DHAMIRA HURU: CCM wanaweza kulazimisha sheria; Hawawezi kulazimisha Katiba bila kupingwa!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Na. M. M. Mwanakijiji

Siasa ni sanaa na sayansi. Sehemu ya sanaa ni sehemu ya kumanipulate events, situations, and yes even people. Hakuna namna moja ya kufanya siasa. Keshokutwa wabunge wa CDM wanaweza kurudi Bungeni kama kawaida na kuendelea na majukumu yao kama kawaida. Kutoka kwao Bungeni ni sehemu ya siasa kama vile wale walioamua kutumia jukwaa la siasa kubeza na kukejeli wenzao. Its part of politics. CDM hawaitaji kususia Bungeni, walichosusia ni kuburuzwa na ni wajibu wa kila Mtanzania ambaye anaamini katika dhamira yake kuwa CCM inataka kuliburuza Taifa kwenye mjadala wa Katiba. Ushahidi upo - japo watu wameshasahau - nitawakumbusha siku moja kuwa mchakato mzima ulipangwa uwe hivi na ndivyo utakavyokuwa.

Ninaamini uamuzi wa CDM ni sahihi kwani dhamira ya mwanadamu haina shurti. Hakuna kitu kikuu kwa mwanadamu kama dhamira yake. Ukiondoa imani ya Mungu, mwanadamu anaiamini dhamira yake zaidi kwani ni chombo hicho cha kibinadamu ambacho kinamfanya akubali au akatae. Wakati mwingine katika kukataa ni pamoja na gharama yake. Wapo watu waliotukuza dhamira zao mpaka mauti.

Binafsi naunga mkono uamuzi wa CDM kupinga na ninaunga mkono wale wote ambao watasimama kukataa kushiriki, kujadili, kujihusisha na hata kutolea maoni katika mchakato utakaoandaliwa na CCM. Kwa vile CCM imeamua kuteka hoja nzima ya Katiba Mpya (sote tunajua haijawahi kuwa hoja, ajenda wala mipango yao) ni wazi kuwa matokeo yake yatakuwa kama vile ambavyo CCM inataka. CDM wala hakuna mtu mwingine yeyote anayeweza kuwazuia katika hili. Hata hivyo, wanaweza kulazimisha sheria, wanaweza kuagiza vyombo vya dola na wanaweza kabisa hata kusitisha maandamano yote nchini.

Kitu ambacho hawawezi ndugu zangu ni kulazimisha dhamira zetu. Ni dhamira zetu ambazo ziko huru na unyanyasaji, kusumbuliwa, kutishwa au kushurutishwa kwa namna yoyote ile. Ni dhamira zetu ambazo zinasimama milele huru huku miili imetiwa pingu, na zinabakia huru wakati kejeli na matusi yanaporomoshwa na hata vitisho. Assad wa Syria na Gaddafi kule Libya wote walijaribu kuzima dhamira za watu. Walikuwepo watu waliokataa tawala hizo na hakuna chochote ambacho kiliweza kugeuza au kulazimisha upendo. Leo hii Assad anazidi kutengwa tena katika hali ya kushangaza kabisa kutengwa na Waarabu wenzake! Waarabu wanaamini katika kitu kinachoitwa "Arab Nation" wakizungumzia na kumaanisha unity ya jamii ya watu wao. Na wakiunganishwa siyo tu na utamaduni na nasaba zao lakini zaidi wakiunganishwa na dini vile vile. Leo hii Syria inakataliwa na Saudia, inatakaliwa na Uturuki, inakataliwa na Jordan! Lakini Assad anafikiri silaha zitazima dhamira za wananchi wake.

Nimesikiliza na kufuatili kwa siku hizi mbili maneno ya wabunge wetu Bungeni jinsi ambavyo wanasimama wakiwa wamelewa kabisa madaraka kiasi cha kuamini kwa mioyo yao yote kuwa wao ndio Tanzania na sisi wengine wote ni watu tulio chini yao. Wengine wanazungumza in what I could only describe as an utter contempt of the people of Tanzania. Yaani, kuna wengine walikuwa wanazungumza kana kwamba kwa vile wako madarakani na ni watawala basi hakuna wa kuwahoji, kuwapinga, kuwakatalia na sasa wanataka hata vyombo vya dola vitumike kulazimisha dhamira za watu!

Wengine wanasema - na siwezi kushangaa hatua kali zaidi zikachukuliwa - watu wanaopinga mchakato huu wa CCM kuandika Katiba basi washughulikiwe na vyombo vya dola. Na sitoshangaa vitu kama Jukwaa la Katiba vikapigwa marufuku na baadhi ya watu wakaanza kunyanyaswa kwa sababu tu wamekataa kuingizwa kwenye mkokoteni usio na matairi wa huu unaoitwa mchakato wa Kuandika Katiba Mpya. Kwa kadiri nilivyowasikiliza nilitambua jambo moja kwa usahihi kabisa na kwa wazi katika akili zangu - wamelewa ugimbi wa madaraka kiasi kwamba hawakumbuki, hawajui, na hawataki kuamini kwani walikataliwa zaidi mwaka jana kwenye uchaguzi mkuu.

Walikataliwa mwaka jana kwa sababu walishindwa kulazimisha dhamira ziwakubali. Walitumia kila mbinu kulazimishwa kupendwa lakini mwisho wake walikuwa wametengeneza mapenzi ya hofu. NI sawa na mwanamama ambaye anajifanya anampenda mwanamme ambaye amemteka na kumbaka na kumzalisha watoto. Mwanamme yule akiona tabasamu anafikiri anapendwa, akiona mama amempikia chakula anaamini anapendwa. Hajui tu kiilele cha chuki kilichomo ndani ya mtu. Upendo wa hofu ni upendo wa kisasi.

NI upendo ambao mtu akipewa nafasi ya kufanya kitu kibaya atakifanya kibaya kuliko akili za mwanadamu zinavyoweza kudhania. Namkumbuka miaka hiyo (SIMULIZI LA KWELI) mwanamke mmoja ambaye baada ya kunyanyaswa sana na mume wake (ambaye aliamini anapendwa) alikesha usiku mmoja akiwa amefikia kikomo cha uvumilivu wake na dhamira yake ikimtia moyo na kumsubiri mumewe aliyekuwa amekwenda kilabuni. Mume aliporudi bwiii alianza vituko vyake na mwisho akalala sebuleni kwenye kochi. Kumbe mwanamke alikuwa anachemsha sufuria la mafuta ya kupikia. Jamaa akiwa amelala mdomo wake na harufu ya pombe mwanammke yule alikuja na kumiminia mafuta yale kama mtu anavyomimina mafuta kwenye galoni bila kutumia mrija! Jamaa hakupata hata nafasi ya kuuliza "why!". Mwanamke aliuchukua mwili na kuuweka kwenye gari na akarudi zake kulala!

CCM iangalie sana inavyolishughulikia suala hili la Katiba Mpya. Sasa hivi hawana hoja ya kutushawishi bali wana hoja ya kutalazimisha. Hawana hoja ya kwanini tuwasikilize wao bali wana hoja kwanini tusiwasikilize wapinzani. Wanatumia nguvu kubwa sana kulazimisha. Kwa wale tunaokumbuka tunakumbuka kuwa walifanya hivi kwenye Sheria ya Uchaguzi Mkuu na tukawatakalia hawakuamini lakini kilipokuja kuwauma wao wenyewe wakaanza kulalamika! Hawajajifunza. Wanaamini kabisa kuwa wao ni zawadi ya Mungu kwa Tanzania! Na ambao wamenitibua zaidi ni wale ambao walikuwa wanazungumza kana kwamba watu hawajui tunachogombania ni nini! Wanafikiria kuwa wao wamezama katika kuelewa kwa kina kila kilichomo kiasi kwamba mawazo yoyote yakitolewa na watu nje ya CCM basi yamekosewa prima facie. Yaani, hawajachukua hata muda wa kuangalia kutoka upande mwingine. Wameamua kuangalia kutoka upande wao tu na ni upande wao tu ndio uko sahihi.

Wamechagua upande mbaya wa historia. Hata hivyo, uzuri wa historia ni kuwa haina ubaguzi sote tumo kwenye historia hiyo hiyo na historia itaamua ni upande gani umechagua upande sahihi wa historia. Upande ambao unatumia dhulma, vitisho, madaraka, na hata kuwa tayari kutumia dola ili hoja zake zikubaliwe mara zote umeoneshwa na historia kuwa ni upande mbaya! Upande huo wapo kina Milosevic na Hitler, upande huo wapo kina Stalin na Mussolini! Upande ambao unashindwa kuheshimu dhamira za watu na uhuru wao kukataa ni upande mbaya na wa kukataliwa.

Ndugu zangu, hakuna shaka sheria hii itapitishwa na itasainiwa kwa mbwembwe - isipokuwa kama Kikwete ataamua kuja upande sahihi wa historia kwa kukataa - kama walivyofanya kwenye mswada wa Sheria ya Uchaguzi. Na ikipitishwa kama ilivyo na kusainiwa kuwa sheria ni wajibu wetu kwetu sisi wenyewe na dhamira zetu na ni wajibu wetu kwa ajili ya kizazi kijacho kukataa kabisa kushiriki mchakato huu, kuupinga, na hata ikibidi kuhamasisha watu kutoshiriki (hili linaweza kufanywa kuwa kosa!). Jamani hatuna cha kupoteza isipokuwa utu wetu na thamani ya kutambuliwa utu huo. Hatuna nguvu, fedha, madaraka na vyombo vya dola kuwalazimisha wakubali kuangalia upya, lakini tunazo dhamira na uhuru wetu.

Nimesema mara nyingi kuwa fikra huru hazifungwi pingu lakini niongeze leo kuwa dhamira hazifungwi minyororo kuvutwa! Walikuwepo watu ambao wameteswa na kunyanyaswa na kuambiwa wachague kusema uongo waachiliwe lakini walikataa kufanya hivyo kwa sababu hawakuwa tayari kuishi na kusaliti dhamiri zao. Naam, wapo watu ambao watatoka na kwenda upande mbaya wa historia lakini wale ambao tumeamua kukaa upande sahihi wa historia tusijali vitisho wala kejeli. Jana nimepata nafasi ya kuwatia moyo wanaharakati kadhaa - wasio wanasiasa - waliopo nchini na kuwaambia kuwa uamuzi wowote wa kupinga mchakato huu wa CCM utakuja na gharama kubwa kama tulivyoona Bungeni. Wataitwa majina, akili zao zitahojiwa na mashambulizi ya wazi dhidi yao yatafanywa na mashine za wale walioko madarakani. Lakini watakuwa na uchaguzi ama kuheshimu na kutii dhamira zao au kufuata mkumbo.

Ndugu zangu, mwanadamu anapoteza utu wake pale anapokataa kutii dhamira yake. Kama unaamini CCM inafanya jambo jema na kuwa inafanya haya kwa nia nzuri na kuwa sheria hii ni nzuri na ndicho tunachokihitaji basi una uchaguzi mmoja tu - kuunga mkono sheria hiyo, kujitokeza kwenye mchakato huu na kuwashawishi wengine kufanya hivyo ili waone makosa ya maamuzi yao. LAKINI!!... kama dhamira yako inakutuma na kukufanya uamini kuwa mchakato mzima umekosewa toka mwanzo na unalengo la kulazimisha vile ambavyo CCM inataka kwenye Katiba Mpya na ya kuwa hukubaliani na mtindo mzima unavyokwenda - uchaguzi wako nao ni mmoja tu. Kupinga, kukataa na kuamua kutokushikiri hadi pale ambapo mfumo mzuri, huru na wenye kuheshimu KANUNI YA KWANZA (Soma Tanzania Daima leo) ya kuandika Katiba Mpya.

Hakuna uamuzi wa katikati.
 
Well said Mwanakijiji, ni uchambuzi mzuri unao reflect uhalisia uliopo. Walichokifanya CDM ni sahihi kwa mantiki kwamba " A riot is the language of unheard" wao pia hwakusikilizwa na wameamua kufikisha ujumbe kwa namna walivyofanya maana ndio lugha iliyowastahili kuongea.

Lakini kama watanzania wazeleondo tusihofie wanachokifanya CCM and their allies maana hawawezi kuushindana na dhamira zetu za ndani kama ulivtokwisha kubainisha hapo juu. Dhamira ya mwanaharakati yoyote ni kuleta mabadili juu ya jambo fulani ambalo linaonekana kutokuwa sawa na anafanya hivyo kwa kuleta mabadiliko yeye mwenyewe au kwa kuweka misingi ya hayo mabadiliko kutokea au kuletwa na watakao fuata nyumba yake au baada ya yeye.

Tukumbuke kuwa CCM na nguvu ya dola walionayo kuwa wanaweza kuwapiga risasi wanaharakati, kuwafunga, kuwaweka kizuizini, kuchoma mali zao na vingingine vingi ila kamwe hawataweza kuchoma au kuzui mawazo/dhamira za kimapinduzi au uanaharakati miongongi mwa watu wenye dahmira ya dhati ya kulikomboa Taifa letu la Tanzania.
 
Namkumbuka miaka hiyo (SIMULIZI LA KWELI) mwanamme mmoja ambaye baada ya kunyanyaswa sana na mume wake (ambaye aliamini anapendwa) alikesha usiku mmoja akiwa amefikia kikomo cha uvumilivu wake na dhamira yake ikimtia moyo na kumsubiri mumewe aliyekuwa amekwenda kilabuni.

Ushoga umeanza zamani, au mfupa hauna ulimi?! ;)
 
Fikra chanya, hakika tutashinda jamani humu JF kuna alot of intellectuals ni wajibu kusimamia hili suala tuwaelekeze ndugu zetu jamii yote ya kitanzania upotoshaji wa chama tawala na serikali yake .wanachokifanya chama tawala kwa sasa ni kitendo cha kidharirishaji tena ni udharirishaji mkubwa wa hii inayoitwa demokrasia ni ukweli usiofichika kwa this government imefika saturation ...

ni wito kwa sisi wenye nia ya dhati na ukombozi wa nchi yetu kutumia furksa zetu kupinga huu UBABE wa hii serikali
WATAWALA TAMBUENI "For every action, there is an equal and opposite reaction."

KATIBA NI MALI YETU SISI WATANZANIA NA SIO TAASISI WALA CHAMA CHA SIASA KWANINI NYIE WATAWALA MTUENDESHE HIVYO.

THIS TIME LIWALO NA LIWE AGRRRRRRRH
 
Mzee Mwanakijiji: Inatia moyo, imenipa nguvu na tumaini la kuendelea kusimamia yale ninayoamini ni sahihi katika mchakato wa katiba.
 
CCM na CUF kwa kweli hawana jipya, nilimsikia mchangiaji wa CUF aliyehongwa helcopter wakati wa uchaguzi Igunga, jinsi alivyokuwa na mapenzi na CCM mwanzo hadi Mwisho ni kukashifu CDM tu.

Wabunge wote kwa sasa hivi hawajadili mapungufu ya mswada huo isipokuwa ni kuwashambulia Waheshimiwa wabunge wa CDM mwanzo hadi mwisho wanadhani wananchi watawasikiliza. Watanzania wa sasa hivi siyo wa enzi za Kidumu.
 
Na ambao wamenitibua zaidi ni wale ambao walikuwa wanazungumza kana kwamba watu hawajui tunachogombania ni nini! Wanafikiria kuwa wao wamezama katika kuelewa kwa kina kila kilichomo kiasi kwamba mawazo yoyote yakitolewa na watu nje ya CCM basi yamekosewa prima facie. Yaani, hawajachukua hata muda wa kuangalia kutoka upande mwingine. Wameamua kuangalia kutoka upande wao tu na ni upande wao tu ndio uko sahihi.

Kuhusiana na dhamira; je, yao hii ni moja ya dhamira zisizo huru?! Na ikifafanuliwa kama dhamira, je, katika mpambano kati ya dhamira huru na ile isiyo huru ni sharti iliyohuru ishinde?!
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Siasa ni sanaa na sayansi. Sehemu ya sanaa ni sehemu ya kumanipulate events, situations, and yes even people. Hakuna namna moja ya kufanya siasa. Keshokutwa wabunge wa CDM wanaweza kurudi Bungeni kama kawaida na kuendelea na majukumu yao kama kawaida. Kutoka kwao Bungeni ni sehemu ya siasa kama vile wale walioamua kutumia jukwaa la siasa kubeza na kukejeli wenzao. Its part of politics. CDM hawaitaji kususia Bungeni, walichosusia ni kuburuzwa na ni wajibu wa kila Mtanzania ambaye anaamini katika dhamira yake kuwa CCM inataka kuliburuza Taifa kwenye mjadala wa Katiba. Ushahidi upo - japo watu wameshasahau - nitawakumbusha siku moja kuwa mchakato mzima ulipangwa uwe hivi na ndivyo utakavyokuwa.
......... Hakuna uamuzi wa katikati.

Asante, Mzee Mwanakijiji kwa hili, ila mimi naomba kutofautiana na wewe, na msimamo wa Chadema.

Wakati wa kutangaza matokeo ya urais, mimi binafsi nilikuwepo pale ukumbini, Chadema walisusa, nilitofautiana nao na nikasema humu kuwa hiyo ni golden opportunity ya kuiambia dunia kuwa uchaguzi wetu haukuwa huru na wa haki, you just tell it infrot of their faces, mpaka CNN, BBC na vyombo vya habari vya kimataifa vilikuwepo. Nilishambuliwa sana, ila nilisimama niliposimama.

Waliposusio hatuba ya rais pale bungeni Dodoma, pia nilikuwepo, nilisema tena it was not right na tulipofanya mjadala wa kumtambua rais au kutomtambua, pia nilisema, its a waste, kutomtambua kwa kauli na kumtambua kwa vitendo. Rais ana axist in real man hivyo umtambue usimtambue anabaki ni rais na yupo, hivyo kutomtambua ni kujidanyanya.

Nikimalizia hili la juzi, kwanza Lissu ni school mate wangu pale Ilburu, hivyo namfahamu fika, pili tulikuja kukutana nae Atlanta akiwa mwana harakati wa LEAT, hotuba yake ilikuwa na lots of flaws, kwa vile yeye ndie waziri kivuli wa sheria, Chadema walimwachia afanye kila kitu kwenye hotuba ile, laiti kama ingepitiwa na wabunge wengine wa Chadema, makini zaidi ya Lissu, wangekuja bna hotuba nyingine bora zaidi.

Naunga mkono walkout kama ishara ya protest lakini siungi mkono kuususia mjadala mzima bungeni unaomalizika leo. Japo Chadema inao wanasheria makini, lakini ni bure kabisa, wameshindwa kutumia upportunities za kuuzuia uwasilishwaji wa muswada huo kwa mara ya pili ambazo ziko proivided for na kanuni, hivyo kupoteza golden chance ya kuusimamisha muswada ule.

Kanuni za bunge ziko wazi kabisa kwa mbunge asiyeridhika na uwasilishwaji wa muswada na unaeleza wazi nini cha kufanya!. Chadema hawakufanya walichotakiwa kufanya na sasa wanaishia kuysusa huku wenzao wanazungumza!. Leo muswada unamalizika, bunge litakaa kama kapati kupitia kifungu kwa kifungu, vifungu vyote vitaafikiwa, bunge likakaa kama bunge, watausoma kwa mara ya tatu na kuupitisha hapo hapo.
Na kwa hasira na kibri, Jumatatu, JK atausaini kwa mbwembwe pale ikulu na utakuwa sheria!. Who are the looses?!.

Maadam Chadema wameamua kufa kuzungu na tai shingoni, na hawawezi tena kumeza matapishi yao, hii naiongeza kwenye ile list yangu ya "Chadema are Wrong!. That was yet Another Big Mistake!". (Naianzishia thread yake).


Pasco.
 
Kuhusiana na dhamira; je, yao hii ni moja ya dhamira zisizo huru?! Na ikifafanuliwa kama dhamira, je, katika mpambano kati ya dhamira huru na ile isiyo huru ni sharti iliyohuru ishinde?!

swali zuri sana. Watu wanaweza kutofautiana katika kujenga dhamira (formation of conscience). Sasa conscience inajengwa kwanza kwa kupewa taarifa sahihi na ukweli.

Dhamira haijengwi kwa kuukataa ukweli bali kwa kuutafuta na kuupata ukweli, kutafuta chema na kizuri (search for the truth, good, and beautiful). Dhamira ya mwanadamu basi inahitaji ukweli ili iweze kufikia uamuzi sahihi. So, mtu anapokataa kitu anaweza kukataa lakini anakataa kwa sababu anajua ukweli au anakataa kwa sababu hataki ukweli?

Hivyo ni dhamira ile ambayo iko katika upande wa ukweli ndiyo iko huru - utaifahamu 'kweli nayo kweli itawaweka huru'
 
Ndugu wanajamii na wananchi wengine,
Inasikitisha sana hali ya wasiwasi iliyopo miongoni wa wabunge, viongozi wa serikali na wananchi kwa ujumla juu ya mtafaruku uliotokea bungeni hatimaye wabunge wa Chadema na baadhi ya wabunge wengine wa upinzani kutoka bungeni. Matukio haya ya walkout bungeni yanaashiria matatizo au dissatisfaction miongoni mwetu; hali yetu ya amani ipo hatarini. Ushindani wa pande mbili ambazo hakuna anayekubali kumsikiliza au kumwamini mwenzake, ni mbaya sana.

Naomba kupitia kwa Mh Pinda ,Waziri Mkuu, kuangalia upya msimamo wa serikali katika suala hili la mswada. Nashukuru na ilikuwa ni busara kwa serikali, kufanya marekebisho yalioyafanywa mara ya kwanza ambapo wengi wa wananchi wa Zanzibar walikuwa wameukataa mswada hata na kuuchana. Lakini baada ya marekebisho, mswada umekubalika vizuri na wazanzibari. Kama sikosei, moja ya suala walililokuwa wanakataa ni Raisi wa JMT kupata ushauri kutoka kwa Raisi wa Zanzibar, neno “may” lilileta utata. Sasa neno “shall” limetumika na kubadilisha hali ya hewa kabisa. Kwa kweli azma ya awali ya serikali ya kuwepo na utashi kwa raisi wa JMT kupata ushauri kutoka kwa Raisi wa Zanzibari ilikuwa sahihi.Kwa nini nasema hivi: Raisi wa JMT ni yupo juu ya Raisi wa Zanzibar, hivyo neno “may” lilikuwa appropriate. Kama ilivyokuwa katika hotuba ya Upinzani iliyosomwa Mh Lissu, kwamba serikali ya Tanganyika inapashwa kuwepo na ndiyo Raisi wake ndiye anapashwa to consult Raisi wa Zanzibar, na sio wa JMT. Hivyo suala la serikali tatu is inevitable. Wabunge wa Zanzibar wamekuwa na hamaki dhidi ya Chadema bila sababu.

Sidhani kama Chama cha Chadema wanasema hawataki muungano, bali yafanyiwe marekebisho juu ya muungano huo, moja ni hili la kuwa na serikali tatu. Hakuna sehemu nyingine yakufanya marekebisho hayo bali katika mswada huu. Ingawaje suala la mjadala wa katiba bado, lakini kuwepo na provision au tahadhari ya kuwepo katika katiba mpya. Naamini serikali tatu utatoa matatizo mengi (Kero) za Muungano.

Serikali isione aibu kuondoa mswada huu na kuanza upya, kwani kuacha hali hii iendelee tutapata matatizo makubwa ambayo uenda hata katiba tuyotaka, haitapatikana. Kuondoa mswada tunaweza kuonekana kuwa tunachelewesha, lakini zipo faida kubwa sana. (a) Kutakuwepo na hali ya utulivu na amani (b) hali hiyo ya amani itafanya wananchi waweze kuchangia na kutoa maoni mazuri katika mstakabali wa nchi yetu. c) Mtafaruku wa wananchi utaathiri maendeleo kwa ujumla, hatuitaji maandamo ya mara kwa mara.

Endapo mswada ukiwa withdrawn , utatoa nafasi nyingine kwa wananchi kuujadili tena. Tuwape kamati zetu zifanye tena mikutano ya kupata maoni yao. Hakuna baya katika hili. Nadhani wataalamu wetu hata Prof Shivyi alishauri hivyo, kutokana na mabadiliko mengi ya msingi kufanyika kwenye mswada. Hili sio jambo la kushindana na kushabikia kwa nguvu zote.

Naiomba sana serikali yetu na Spika wetu wa Bunge, kuangalia upya msimamo huo. Jamani tunahitaji amani, utulivu, furaha, heshima na hatimaye maendeleo. Kauli za baadhi ya Wabunge kuwa Mh Lissu apate mkong’oto, Eti wanataka kuleta ukameruni! Hizi si kauli nzuri kutolewa na wabunge, Jamani hatufafika huko ambapo Mwl Nyerere alikuwa anafikiria tuwe.

Chonde chonde chonde jamani!!!
 
Asante, Mzee Mwanakijiji kwa hili, ila mimi naomba kutofautiana na wewe, na msimamo wa Chadema.

Wakati wa kutangaza matokeo ya urais, mimi binafsi nilikuwepo pale ukumbini, Chadema walisusa, nilitofautiana nao na nikasema humu kuwa hiyo ni golden opportunity ya kuiambia dunia kuwa uchaguzi wetu haukuwa huru na wa haki, you just tell it infrot of their faces, mpaka CNN, BBC na vyombo vya habari vya kimataifa vilikuwepo. Nilishambuliwa sana, ila nilisimama niliposimama.

Waliposusio hatuba ya rais pale bungeni Dodoma, pia nilikuwepo, nilisema tena it was not right na tulipofanya mjadala wa kumtambua rais au kutomtambua, pia nilisema, its a waste, kutomtambua kwa kauli na kumtambua kwa vitendo. Rais ana axist in real man hivyo umtambue usimtambue anabaki ni rais na yupo, hivyo kutomtambua ni kujidanyanya.

Nikimalizia hili la juzi, kwanza Lissu ni school mate wangu pale Ilburu, hivyo namfahamu fika, pili tulikuja kukutana nae Atlanta akiwa mwana harakati wa LEAT, hotuba yake ilikuwa na lots of flaws, kwa vile yeye ndie waziri kivuli wa sheria, Chadema walimwachia afanye kila kitu kwenye hotuba ile, laiti kama ingepitiwa na wabunge wengine wa Chadema, makini zaidi ya Lissu, wangekuja bna hotuba nyingine bora zaidi.

Naunga mkono walkout kama ishara ya protest lakini siungi mkono kuususia mjadala mzima bungeni unaomalizika leo. Japo Chadema inao wanasheria makini, lakini ni bure kabisa, wameshindwa kutumia upportunities za kuuzuia uwasilishwaji wa muswada huo kwa mara ya pili ambazo ziko proivided for na kanuni, hivyo kupoteza golden chance ya kuusimamisha muswada ule.

Kanuni za bunge ziko wazi kabisa kwa mbunge asiyeridhika na uwasilishwaji wa muswada na unaeleza wazi nini cha kufanya!. Chadema hawakufanya walichotakiwa kufanya na sasa wanaishia kuysusa huku wenzao wanazungumza!. Leo muswada unamalizika, bunge litakaa kama kapati kupitia kifungu kwa kifungu, vifungu vyote vitaafikiwa, bunge likakaa kama bunge, watausoma kwa mara ya tatu na kuupitisha hapo hapo.
Na kwa hasira na kibri, Jumatatu, JK atausaini kwa mbwembwe pale ikulu na utakuwa sheria!. Who are the looses?!.

Maadam Chadema wameamua kuyfa kuzungu na tai shingoni, na hawawezi tena kumeza matapishi yao, hii naiongeza kwenye ile lust yangu ya "Chadema are Wrong!. That was yet Another Big Mistake!". (Naianzishia thread yake).


Pasco.
unaweza kuona hili kama kosa la CDM na mafanikio kwa CCM na CUF kwa sasa, lakini Tanzania ipo hata baada ya 2015 na dhamila huru zisizo na unafiki zitaendelea kuwepo hata kama wanaharakati wa sasa hawatakuwepo au kutokuwa na uwezo wa kutenda kama wanavyotenda sasa. IKiwa malalamiko ya msingi hayatashughurikiwa sasa kwa kulazimisha kutungwa sheria inayokataza mambo yanayowahusu raia moja kwa moja kujadiliwa ni kuahirisha tatizo na kujenga nyumba kwa mbao sehemu yenye mchwa. Kama CCM wana ahirisha tatizo is ok, lakini amini kuwa hata kama CDM, NCCR,TLP etc visipokuwepo katiba isiyotokana na mchakato huru utabaki agenda kwa chaguzi zijazo.
 
swali zuri sana. Watu wanaweza kutofautiana katika kujenga dhamira (formation of conscience). Sasa conscience inajengwa kwanza kwa kupewa taarifa sahihi na ukweli.

Dhamira haijengwi kwa kuukataa ukweli bali kwa kuutafuta na kuupata ukweli, kutafuta chema na kizuri (search for the truth, good, and beautiful). Dhamira ya mwanadamu basi inahitaji ukweli ili iweze kufikia uamuzi sahihi. So, mtu anapokataa kitu anaweza kukataa lakini anakataa kwa sababu anajua ukweli au anakataa kwa sababu hataki ukweli?

Hivyo ni dhamira ile ambayo iko katika upande wa ukweli ndiyo iko huru - utaifahamu 'kweli nayo kweli itawaweka huru'

Ngoja tuangalie mawazo mema ya binadam huyu na tutafakari katika mazingira yanayoendelea ndani ya nchi yetu TUKUFU ;

''The most dangerous man, to any government, is the man who is able to think things out for himself." ~ H. L. Mencke

Wengi wenu humu ndani mu hatari sana kwa serikali yetu,ni vema tujizatiti kuitafuta kweli yote na kuisimamia iwafikie Watanzania wenzetu wengi ambao kwa kiasi kikubwa hawana uhuru binafsi wa kuwaza,hawajui kama kitu pekee ambacho MUNGU amewapa uhuru wa matumizi yake kwa 100% pasipo kuingiliwa na binadam awaye yote ni MAWAZO,lakini wengi wa Watz wameweka Imani yao kwa watawala na wasomi ambao kwa kiwango kikubwa wameamua kusitisha kwa makusudi kazi ya kuwaza wamebaki kunena vitu bila kuviwazia kwa mapana yake.

Nilimsikiliza Profesa ???? nafikiri ni pro Fedha akiongea na wabunge, aliamua kuzima kabisa kitengo cha kufikiri na kuendeleza bla bla kwenye jambo zito kama KATIBA, haya mara kaja Dr mwingine toka kitivo cha siasa UDSM nae ameamua kuswitch off kitengo cha kufikiri na kuamua kubwabwaja hovyo, amefikia kuaminisha watu kuwa CDM wanataka kupunguza madaraka ya RAIS kinyume cha katiba iliyopo, najiuliza madaraka ya Rais yanaingiaje kwenye sheria ya namna ya mchakato wa kutengeneza katiba mpya, katiba haiwezi kuwa mali ya mtu mmoja au taasisi moja.

Rais ni taasisi haiwezi pekee yake iachiwe kutengeneza mchakato wa kutengeneza katiba mpya,kwani sheria hiyo ikitamka kwamba TUME YA KUREKEBISHA KATIBA itakuwa na wajumbe 50,taasisi ya Raisi itatoa wajumbe 4, taasisi ya Mwanakijiji itatoa wajumbe wawili, taasisi ya nkwesa makambo itatoa wajumbe 2 nk.nk na kuhusisha taasisi nyingi za kijamii kadri inavyowezekana ili kwamba zenyewe ndo zitengeneze hadidu za rejea. HII yote haiwezekani kwa sababu wengi wa waliokwenye nafasi za kupeleka mbele mawazo huru,hawawazi kwa uhuru na wakati m,wingine hawawazi kabisa.

CDM walichofanya kimebeba ujumbe mzito sana na kitawafunguwa wengi kutoka katika jela ya kutokuwaza...
 
CCM wanafikiri kuwa watatawala nchi hii milele kama wasemavyo. Dola ya Kirumi iko wapi? KANU iko wapi? ni suala la wakati tu. Bali kibaya ni kuwa wanatutia umaskini wa kujitakia. Tia tia maji itakuja watumbukia tu! WAtakuwa wapinzani siku moja na sio siku nyingi.
 
Nimebakia na maswali kadhaa nikijiuliza kuhusu dhamira ya Rais Kikwete alipokubariana na kuandikwa Katiba Mpya, jambo ambalo halikua katika agenda zake wala Ilani ya chama chake alikua na malengo gani? Alikuwa anaamanisha kuwepo Katiba ambayo itapatikana kwa vigezo vinavyokubarika ama ujanjaujanja?

Kama wasaidizi wake (Werema na Kombani) walipinga mchakato huu, imekuaje amewaachia hii kazi? Ni kikao/vikao vilifanyika ndani ya chama chake kukubariana juu ya kuandikwa Katiba mpya? Kama wana CCM wenzake walikua wanapinga,leo tuwaamini vipi wanapoteka mchakato na kuonyesha eti wao ni wapenzi wa Katiba mpya?

Kuna maswali mengi tu najiuliza na nadhani hata Watanzania wenzangu mtakua mnajiuliza bila kupata majibu.
 
Asante, Mzee Mwanakijiji kwa hili, ila mimi naomba kutofautiana na wewe, na msimamo wa Chadema.

Wakati wa kutangaza matokeo ya urais, mimi binafsi nilikuwepo pale ukumbini, Chadema walisusa, nilitofautiana nao na nikasema humu kuwa hiyo ni golden opportunity ya kuiambia dunia kuwa uchaguzi wetu haukuwa huru na wa haki, you just tell it infrot of their faces, mpaka CNN, BBC na vyombo vya habari vya kimataifa vilikuwepo. Nilishambuliwa sana, ila nilisimama niliposimama.

Waliposusio hatuba ya rais pale bungeni Dodoma, pia nilikuwepo, nilisema tena it was not right na tulipofanya mjadala wa kumtambua rais au kutomtambua, pia nilisema, its a waste, kutomtambua kwa kauli na kumtambua kwa vitendo. Rais ana axist in real man hivyo umtambue usimtambue anabaki ni rais na yupo, hivyo kutomtambua ni kujidanyanya.

Nikimalizia hili la juzi, kwanza Lissu ni school mate wangu pale Ilburu, hivyo namfahamu fika, pili tulikuja kukutana nae Atlanta akiwa mwana harakati wa LEAT, hotuba yake ilikuwa na lots of flaws, kwa vile yeye ndie waziri kivuli wa sheria, Chadema walimwachia afanye kila kitu kwenye hotuba ile, laiti kama ingepitiwa na wabunge wengine wa Chadema, makini zaidi ya Lissu, wangekuja bna hotuba nyingine bora zaidi.

Naunga mkono walkout kama ishara ya protest lakini siungi mkono kuususia mjadala mzima bungeni unaomalizika leo. Japo Chadema inao wanasheria makini, lakini ni bure kabisa, wameshindwa kutumia upportunities za kuuzuia uwasilishwaji wa muswada huo kwa mara ya pili ambazo ziko proivided for na kanuni, hivyo kupoteza golden chance ya kuusimamisha muswada ule.

Kanuni za bunge ziko wazi kabisa kwa mbunge asiyeridhika na uwasilishwaji wa muswada na unaeleza wazi nini cha kufanya!. Chadema hawakufanya walichotakiwa kufanya na sasa wanaishia kuysusa huku wenzao wanazungumza!. Leo muswada unamalizika, bunge litakaa kama kapati kupitia kifungu kwa kifungu, vifungu vyote vitaafikiwa, bunge likakaa kama bunge, watausoma kwa mara ya tatu na kuupitisha hapo hapo.
Na kwa hasira na kibri, Jumatatu, JK atausaini kwa mbwembwe pale ikulu na utakuwa sheria!. Who are the looses?!.

Maadam Chadema wameamua kufa kuzungu na tai shingoni, na hawawezi tena kumeza matapishi yao, hii naiongeza kwenye ile list yangu ya "Chadema are Wrong!. That was yet Another Big Mistake!". (Naianzishia thread yake).


Pasco.

Akili ipo timamu mbona kwenye RED na BLUE zinatofautiana Mkuu? premises deffer with conclusion
 
Back
Top Bottom