Dhana ya Kuinuana Kiuchumi baina ya Wanafamilia; Kuna haja unapompa ndugu yako Mtaji wa biashara umtoze riba ili kuongeza uwajibikaji?

Grahams

JF-Expert Member
Mar 19, 2016
11,014
33,913
Binafsi naamini kwenye familia, mmoja anaweza kuinuliwa ili aweze kuwainua wengine. Ndiyo maana kwenye maandiko Kitabu cha Mwanzo 42:25-28 unaona Yusufu alivyoinuliwa ili kuwasaidia ndugu zake. Kuna mtu anaweza kujiuliza kwani ni lazima kuwasaidia ndugu zako, Jibu sio lazima (Sijui kama kuna sheria inayolazimisha ndugu kusaidiwa hata Baba/Mama sio lazima) kuwasaidia lakini unajiuliza ni faida kiasi gani unapata kuona ndugu zako wakihangaika mitaani bila mafanikio wakati wewe ukiwa na nafuu?

Binafsi nimejaribu mara kadhaa kuwainua ndugu zangu (Tumbo moja) bila mafanikio mwisho wa siku najikuta napoteza mitaji tu. Natolea mfano, mwaka fulani nilimpa brother angu mtaji wa kumwezesha afanye biashara fulani iliyonigharimu kiasi. Bahati mbaya biashara akaiua/akala mtaji. Next time, nikampa mtaji mdogo wangu afanye biashara fulani aliyoitaka. Bahati mbaya naye akapoteza mtaji bila kufanikiwa. Simu za brother zikawa nyingi kuomba assistance huku akinishtakia kwa Wazee. Baada ya mivutano kidogo nikampa mtaji mwingine. Shida inakuja kwenye suala la kuikuza biashara na kuiendeleza, brother anafail, Kwahiyo baada ya muda mtaji huu pia ukafa.

Sasa nimempa mtaji wa mwisho wa biashara, akipoteza na huu Potelea mbali. Sitajali lawama za Walimwengu, hata Mungu anaona nilivyojitolea.

Swali, Je, kuna haja ya tunapowapa mitaji ndugu zetu(tuandikishiane) na tuanze kutoza riba ili kuongeza uwajibikaji (accountability)?? Jambo hili litakuwa na athari zozote kwa ustawi na mahusiano ya familia?
 
Urafiki na ndugu/wazazi kwenye masuala ya kiuchumi ni ngumu sana.

Ila kama ukipata nafasi ya kumsaidia..unamsaidia.

Ukiona anajitambua + ana nia + anaiheshimu hela(Financial discipline) sabbu kuna wengine wakizipate ndo uzinzi + kulewa mwanzo mwisho.

Fanya mpango umfungulie hata mtaji wa kutosha kabisa na yeye apambane...usichukue riba yoyote kwa sabbu atasema haoni faida kwa sabbu yako.

Then akianguka(kwa sabbu biashara/mradi wowote ni kama kubeti) muongezee tena mtaji.UMUINUE

baada ya hapo nawa mikono endelea kufanya yako...Hapo hata Mungu + wa Mataifa watakuwa wamejionea kwa macho yao wenyewe.
 
Katika swala la kupeana mtaji na ndugu ni bora umpe mtaji unaoona hautakuathiri hata kidogo kiuchumi endapo utapoteza, yani ni bora kurisk kiasi ambacho uko tayari kukipoteza bila kuathiri hali yako ya kiuchumi kabisaa

Maana akiupoteza mtaji au akiula kumtia mikononi mwa sheria ni ngumu sababu damu ni nzito kuliko maji na pia swala la pili ni wanafamilia hawatakubali umuweke ndani kwa mikono miwili hata kama amezingua mno

Kikubwa ukitaka kufanya biashara fanya na watu unaoweza kuwamudu mkuu, kumsaidia ndugu sio vibaya ila waswahili walisema "WEMA USIZIDI UWEZO"
 
Urafiki na ndugu/wazazi kwenye masuala ya kiuchumi ni ngumu sana.

Ila kama ukipata nafasi ya kumsaidia..unamsaidia.

Ukiona anajitambua + ana nia + anaiheshimu hela(Financial discipline) sabbu kuna wengine wakizipate ndo uzinzi + kulewa mwanzo mwisho.

Fanya mpango umfungulie hata mtaji wa kutosha kabisa na yeye apambane...usichukue riba yoyote kwa sabbu atasema haoni faida kwa sabbu yako.

Then akianguka(kwa sabbu biashara/mradi wowote ni kama kubeti) muongezee tena mtaji.UMUINUE

baada ya hapo nawa mikono endelea kufanya yako...Hapo hata Mungu + wa Mataifa watakuwa wamejionea kwa macho yao yenyewe.
Uliyoyasema ni sahihi sana Mkuu, tatizo kubwa nililoliona ni kutokuwa na nidhamu ya hela. Kama ulivyosema, shida kubwa aliyonayo akipata hela ni Ulevi pamoja na Uzinzi.

Binafsi nimefikia hatua naumia kwa kuwa wakati mwingine ili kumpa mtaji naingia benki na kukopa kwa ajili yake.
 
Mimi ninachoamini hatuwezi fanikiwa wote, hata kama mnatoka eote familia moja. Kuna watakaofanikiwa zaidi kuna watakao kwama.

Saidia pale unapoweza.

Lawama hazikosekani siku zote.

Manung'uniko lazima yawepo.

Muda mwingine mtu anapokwama haangalii changamoto zake anatafuta pakutupia lawama.
 
Katika swala la kupeana mtaji na ndugu ni bora umpe mtaji unaoona hautakuathiri hata kidogo kiuchumi endapo utapoteza, yani ni bora kurisk kiasi ambacho uko tayari kukipoteza bila kuathiri hali yako ya kiuchumi kabisaa

Maana akiupoteza mtaji au akiula kumtia mikononi mwa sheria ni ngumu sababu damu ni nzito kuliko maji na pia swala la pili ni wanafamilia hawatakubali umuweke ndani kwa mikono miwili hata kama amezingua mno

Kikubwa ukitaka kufanya biashara fanya na watu unaoweza kuwamudu mkuu, kumsaidia ndugu sio vibaya ila waswahili walisema "WEMA USIZIDI UWEZO"
Changamoto usipompa mtaji utakaomwezesha kufanya kazi na kujikimu italazimu kila tatizo unapigiwa simu wewe tu kusaidia, kwahiyo nilidhani unapowainua wawili, watatu inakupunguzia mzigo. Bahati mbaya wenzako hawa feel maumivu yako, kwani unajikuta umejinyima kuweza kumpa mtaji
 
Kiroho Riba ni mbaya kwa ndugu yako wa damu mkuu
Uko sahihi Mkuu, sasa kama mtu unampa mtaji 3 times anaua si manake unayeumia ni wewe uliyempa? Manake wakati mwingine inakulazimu uingie benki ukope ili kumpa mtaji ndugu yako
 
Nilijikusanya nikapata kama milioni 1 na laki 2.

Nimeamua kiroho safi kumpa kaka yangu Tshs laki 9 afanyie biashara.

Makubaliano ni baada ya muda tuje tugawane faida.

Baada ya miezi 6 naichukua + kafaida katakakopatikana, naenda kuoa

Sinaga hata muda wa kumuuliza anaizungushaje huko. Akipata loss, all is well its business.

ALINIINUA KIMASOMO NA MIMI NAMUINUA KIUCHUMI

Nimebakiza laki 1 tu hapa, 200k ilishatumika.
 
Uliyoyasema ni sahihi sana Mkuu, tatizo kubwa nililoliona ni kutokuwa na nidhamu ya hela. Kama ulivyosema, shida kubwa aliyonayo akipata hela ni Ulevi pamoja na Uzinzi.

Binafsi nimefikia hatua naumia kwa kuwa wakati mwingine ili kumpa mtaji naingia benki na kukopa kwa ajili yake.
Duuh isee pole sana Chief...inaonekana una moyo wa huruma sana.

Kiukweli mzazi ni mzazi tuu,ndivyo hivyo ndugu ni ndugu tuu.

Sasa huyo nahisi hajitambui..kiukweli kama angekuwa mdogo wangu ningemkata vibao vya kutosha..kwa sabbu ni changamoto sana kukaa na watu wasiojitambua. Na jinsi ninavyochukia mijitu mizinzi

Yaani mzee unakomaa balaa...alafu anakula kilaini laini tuu anajua flani yupo,hayo ni mazoea.

Cha kufanya hebu jaribu kumuita mzungumze mkiwa peke yenu...then mpe ushauri + maonyo makali na tahadhari juu.Baada ya hapo mpe tena mtaji kdg.

Akileta ubabaishaji tena waite wazee wenu mkae kama familia...uzungumze yote mliyoyazungumza kipindi mkiwa peke yenu pia weka na gharama zilizokucost baada ya hapo mpe tena mtaji then chapa mguu mbele.


Yatakayomkuta huko yamkute..ila wazazi + Mungu watakuwa mashahidi
 
Nilijikusanya nikapata kama milioni 1 na laki 2.

Nimeamua kiroho safi kumpa kaka yangu Tshs laki 9 afanyie biashara.

Makubaliano ni baada ya muda tuje tugawane faida.

Baada ya miezi 6 naichukua + kafaida katakakopatikana, naenda kuoa

Sinaga hata muda wa kumuuliza anaizungushaje huko. Akipata loss, all is well its business

Nimebakiza laki 1 tu hapa, 200k ilishatumika.
Hongera Mkuu, namwombea huyo ndugu yako afanikiwe

Mimi nimejaribu hivyo nimeambulia kupoteza mitaji
 
Hongera Mkuu, namwombea huyo ndugu yako afanikiwe

Mimi nimejaribu hivyo nimeambulia kupoteza mitaji
Asante mkuu.
Ndugu yangu alinipambania toka nikiwa form 1 mpaka nafika chuo kikuu yuko na mimi. Tena akiwa anafanya kazi ya 120,000 per month. Ndio mana hata sina muda wa kumfuatilia sana. Hanywi pombe wala kuwa marafiki wa hovyo
 
Back
Top Bottom