Dhana ya kuajiri Walimu wengi wa Sayansi ili kujenga viwanda

Status
Not open for further replies.

Apollo one spaceship

JF-Expert Member
Jan 28, 2021
242
431
Binafsi nadhani hii dhana ipo Afrika peke yake.
Sidhani kama mataifa ya Magharibi yalitumia hii dhana ili kukuza viwanda vyao,walianza kwa utafiti na ubunifu na sio kukaririshwa masomo darasani.

Cha ajabu hawa walimu wa Sayansi;
*Wakiona mwanafunzi anawadadisi au kuwauliza maswali mengi,atakiona cha mtema kuni
*Wakiona mwanafunzi anashindwa kuelewa wanachoeleza darasani,watamshauri ameze au akariri kitu kama kilivyo
*Hawaijui Sayansi kiundani,wengi wanachojua Ni kupata concept ya mada husika kwa juujuu na Kisha wanameza calculation zinavofanyika.
*Wanaiba mitihani kufaulisha wanafunzi.Hii inaonesha wana udhaifu kwenye kufundisha.
*Wanaamini elimu Ni mateso,wanashauri wanafunzi wasome kwa kukesha usiku darasani ili kufaulu mitihani
*Wanasifia madivisheni one kuliko ujuzi wa kiuvumbuzi wa mwanafinzi

Ishu ya viwanda Ni kaz kubwa na inahtaj uwekezaji
 
Sayansi ni mtoto wa sanaa.

Bila sanaa, sayansi haiwezi kuendelea. Hapo ndipo tunaposhindwa na mataifa au jamii zilizoendelea kisayansi.

Huwezi kufundisha au kuielewa vizuri sayansi kwa sababu sayansi ni outcome ya sanaa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom