiwa. Simu za brother zikawa nyingi kuomba assistance huku akinishtakia kwa Wazee. Baada ya mivutano kidogo nikampa mtaji mwingine. Shida inakuja kwenye suala la kuikuza biashara na kuiendeleza, brother anafail, Kwahiyo baada ya muda mtaji huu pia ukafa.

Sasa nimempa mtaji wa mwisho wa biashara, akipoteza na huu Potelea mbali. Sitajali lawama za Walimwengu, hata Mungu anaona nilivyojitolea.

Swali, Je, kuna haja ya tunapowapa mitaji ndugu zetu(tuandikishiane) na tuanze kutoza riba ili kuongeza uwajibikaji (accountability)?? Jambo hili litakuwa na athari zozote kwa ustawi na mahusiano ya familia?
Riba haina ulazima sana kwanza ni kuweka mpango mkakati wa muda mrefu kama ndugu kuona kama huo ni utamaduni kunyanyuana siyo kitu cha ajabu saana "kwamba asibaki mtu nyuma" kwa kushindwa kuinuliwa.

Mfano wewe umefanikiwa pengine labda ni biashara ya spare unamchukua ndugu mmoja unamuweka ofsin unampa chakula,maradhi na mavazi humlipi mshahara.

Unafanya naye biashara kwa kipindi cha miaka minne itategemea na ushapu wake ukiona ameiva unamfungulia duka lake spare na yeye anaenda na mfumo huo kwa anayemfuata ukishakuwa ni utamaduni inakuwa ni kitu cha kawaida ndipo neno la kuna familia zimebarikiwa linakuja.
 
Ngoja nisearch nione, huenda ikamsaidia. Ujana Maji ya moto
Wewe ni tatizo pia, tena kubwa tu. Unawezaje kumfanyia babysitting mtu mzima kidume?

Unadhani wewe ni Yesu wa kubeba misalaba ya wengine? Au unadhani unapaswa kuyajali maisha ya mtu mzima zaidi ya yeye mwenyewe?

Kama una pesa zinakusumbua basi angalau uwatoe out hao watoto 3 wajisikie wana baba mdogo. Achana na huo ujinga. Yakimshinda arudi kwa baba yake!
 
Tatizo jingine ni wazazi , wao wanajua umempa mtaji mara tatu na hakuna cha maana alichofanyia. Badala ya kumkanya muhusika juu ya mwenendo wake mbaya wanaanza kumkingia kifua ili umsaidie tena kisa ndugu yako. Upuuzi wa hivi huwa sikubali. Mwisho wa siku namchanganya muhusika na hao wazazi wake ambao wanashindwa kumkanya mtoto wao
Unajua kuna mambo mengine huhitaji watu wakwambie kuwa umekuwa, kuna watu wanajikuta wanaishi na kufikiri kitoto na kujihisi bado hawajakua.

Ni ujinga tupu
 
Riba haina ulazima sana kwanza ni kuweka mpango mkakati wa muda mrefu kama ndugu kuona kama huo ni utamaduni kunyanyuana siyo kitu cha ajabu saana "kwamba asibaki mtu nyuma" kwa kushindwa kuinuliwa.

Mfano wewe umefanikiwa pengine labda ni biashara ya spare unamchukua ndugu mmoja unamuweka ofsin unampa chakula,maradhi na mavazi humlipi mshahara.

Unafanya naye biashara kwa kipindi cha miaka minne itategemea na ushapu wake ukiona ameiva unamfungulia duka lake spare na yeye anaenda na mfumo huo kwa anayemfuata ukishakuwa ni utamaduni inakuwa ni kitu cha kawaida ndipo neno la kuna familia zimebarikiwa linakuja.
Kwa muda mrefu nimewaona wenzetu Wachagga wakifanya hivi, sisi makabila mengine sijui tunakwama wapi. Yaani ile commitment ndiyo hakuna
 
Wewe ni tatizo pia, tena kubwa tu.

Kama una pesa zinakusumbua basi angalau uwatoe out hao watoto 3 wajisikie wana baba mdogo. Achana na huo ujinga. Yakimshinda arudi kwa baba yake!
Hilo Mkuu nimelitafakali, huenda ndiyo tatizo lilipo all in all ushauri wako nitaufanyia kazi.
 
Tatizo ni wewe unayempa ndugu mtaji mara tatu anauunguza alafu unalalamika, tena ukijua kabisa hana nidhamu ya pesa. Kwa hiyo akitoa rejesho ndo hatokula mtaji?
Nilidhani kwa kufanya hivyo itamsaidia kujihisi kuwajibika.

Since ni mtu mzima natumai atajifunza this time ikiwa vinginevyo ni juu yake
 
Uliyoyasema ni sahihi sana Mkuu, tatizo kubwa nililoliona ni kutokuwa na nidhamu ya hela. Kama ulivyosema, shida kubwa aliyonayo akipata hela ni Ulevi pamoja na Uzinzi.

Binafsi nimefikia hatua naumia kwa kuwa wakati mwingine ili kumpa mtaji naingia benki na kukopa kwa ajili yake.
Pole sana na hongera kwa kuwa na roho ya kiungwana mkuu ila naona ungemshauri hilo analofanya ambalo halileti tija kwake aliache ahamie katika industry nyingine
 
Naogopa kusema kuwa kama siyo wewe ni wakufaa kulaumiwa kwenye mkwamo wake basi wewe haukuwa msaada sahihi wa tatizo lake .

Nikama natamani kukuuliza maswali matatu madogo yahusuyo chanzo cha mafanikio yako na weredi wa uliyemsaidia :-

1.
(a) Mafanikio yako yametokana na (ELIMU) bila kujali ukubwa wa mshahara wako (ninachotaka kusema hapa nikuwa ,wenda uwelimu yako imekusaidia kujitambua na kukuongezea umakini .

(b) Au ulifanikiwa tu kwa kudra za Mwenyezi Mungu plus ujanja ujanja?

2.
(a) Msaidiwa anakiwango gani cha elimu ,anaujuzi wowote?

(b) Ulimsaidia kwa kumuwekezea kwenye kile alicho na ujuzi nacho , wewe ndiye uliyempangia chakufanya au ulimsaidia fedha kisha yeye asonge zake tu kwa kudra za Mungu?

3.
(a) Baada ya kumsaidia fedha /mali ulimsaidia ,pia kumpa usimamizi wa karibu juu ya kumfanikishia kuzifikia ndoto zake ? Au ulimpa ili tu uondoe lawama kwa family ?

Sitaki kusema watu wengi hasa tunaojiita watoa msaada wa family zetu ndiyo haswa huwa vyanzo vikuu vya kudumaza ndoto na ustawi wa family zetu .

Wengi wetu hasa waafrika tunahulka za UBINAFSI ,wengi huwa tunataka kuonekana miungu watu kwenye family zetu kutokana na aidha vyeo au mali tulizonazo na hata pale tunapotakiwa au tunapowasaidia wengine huwa tunafanya hivyo lakini siyo kwa dhamira zetu za ndani ,lengo kubwa ni washindwe ili tujidhihirishe kwao na kwakuokoo kuwa Mafanikio siyo lelemama

NAOGOPA KUHITIMISHA KWA KUSEMA MTOA MADA HUWA HAITOI MISAADA YAKE KWA LENGO LA DHATI LA KUMSAIDIA MWWNAFAMILY WAKE AFANIKIWE BALI NI KWA LENGO LA KUTAKA KUJIONDOA KWENYE KUNDI LA LAWAMA .

Binafsi ninamfano wangu kwa mdogo wangu wa kike aliyekuwa ameishia form four wakati ule , na kupachikwa mimba ,kwababhati mbaya aliyempa mimba alipoteza mvuto nae ndani ya muda mfupi Baada ya kujifungia na akahamishia mahaba kwa mschana mwingine ,kwetu halikuwa kosa , tatizo lilianzia pale mdogo wetu alipoomba apewe mtaji , sisi tukamwambia kwa sasa hana sifa ya kupewa mtaji hadi hapo atakapotimiza vigezo , na kigezo No 1 akubali kuendelea na shule au arudi nyumbani na kukaa miaka miwili ili achunguzwe ili tuone kama atakuwa na sifa zitakazomfanya apewe msaada .

Alikubali kurudi shule na kuendelea na form five na six na hata chuo .

Wakati yupo chuo alichagua kuwa mtabibu ,hii ilimfanya boom lake la kwanza aliwekeze kwenye duka la madawa baridi na Baada ya muda kidogo akatushawishi tumuongezee nguvu kwenye biashara yake hiyo ,Baada ya maswali mawili matatu tulijiridhisha nakumsaidia kutimiza hitaji lake huku tukimsaidia kumpa mbinu kadhaa za kiushindani zikiwemo kuweka record za wagonjwa anaowahudumia ,anuani za wanakotoka pamoja na history za magonjwa yanayowasumbua .

Pia tulimsaidia gari ndogo ili awe anawatembelea kwenye makazi yao walau maramoja kwa wiki sambamba na kuwapelekea walau dawa za kupunguza maumivu na juice za na maji madogo sambamba na kuwapa ushauri wa kitaalamu uhusuyo matatizo yanayowahusu .

Hii ilimjengea jina sana kiasi cha kuongeza idadi ya wateja (wagonjwa) hivyo kulazimika kuongeza eneo la kuwapokea sambamba na kuandaa eneo la kuwapumzisha kwa muda wale ambao wanakuna wakiwa hawako kwenye hali ya kuweza kukaa na sasa anamiliki hospital Arusha na hajawahi kuhangaikia ajira tena serikalini na tatizo lake KIUCHUMI nikama limekwisha kusovika kwa zaidi ya 85% .

Mtoa mada wenda ukawa na chakujifunza , samahanini kwa maelezo MAREFU
Kuna ndugu wengine ukimpiga tafu mtaji anaenda fanyia starehe pombe..au mwingine ananunua furniture zA gharama anashop mlimani city hata mchele au maharage ananunua mlimani city ..hawa tunawaweka kundi lipi?
 
Pole sana na hongera kwa kuwa na roho ya kiungwana mkuu ila naona ungemshauri hilo analofanya ambalo halileti tija kwake aliache ahamie katika industry nyingine
Nimefanya hivyo Mkuu, akipuuza atakuja kujuta mbele ya safari.

Yaani mtu mzima anataka aongozwe Kama school kid
 
wacha niwashirikishe jambo nililo learn kwa wahindi since niliwahi kufanya kazi na muhindi just as a friend sababu kuna kitu nilikua nafahamu kuhusu business anayoanzisha akaomba nimhelp for two month atanilipa fresh kwa hiyo nilipata kumuuliza na kuongea nae mambo mengi ambayo nikaja kujua why wahindi akifanikiwa mmoja ni lazima familia nzima ifanikiwe hata kama hawatakua matajiri sana wote but wote watakua financially stable.

Wahindi huwa wanaitana as family (familia zao huwa ni kubwa sana cas zina include mpaka aunt, uncle, wake walioolewa kwenye hiyo familia, waume nk)

1- walio stable financially wanamake sure wanaanzisha family business, hii inakua ni ya whole family yani wale ambao hawana pesa ndo watakao make sure business inarun na inafanikiwa na kuzaa matunda,.means wale wasio na uwezo ndio watakua wafanyakazi na wataishi kwa salary. So every month kila mwanafamilia anapata gawio la faida kama mshahara (NOTE: Only waliotoa pesa na wanaofanya kazi) so hiyo biashara huwa msimamizi mkuu anakua father house na kama ni mzee basi mtoto wa kwanza anakua msimamizi mkuu.

2- after biashara ikikua na kuwa stable kabisa let say imeshakua kampuni kubwa inaingiza millions, basi wote tena meeting ya familia wanakaa, every person ambae anawazo jipya la business na wale waliomaliza kusomeshwa wanaleta proposal zao za business, then zile proposal zitakazokubalika, WANAKOPESHWA PESA na familia. nimeandika kwa herufi kubwa hilo nano sababu wako very serious na mikopo yao, hata kama wewe ni mtoto ndani kabisa ya familia hupewi bure unakopeshwa kiasi chochote unachotaka,then unaenda kuanzisha unachotaka kuanzisha BUT Familia pia inakusimamia kwa karibu na kukusupport kwa kila hali hadi ufanikiwe ili uanze kurejesha mkopo (bila riba), ukishindwa kurejesha mkopo basi hautakua na thamani tena kwenye familia na hakuna mwanafamilia atakupenda, ila hufanya kila jambo ufanikiwe.

3-biashara au kampuni ikishakua stable inaingizwa kwenye asset za familia so inakua ni family business japo wewe ndo msimamizi mkuu na mwenye mamlaka zaidi kwenye hiyo business, thats why wenzetu wana GROUP OF COMPANIES NYINGI KWA MTINDO HUO, zote ni bhakresa au PATEL but ni family business as walioanzisha some of them ni watoto au wake au ndugu wa familia.

Tunahaja ya kuiga huu mfumo sababu nimeona hata comment zetu humu watz ni za kuona ndugu hasaidiki, but usiishie kutoa mtaji tu, simamia hadi uhakikishe amekaa sawa, ukiona anaelekea kuanguka take position fanya biashara iwe ya familia sio yake japo anashiriki. Hiyo itawainua as family na sio mmoja mmoja. Tujitahidi watz tubadirike na tuanze kua na family business.

Wewe baba au mama ubabiashara yako, make sure watoto wanajua vizuri biashara hio, wafanye part of business yako, walete waje wafanye kazi waongeze nguvu kwenye hiyo business, hata kama una duka moja fungua na lingine na lingine wape wafanye, sio mzazi una business kibao na mwanao amesomea business au finance au any related na kampuni yako then unamuacha akatafte kazi kwa mtu mwingine alipwe salary na kumpa faida mwingine na wewe una hire mtu mwingine unamlipa salary wakati mtoto wako abgeweza kuifanya na kusave costs ili kuongeza faida.

NAWASIHI TUANZE KUA NA FAMILY BUSINESS, WEWE MWENYE UWEZO UNAWEZA KUWAINUA WENGINE PIA, USIWAPE MITAJI BALI WASHIRIKISHE MFANYE KITU KWA PAMOJA KULETA TIJA NA MAENDELEO THEN WEWE TOA MTAJI NA WAFANYE KUA SEHEMU YA BUSINESS AS FAMILY NA WASIJIONE WALA USIWAONE VIBARUA BALI WALIRIKI WENZA HATA KAMA MTAJI UMETOA WEWE, MKIFANIKIWA WATAANZISHA NA ZINGINE HADI MNAJIKUA MMEKUA MILLIONARES AS FAMILY.
 
Kuna ndugu wengine ukimpiga tafu mtaji anaenda fanyia starehe pombe..au mwingine ananunua furniture zA gharama anashop mlimani city hata mchele au maharage ananunua mlimani city ..hawa tunawaweka kundi lipi?
Yaani hela ya mtaji anakwenda kuilia Bata, utasema wewe uliyempa unachota mahali
 
Nimefanya hivyo Mkuu, akipuuza atakuja kujuta mbele ya safari.

Yaani mtu mzima anataka aongozwe Kama school kid
Yah kuna watu wana bahati ya kubebwa mie pia ndugu yangu ananipiga tough sana! But najitahidi nisim dissapoint kabisa.
 
Yah kuna watu wana bahati ya kubebwa mie pia ndugu yangu ananipiga tough sana! But najitahidi nisim dissapoint kabisa.
Haileti picha nzuri kupewa mtaji then uutumie ndivyo sivyo, tena unakuta anayekupa hata amekopa benki.

So ukibeba make sure unabebeka, lengo ni kupunguza umasikini level ya familia
 
Back
Top Bottom