Allineando
JF-Expert Member
- Aug 7, 2016
- 2,064
- 1,122
Muongo mkubwa wewe.. Mpiga debe tuu unaonyesha
Siyo kweli mkuu. Unawafahamu Kagame na Nkurunzinza? Je, dhambi zao za kubadili katiba zilianzia kwa wananchi?Hata siamini, maana mchakato wa kubadili Katiba huanzia kwa Wananchi > Bungeni > Raisi.
huyu kibamba nae amekuwa zwazwaaa, au?Habari zenu familia ya JF.
Niende kwenye mada hapo juu.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba nchini, Deus Kibamba akihojiwa hivi punde na Radio DW Idhaa ya kiswahili ya Born Ujerumani, ktk kipindi cha Africa Wiki Hii, amesema Kikwete alijaribu kwa siri sana kuongeza mihula ya Urais lakini mpango wake wa kubadili kipengele hicho cha katiba ukashindikana.
Cha ajabu ni kuwa Kikwete alikuwa akidai kauchoka urais na anatamani muda wake uishe akapumzike. Hivi Kikwete kipindi kile angeibuka hadharani na kutangaza nia yake hiyo ya kutaka kuendelea na uongozi wa nchi hali ingekuwaje wakati huo?
Je kama Kikwete ndiye Rais hadi Leo tungekuwa na hali gani kiuchumi, kisiasa, kidiplomasia na maeneo mengine muhimu?