Dhambi ya Ubaguzi: Wafanyakazi the Guardian walalamika Wahindi kununuliana magari huku wafanyakazi wakilazimishwa kuwa vibarua

Yani hv hamuwajui wahindi waafrika ni watu ambao mpaka mwaka huu bado hawajui hila za watu wageni nchini kwao
 
Na ndio maana nashikiria msimamo wangu. Watoto wenu msiwaaminishe kuwa wakipata elimu ndio wametusua. Mwanangu soma upate maisha mazuri. Iala wewe hapo mwenye elimu sa hv na ajira yako upo frustrated kisa gari la mill 13.5.
Miaka 55 ni kawaida kwa private companies kustaafisha waajiliwa wao sio kama serikalini. They believe huna kipya nguvu zimeisha.

Cha msingi
Chukua chako mapema, na iwe funzo kwenu mkimuona mtoto wenu amejiajiri kaacha kazi msimsimange kwamba tafuta ajira sababu mnamtakia mwishoni aje kuwa na frustration kama ninyi.
Wapeni moyo na tumieni uzoefu wenu kusaidia watoto wenu waliojiajiri.

Kwa nini?

Kwa sababu hadi unafikisha miaka 55 hukumuandalia mazingira zaidi ya kumsisitiza aaome afaulu apate ajira.

Najua ni ngumu kukubali lakini ndio ukweli

Hapo mwenye maamuzi ni mmiliki, yeye kawaamini hao na hamuwezi kumpangia.
Ukweli huu mchungu naubeba mkuu
 
Huyo ndio tegemeo,hata tanzanite mzee alikua anauzia ofisini kwake bonite,nimeenda mara 2 kununua kipindi cha 2013
Basi anaaminika sana which is good. Tangu enzi za Toyota Cressida (Wine Color) mpaka leo ni miaka mingi imepita.
 
U
WAFANYAKAZI wa The Guardian ambao baadhi hawajalipwa mshahara wa mwezi wa tano kutokana na matatizo ya kibiashara wameshangazwa na hatua ya meneja mkuu, bwana Srinivas Chintaluri kumnunulia gari ndugu yake Bw Balaji Balasubramaniyan ambaye ni Mkurugenzi wa Teknohama aina ya Toyota Sienta lenye thamani ya 13.5m/-.

Bw Chintaluri ambaye pia ni Mkurugenzi wa Fedha wa ITV na Radio One, amekuwa akiwalazimisha Watanzania wenye umri wa miaka zaidi ya 55 kustaafu na kuchukua mafao yako NSSF na baada ya hapo kuwapa mikataba kama vibarua kwa shabaha ya kupunguza gharama za uendeshaji.

“Haileti maana kampuni inashindwa kulipa mishahara, kodi ya serikali na michango ya NSSF kwa wakati lakini uongozi wa Chintaruli unamnunulia mtu ambaye kimsingi hana utaalamu wowote wa IT huku Watanzania wenye uwezo wakisitishiwa mikataba,” alisema mmoja wa wafanyakazi hao.

Wafanyakazi hao wanadai Bw Balasubramaniyan kama ilivyo kwa Mkurugenzi wa Biashara Ajay Goyal and Meneja Uendeshaji, Murugan Eswar ni miradi maalum ya Mkurugenzi wa Bonite Bottlers, Zoeb Hasuji ambaye kwa kushirikiana na Mkuu wa Ulinzi wa IPP Media, Ayoub Semvua wamekuwa wakifanya jitihada za kuwatafutia vibali vya kufanya kazi nchini pasipo na ujuzi wowote.

“Huyu Bw Balasubramaniyan hana utaalamu wowote wa IT, baada ya kuwafukuza kazi Watanzania vijana Dotto na Gaetano mwaka jana na kubaki na Allan Mshana, hali imekuwa mbaya kwani kazi zote zinafanywa na Mtanzania Mshana kwani huyo Mhindi hana kitu,” alisema mfanyakazi mwingine huku akitaka Ofisi ya Kamishna wa Kazi kuchunguza kama Wahindi waliopo The Guardian Limited wanastahili kuwepo.

Wamesema wakati kampuni inadaiwa kufanya vibaya kibiashara hali hiyo haionyeshwi miongoni wa Wahindi hao ambao wanaendelea kupeana mikataba minono ya kununuliana magari, kulipiana nyumba, ada za watoto, gharama za matibabu na likizo huku wakiwa himiza Watanzania wenye umri wa zaidi ya miaka 55 kwenda kuchukua mafao yao NSSF kwa lengo la kupunguza gharama za michango.

“Tunaomba sana Serikali yetu kuingilia kati jambo hili na kufanya uchunguzi wa kina kwa sababu hata vijana wa Kitanzania mikataba yao ikiisha wanalazimishwa kusaini mikataba ambayo ni kinyume cha sheria kwa kunyimwa matibabu na familia zao, kupunguziwa mishahara na kadharika,” walisema.

Mwaka jana, wafanyakazi hao waliandika waraka kulalamikia uwepo wa Wahindi wasio na sifa huku kazi zao zikifanywa na Watanzania ambao kwa sasa wamesitishiwa mikataba yao.

Wahindi waliopo wamesababisha Watanzania kupoteza kazi ni Bw Goyal, Balasubramaniyan na Eswar wakati Chintaruli anafanya kazi The Guardian na ITV kinyume na Sheria za nchi.

Kazi za akina Goyal, Eswar na Balasubramaniyan zilikuwa zinafanywa kwa ufanisi na Watanzania Kauthar De Souza na Moez Kaderbhai ambao waliacha kazi mwaka jana kwa mizengwe ya menejimenti.

Lakini cha ajabu ni kwamba, uongozi wa Chintaluri kwa kushirikiana na Hassuji walisitisha mkataba wa kijana mdogo wa Kitanzania, Avit Riwa ambaye alikuwa Mhasibu Mkuu mwanzoni mwa mwaka jana kwa madai ya mshahara wake wa 6m/- kuwa kubwa sana. Riwa ambaye ni msomi mwenye MBA na CPA, aligoma kupunguziwa mshahara. Mshahara wake ulijumuisha pango la nyumba na gari lake ambalo aliendesha mwenyewe.

Jambo la ajabu ni kwamba wakati Hassuji na wasaidizi wake wanafanya kila liwezekanalo kuwaleta Wahindi kufanya kazi TGL, kampuni imeendelea kufanya vibaya kibiashara kiasi kwamba wafanyakazi hawajalipwa mishahara kwa miezi miwili sasa huku pesa nyingi ikitumika kuhonga maafisa wa serikali ili kupata vibali vya kazi vya kuishi nchini na polisi ili kujinusuru na tuhuma mbalimbali za uhalifu zinazowakabili.
Umenikumbusha kule Moshi Kilimanjaro, kampuni ya bonite bottlers ltd inaitwa in ya Regnald mengi kumve ni ya wahindi kuanzia malori ya kihindi Hadi wafagiaji ni wahindi
 
U

Umenikumbusha kule Moshi Kilimanjaro, kampuni ya bonite bottlers ltd inaitwa in ya Regnald mengi kumve ni ya wahindi kuanzia malori ya kihindi Hadi wafagiaji ni wahindi
Baada ya jamaa kufa wamechukua kampuni wao,nafikiri walikuwa shareholders
 
ITV ikiendelea hivi na watoto wa Marehemu Mengi wakiwa wanazubaa zubaa tu, inakufa within 5 years. Poor management ishaanza na ITV itakufa soon
 
mkurugenzi kuwa na gari unaona noma au kumnunulia ndugu yake umeona tabu unajua mshahara wa mkurugenzi wewe mbeba chupa za soda
 
Back
Top Bottom