Dhana na Miongozo ya "Katika Utawala Wangu..."

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Guys... Who is legal advisor wa Rais Magufuli? Au advisor wa namna yeyote ile?

Hii ziara ya Pwani yametokea matamko ya Rais ya kusema "katika utawala wangu" but kwangu naona hakuna jitihada kuweka mfumo, kanuni Na Sheria Imara zinazoeleweka ili uwajibikaji uwe ni kitu Na tunu ya kawaida si mfumo w utegemezi wa kiongozi mkuu wa nchi au hamasa yake kuongoza Na "kunyoosha" Taifa!

JPM alipokujaa alishangaa kukuta madudu na machafu kupindukia, sababu yawezekana sana kuwa JK naye alisema "katika utawala wangu" akajifanyia mambo Na maamuzi mengi ambayo Magufuli anayashangaa. Labda naye Kikwete alikuta aliyoyarithi ambayo yalifanywa kwa mantiki ya "katika utawala wangu.." iwe ni Serikalini au hata katika Chama.

Leo Magufuli anaongoza nchi Na kufanya kila kitu kwa kigezo cha "katika utawala wangu" Keaho akiondoka Magufuli, atakayekuja naye atasema "katika utawala wangu" na kubadilisha Yale yaliyofanya "katika utawala wangu" wa Magufuli !

Now nikiangalia kwa nini kuna non-responsive kutoka taasisi, mashirika, Serikali, watendaji Na hata wananchi, jibu lake ni kila mtu anajua "katika utawala wangu" utapita Na kuna expiry date Na si mfumo unaoeleweka kisheria... Wanapuuzia wanajua wakisema "ametukuta, ataondoka, atatuacha"!

Nchi imekuwa ikiendeshwa au kuongozwa na maamuzi kufanywa kwa dhana na fikra za "katika utawala wangu.." kuanzia Rais mpaka Mkuu wa Wilaya au hata mwenyekiti wa kijiji kupuuzia kabisa mipaka ya kisheria, mamlaka,kanuni hata katiba.

Zaidi, dhana hii ya "Katika utawala wangu.." si kwamba imekwamisha maendeleo ya jamii na Taifa, lakini hata imepunguza uwajibikaji wa kweli, kujenga kiburi nauungwana wa kukiri makosa, kujikosoa au kujisahihisha kunakosekana.

Mfano inawezekana DC wa Hai juzi akivunjavunja shamba la Mbowe alitumia kigezo hicho cha "katika utawala wangu.." au leo Mkuu wa TRA Arusha anaposema ukikutwa huna risiti fainielfu thelathini, naye anatumia nguvu ya "katika utawala wangu".

Keshoanapokuja mtendaji au kiongozi mwingine naye akasema "katika utawala wangu" (mfano mzuri ni Nape na Mwakyembe wizara ya habari) naye akaamua kusema anabadilisha na kufuta kila kilichofanywa na aliyemtangulia kwa kuwa "katika utawala wangu" haoni manufaa.

Kuna tofauti ya kufanya mambo "katika utawala wangu" kama mambo hayo hayahusu kanuni, sheria, taratibu, katiba au maamuzi yenye impact kubwa kwa jamii na Serikali.

Ni haki kusema "katika utawala wangu" uvivu,uzembe, ubabaishaji, uchelewaji, umangimeza, uhujumu nu mwiko na kamwe hautavumiliwa. Lakini kuna haja ya kuweka na kurejea misingi iliyopo na kuhoji kwa nini utovu wa nidhamu upo na au unaongezeka!

Leo Rais Magufuli kawasema Brela mpaka kutoa tamko (presidential executive order) verbally kuwa wenye nia ya kuanzisha viwanda au biashara wasisubiri Brela, waanze mchakato maana Brela wanajivutavuta na kupunguza kasi ya maendeleo na azma ya viwanda ya awamu ya tano. Najiuliza je kwa nini Brela leo ni miezi 20 tangu awamu ya Tano iingie madarakani bado inajivutavuta na kuwa na umangimeza au ukiritimba ambao unakwamisha ufanisi? je hawana kanuni za uwajibikaji? au usimamizi wa kanuni za uwajibikaji na majukumu zina mapengo na mianya ya uzembe, uhujumu au hata kulea rushwa na kero?

Je yawezekana huko Brela hakuna hizi kanuni kwa kuwa kila mkubwa wa sehemu anafanya mambo ya "katika utawala wangu" na kujiamulia mambo na wafanyakazi wa chini kwa kukosa mfumo unaoeleweka na kushuhudia kwao wakubwa wakifanya mambo kwa itikadi ya "katika utawala wangu" basi wanajijengea kiburi cha "alitukuta, atapita, atatuacha hapahapa"?

May be tukiongelea mambo kwa mtazamo huu, ubishi na ushabiki unaopinga kujengwa kwa mfumo huru Imara kuanzia Katiba, Sheria na Kanuni hata uwajibikaji wake utaangalia mambo kiuhalisia Na si kushangilia current happenings ambazo "baada ya utawala wangu" tutarudi kule kule au atakuja mwingine na mtazamo wake na kusema "katika utawala wangu"?
 
Nakumbuka ziara ya Rais aliepita wa Us alipokuja Africa sina uhakika wapi nafikiri alipohutubia AU Addis Ababa alisema Africa iondoke ktk dhana ya watu kuwa mashujaa na hasa kipindi cha kumtoa mkoloni mashujaa wetu kama Nyerere,Nkwame N.k wengi walipatikana kipindi hicho kwa sasa Africa inahitaji taasisi imara

Itakuwa kila mtawala anakuja na maelekezo yake kutokana na utashi wake na wala hatujishughulishi kuweka mifumo imara ya kitaasisi na hii itasaidia na haitajalisha nani anakalia ofisi kuu anakuta mifumo ya kitaasisi ipo madhubuti
 
Nchi imemshinda kuongoza, aliowateua nao wanafata upepo unakovuma hawana malengo,mipango imefika ugoto, kila kiongozi aliyepewa kusimamia majukumu katika halmashauri na kurungenzi mbalimbali ni kulialia tu hata wananchi wamebaki watazamaji mana kila siku zinavyoenda afadhali ya jana.."Katika utawala wangu" ni kauli ya uoga na kutojiamini.
 
Shida inaanzia kwenye fikra kwamba unapochaguliwa kuongoza nchi unakuwa juu ya katiba na utawala wa sheria.
Uko sahihi, lakini kuna tatizo jingine-wakati wa JK watu walikuwa wanasema nchi ilipigwa ganzi mambo yakawa yanafanyika shaghalabaghala, lakini awamu hii pia naona kama imepigwa ganzi watu wanashangilia kila linalofanywa bila kujali athari zake kwa taifa!
 
Guys... Who is legal advisor wa Rais Magufuli? Au advisor wa namna yeyote ile?

Hii ziara ya Pwani yametokea matamko ya Rais ya kusema "katika utawala wangu" but kwangu naona hakuna jitihada kuweka mfumo, kanuni Na Sheria Imara zinazoeleweka ili uwajibikaji uwe ni kitu Na tunu ya kawaida si mfumo w utegemezi wa kiongozi mkuu wa nchi au hamasa yake kuongoza Na "kunyoosha" Taifa!

JPM alipokujaa alishangaa kukuta madudu na machafu kupindukia, sababu yawezekana sana kuwa JK naye alisema "katika utawala wangu" akajifanyia mambo Na maamuzi mengi ambayo Magufuli anayashangaa. Labda naye Kikwete alikuta aliyoyarithi ambayo yalifanywa kwa mantiki ya "katika utawala wangu.." iwe ni Serikalini au hata katika Chama.

Leo Magufuli anaongoza nchi Na kufanya kila kitu kwa kigezo cha "katika utawala wangu" Keaho akiondoka Magufuli, atakayekuja naye atasema "katika utawala wangu" na kubadilisha Yale yaliyofanya "katika utawala wangu" wa Magufuli !

Now nikiangalia kwa nini kuna non-responsive kutoka taasisi, mashirika, Serikali, watendaji Na hata wananchi, jibu lake ni kila mtu anajua "katika utawala wangu" utapita Na kuna expiry date Na si mfumo unaoeleweka kisheria... Wanapuuzia wanajua wakisema "ametukuta, ataondoka, atatuacha"!

Nchi imekuwa ikiendeshwa au kuongozwa na maamuzi kufanywa kwa dhana na fikra za "katika utawala wangu.." kuanzia Rais mpaka Mkuu wa Wilaya au hata mwenyekiti wa kijiji kupuuzia kabisa mipaka ya kisheria, mamlaka,kanuni hata katiba.

Zaidi, dhana hii ya "Katika utawala wangu.." si kwamba imekwamisha maendeleo ya jamii na Taifa, lakini hata imepunguza uwajibikaji wa kweli, kujenga kiburi nauungwana wa kukiri makosa, kujikosoa au kujisahihisha kunakosekana.

Mfano inawezekana DC wa Hai juzi akivunjavunja shamba la Mbowe alitumia kigezo hicho cha "katika utawala wangu.." au leo Mkuu wa TRA Arusha anaposema ukikutwa huna risiti fainielfu thelathini, naye anatumia nguvu ya "katika utawala wangu".

Keshoanapokuja mtendaji au kiongozi mwingine naye akasema "katika utawala wangu" (mfano mzuri ni Nape na Mwakyembe wizara ya habari) naye akaamua kusema anabadilisha na kufuta kila kilichofanywa na aliyemtangulia kwa kuwa "katika utawala wangu" haoni manufaa.

Kuna tofauti ya kufanya mambo "katika utawala wangu" kama mambo hayo hayahusu kanuni, sheria, taratibu, katiba au maamuzi yenye impact kubwa kwa jamii na Serikali.

Ni haki kusema "katika utawala wangu" uvivu,uzembe, ubabaishaji, uchelewaji, umangimeza, uhujumu nu mwiko na kamwe hautavumiliwa. Lakini kuna haja ya kuweka na kurejea misingi iliyopo na kuhoji kwa nini utovu wa nidhamu upo na au unaongezeka!

Leo Rais Magufuli kawasema Brela mpaka kutoa tamko (presidential executive order) verbally kuwa wenye nia ya kuanzisha viwanda au biashara wasisubiri Brela, waanze mchakato maana Brela wanajivutavuta na kupunguza kasi ya maendeleo na azma ya viwanda ya awamu ya tano. Najiuliza je kwa nini Brela leo ni miezi 20 tangu awamu ya Tano iingie madarakani bado inajivutavuta na kuwa na umangimeza au ukiritimba ambao unakwamisha ufanisi? je hawana kanuni za uwajibikaji? au usimamizi wa kanuni za uwajibikaji na majukumu zina mapengo na mianya ya uzembe, uhujumu au hata kulea rushwa na kero?

Je yawezekana huko Brela hakuna hizi kanuni kwa kuwa kila mkubwa wa sehemu anafanya mambo ya "katika utawala wangu" na kujiamulia mambo na wafanyakazi wa chini kwa kukosa mfumo unaoeleweka na kushuhudia kwao wakubwa wakifanya mambo kwa itikadi ya "katika utawala wangu" basi wanajijengea kiburi cha "alitukuta, atapita, atatuacha hapahapa"?

May be tukiongelea mambo kwa mtazamo huu, ubishi na ushabiki unaopinga kujengwa kwa mfumo huru Imara kuanzia Katiba, Sheria na Kanuni hata uwajibikaji wake utaangalia mambo kiuhalisia Na si kushangilia current happenings ambazo "baada ya utawala wangu" tutarudi kule kule au atakuja mwingine na mtazamo wake na kusema "katika utawala wangu"?
Hivi USA wakati wa Obama Na wakati wa Trump kuna kufanana??
Au wakati wa Bush junior kulinganisha Na wakati wa Bill Clinton .
Au waweza Kulinganisha kipindi Cha Reagan vs kipindi Cha Jimmy Carter.
Kitu kikubwa ninacho kiona kila kiongozi mosi huja ni vipaumbele vyake Na pili huja kurekebisha pale waliotangulia walitereza either Kwa bahati mbaya au Kwa mapungufu yao.
Na tatizo la Tz Kwa zaidi ya 20 years tume kuwa hatuna Tunakwenda kwenye muelekeo wa maendeleo chini ya kiwango hivyo tunatakiwa tu pige hatua nne mahali ambapo kikawaida tungepiga hatua moja au mbili. Hivyo Kwa sasa hivi tunatakiwa tufanye vitu above standard.
Na Kama wewe ni Rev Kama unavyojiita basi utakuwa unajua historia ya italia Na in particular Muscolini alivyoweza kuibadili Italia. Mahal I palipokuwa na matete watu waliweza kujenga makazi n.k .
Tumechelewa , muunge mkono Raisi wako hata kama humpendi lakini nafikiri unaipenda tz , tukisha rudi kwenye mstari ndio tuta enjoy hiyo mifumo Na sheria nk.
 
Hivi USA wakati wa Obama Na wakati wa Trump kuna kufanana??
Au wakati wa Bush junior kulinganisha Na wakati wa Bill Clinton .
Au waweza Kulinganisha kipindi Cha Reagan vs kipindi Cha Jimmy Carter.
Kitu kikubwa ninacho kiona kila kiongozi mosi huja ni vipaumbele vyake Na pili huja kurekebisha pale waliotangulia walitereza either Kwa bahati mbaya au Kwa mapungufu yao.
Na tatizo la Tz Kwa zaidi ya 20 years tume kuwa hatuna Tunakwenda kwenye muelekeo wa maendeleo chini ya kiwango hivyo tunatakiwa tu pige hatua nne mahali ambapo kikawaida tungepiga hatua moja au mbili. Hivyo Kwa sasa hivi tunatakiwa tufanye vitu above standard.
Na Kama wewe ni Rev Kama unavyojiita basi utakuwa unajua historia ya italia Na in particular Muscolini alivyoweza kuibadili Italia. Mahal I palipokuwa na matete watu waliweza kujenga makazi n.k .
Tumechelewa , muunge mkono Raisi wako hata kama humpendi lakini nafikiri unaipenda tz , tukisha rudi kwenye mstari ndio tuta enjoy hiyo mifumo Na sheria nk.
umezungumzia Marekani yenye mifumo huru ya mizania ya uongozi: Executive, Legislative na Judicialambazo zote zina checks and balances zenye nguvu kuzuia uimla wa mambo.

Kiongozi kuja na kipaumbele si tatizo, tatizo nikuongoza nchi bila mfumo eleweka na wenye mianya mingi ya uholela.

Turudi kwenye mfano wako wa Marekani: ni wapi umesikia Rais wake akiamua matumizi ya fedha, kubadilisha kodi au hata kuingia vitani bila kuhusisha bunge na kupigiwa kura na bunge? je lini umesikia Rais akiingilia utendaji wa idara za Serikali kisa yeye Rais bila kuleta mtafaruku?

Hayo ya kuanza kubezana kama ni Rev. wa kweli au wa uongo ni udhaifu wa kujenga hoja kujibu hoja August..
 
Hivi USA wakati wa Obama Na wakati wa Trump kuna kufanana??
Au wakati wa Bush junior kulinganisha Na wakati wa Bill Clinton .
Au waweza Kulinganisha kipindi Cha Reagan vs kipindi Cha Jimmy Carter.
Kitu kikubwa ninacho kiona kila kiongozi mosi huja ni vipaumbele vyake Na pili huja kurekebisha pale waliotangulia walitereza either Kwa bahati mbaya au Kwa mapungufu yao.
Na tatizo la Tz Kwa zaidi ya 20 years tume kuwa hatuna Tunakwenda kwenye muelekeo wa maendeleo chini ya kiwango hivyo tunatakiwa tu pige hatua nne mahali ambapo kikawaida tungepiga hatua moja au mbili. Hivyo Kwa sasa hivi tunatakiwa tufanye vitu above standard.
Na Kama wewe ni Rev Kama unavyojiita basi utakuwa unajua historia ya italia Na in particular Muscolini alivyoweza kuibadili Italia. Mahal I palipokuwa na matete watu waliweza kujenga makazi n.k .
Tumechelewa , muunge mkono Raisi wako hata kama humpendi lakini nafikiri unaipenda tz , tukisha rudi kwenye mstari ndio tuta enjoy hiyo mifumo Na sheria nk.

Nahisi hukusoma hii:
Kuna tofauti ya kufanya mambo "katika utawala wangu" kama mambo hayo hayahusu kanuni, sheria, taratibu, katiba au maamuzi yenye impact kubwa kwa jamii na Serikali.

Ni haki kusema "katika utawala wangu" uvivu,uzembe, ubabaishaji, uchelewaji, umangimeza, uhujumu nu mwiko na kamwe hautavumiliwa. Lakini kuna haja ya kuweka na kurejea misingi iliyopo na kuhoji kwa nini utovu wa nidhamu upo na au unaongezeka!
 
Shida inaanzia kwenye fikra kwamba unapochaguliwa kuongoza nchi unakuwa juu ya katiba na utawala wa sheria.

Siyo hiyo tu,hata kufikiria kwamba ukiwa mtawala una akili nyingi zaidi kuliko mtawaliwa!Siku hao watawala wakija kung'amua kwamba watawaliwa wanaakili nyingi zaidi kuliko watawala ndipo tutakapopata SERIKALI yenye nguvu na uzalendo na hii ya "UTAWALA WANGU" itaondoka.
 
tatizo la afrika hakuna taasisi huru zaidi ya vitaasisi vya watu binafsi kama viongozi.

Viongozi wengi wa AFRIKA akili hamna kabisa ni watu wa kutumia nguvu zaidi.Wenzetu wanawatumia zaidi wanasheria kuwa marais na wanapiga hatu kubwa kuliko AFRIKA unatumi nguvu kubwa akili kisoda
 
Komredi rev kishoka

Huu mfumo umejikita mizizi ndani ya CCM ndio maana unaona hakuna continuation ya sera wala mipango ktk serikali ya CCM!

Kila rais wa CCM anayekuja huanza kana kwamba nchi ilikua upinzani
....
Mkuu lusungo,hiyo ni kweli kabisa. Kuna mzee wangu mmoja aliwahi niambia kuwa kama CCM ingekuwa na katiba nzuri,tungekuwa na CCM kama taasisi imara ambayo ingeleta viongozi makini. Na hili ni kwa vyama vyote.
Katiba imara & bora,
Taasisi imara,
Uongozi bora.
 
Siyo hiyo tu,hata kufikiria kwamba ukiwa mtawala una akili nyingi zaidi kuliko mtawaliwa!Siku aho watawala wakija kung'amua kwamba watawaliwa wanaakili nyingi zaidi kuliko watawala ndipo tutakapopata SERIKALI yenye nguvu na uzalendo na hii ya "UTAWALA WANGU" itaondoka.
Mkuu Tetty,uliyoyaandika ni kweli kabisa. Kuna viongozi mpaka wanafikia hatua ya kutamka kabisa kwamba wao wana akili zaidi ya wengine ndio maana wapo kwenye hizo nafasi walizonazo.
 
22 Reactions
Reply
Back
Top Bottom