Mchaka Mchaka
JF-Expert Member
- Jul 20, 2010
- 4,516
- 1,404
kabila lake pekee linampa sifa ya kugombea kupitia CDM. Halafu lazima pia wamlipe kwa kazi alio ifanya(kuuwawa kwa chacha)
Uwezo wako wa kutafakari umeishia hapo? kweli wewe ni anasi!
kabila lake pekee linampa sifa ya kugombea kupitia CDM. Halafu lazima pia wamlipe kwa kazi alio ifanya(kuuwawa kwa chacha)
Sitta ni mwana ccm,fuatilia vyema aliyoyasema.Na alimtahadharisha Wangwe kuhusu uwakilishaji wa hoja hiyo iliyohusiana na kampuni ya uchimbaji wa madini...fwatilia mkuu.Kipindi hicho Sitta akiwa spika wa bunge la jamuhuri.
Yule dogo aliyemfanya kitu mbaya Chacha Wangwe!
Yule dogo aliyemfanya kitu mbaya Chacha Wangwe!
huyu si ndo Lipumba aliema ana taarifa za kiintelijensia kuwa kafunzwa ugadi libya
Huyo huyo, Zitto alipopangiwa awe dereva wake alichomoa
bwana deus hata kama cyril n ndugu yako hakuna mantik ya kutogombea hapo, kwanza ww una undugu wa mbali sana na watu wa chami huku ni kwa wajomba wako tu(DAKAU)
Kwa ninavyowafahamu viongozi wa CDM kama kungekuwa na mkono wa serikali povu lingewatoka na kulaani,wangetangaza siku yake maalum lakini leo hata kwa bahati mbaya Chacha Wangwe hatajwi katika harakati za CDM.Kwa kuwa alikuwa shujaa nje ya chama lakini ndani ya chama ni kikwazo kwa wezi wa pesa za ruzuku. Sitoshangaa Mallya akilipwa fadhila kwani mission accomplished.
Nimeshangaa kwa nini GT wanahangaika kukujibu ili hali wanajua lengo lako. Kama hawalijui nina mashaka na u GT wao.Kuna taarifa kutoka sehemu mbali mbali huku Moshi Vijijini na baadhi ya maeneo ya Dar kuwa yule mfanyabiashara aliyehusishwa na ajali ya Chacha Wangwe (Deus Mallya) anaendelea na mikakati yake ya kugombea Ubunge kwenye Jimbo la Moshi Vijijini ambalo kwa sasa linaongozwa na Cyril Chami 'Aliyepigwa chini' kwenye baraza jipya la mawaziri la JK.
Mara kadhaa Deus Mallya amekuwa akikwepa kujibu hili sasa tunaomba kwa kuwa yupo huku atujibu.
Nawasilisha.
Kwanza naomba Radhi kwa kuchelewa kujibu hapa. Account yangu ya Deus F Mallya ina tatizo najaribu kuingia nasahau Password (Au ni tatizo la kiufundi).
Pili nitajibu hoja zote kwa umakini (Japo kwa ufupi) kwama ifuatavyo:
1. Swali la Kugombea au kutokugombea Ubunge Jimbo la Moshi Vijijini sijawahi kutangaza popote. Hata hivyo wakati ukifika na nikiamua kugombea si dhambi. (Rufaa #52/2010 chini ya Jopo la majaji watatu wakiongozwa na Mhe.Jaji.H.R.Nsekela walinipa ushindi baada ya kugundua makosa makubwa yaliyokuwepo kwenye shauri langu dhidi ya Serikali mkoani Dodoma kuhusiana na ajali ya gari mwaka 2008)
2. Ni kweli kuwa Cyril Chami (Mbunge wa Sasa) ni Ndugu yangu (Mjomba mdogo).
3. Si kweli kuwa nimeoa Mtoto wa kiongozi wa ccm huko Kilimanjaro. (Sijao bado)
....Naendelea kujibu mengine.
Alikuwa na udouble agent flani,upande wa pili ndo walimgeuka.Umemsahahu kaka yake ambaye ni ccm nadhani anaitwa samweli wangwe kama sikosei.Yeye alikataa hata uchunguzi wa ziada kwa mwili wa marehemu usifanyike.Na kulitokea mgogoro serikali ya ccm ikauteka mwili wa Wangwe RIP.Kumbuka kulikuwa na tetesi za yeye kupigwa risasi ya mdomo.
Majibu mengine:
Inadaiwa kuwa kuna watu waliokuwa 'Nyuma ya pazia' kwenye kesi ile (Ndiyo maana ilifunguliwa wilaya ya Dodoma Mjini badaya ya Kongwa). Binafsi sina majibu hapa Duniani. Mimi ni Binaadamu kama walivyo wengine. Pia mimi ni mgumu sana kuzungumza nisichokuwa na uhakuka nacho. Ikiwa wapo waliokuwa 'Nyuma ya pazia' kuzuia lengo langu 2010 (Japokuwa halikuwepo kiukweli) Nilishamwambia Mungu Ashughulike nao.
Kuna mdau hapo juu amesema kuwa 'Atapitishwa' Komu 2015. Naomba kumhakikishia kuwa CHADEMA na CCM ni tofauti kama ilivyo Jehanum na Mbinguni. Maamuzi ya CHADEMA huwa hayafanywi kama ya CCM!.. CHADEMA kuna viongozi,CCM kuna Watawala. Kuna taratibu za kumpata mgombea kwa mujibu wa katiba kwa maana hiyo hata kama nisipogombea/kutokupitishwa kwenye kura ya maoni bado nitakuwa na imani na Kiongozi atakayepitishwa. By the way bado tupo kwenye main road kuelekea M4C nadhani haya si vyema sana kujadili kiundani kwa sasa.
Sote ni ndugu,tatizo ni CCM!.