Deudatus Balile Ateuliwa Mhariri Mtendaji wa New Habari Corporation

Huyu Bashe si sio raia sasa ana work na resident permits? Hiyo kazi haiwezi kufanywa na Mtanzania mapaka foreigner aifanye?
 
Hivi huyu Bashe ndiye yule aliyegombea ubunge wa CCM Nzega,?

Na Bashe wake ni huyu,

2925.png
 
Kulikuwa na thread hapa juzi ikieleza kupewa nafasi ya uhariri mkuu kwa Deodatus Balile ambaye ana undugu na Salva Rweyemamu wa Ikulu. Wengi walisikitika mtu huyu kupewa nafasi kwa kuwa walijua magazeti hayo ambayo siku za karibuni yalianza kuchukua mkondo mpya wa kuzungumzia ukweli,kwmba yangeanza kurejea kule kule kwenye propaganda. Ukweli ni leo maana limejaa JK oooh hiki aaaah kile? Yaani hata habari za Loliondo ambazo walikuwa wanatupa kwa kina wameona hazifai huku magazeti yote yakieleza kipato cha Babu. Haya yetu macho na madudu yenu
 
sidhani kama habari ya Loliondo ni habari itakayoongezea taifa kipato wala tija

having said that, pia siamini kama gazeti la fisadi linaweza kusaidia chochote watanzania... lifungiwe tu!!
 
Mtoa mada unatakiwa kupewa semina ili ujuwe jinsi ya kuyatambuwa magazeti huru, hivi wewe na akili zako timamu Habari corpotion ndio inayomiliki gazeti la Mtanzania, na hiyo kampuni ni mali Fisadi Rostam Aziz, wewe unategemea habari gani yenye maslahi ya Taifa kutoka kwenye media hiyo? na ni kwa nini unaendelea kununuwa magazet hayo ili hali huku ukijuwa unazidi kumtajirisha huyu Jambazi Rostam Aziz?
 
Watanzania tuna tatzo la kutokujua magazeti yepi ya kusoma kwa manufaa yetu na ya vizazi vijavyo ...wana JF tunaomba mtoe elimu hii kwa wasomaji wetu
 
Watanzania tuna tatzo la kutokujua magazeti yepi ya kusoma kwa manufaa yetu na ya vizazi vijavyo ...wana JF tunaomba mtoe elimu hii kwa wasomaji wetu

Rweye, kwa vile nawe ni mwana JF na umegundua Watanzania tuna tatizo la kutokujua magazeti yepi ya kusoma kwa manufaa yetu na ya vizazi vijavyo, hivyo kuwaomba wana JF kutoa elimu hii kwa wasomaji wetu, ningekuomba tuanzie na wewe kutuelimisha ni magazeti yepi ya kusoma kwa faida ya yetu na vizazi vijavyo?.
 
Rweye, kwa vile nawe ni mwana JF na umegundua Watanzania tuna tatizo la kutokujua magazeti yepi ya kusoma kwa manufaa yetu na ya vizazi vijavyo, hivyo kuwaomba wana JF kutoa elimu hii kwa wasomaji wetu, ningekuomba tuanzie na wewe kutuelimisha ni magazeti yepi ya kusoma kwa faida ya yetu na vizazi vijavyo?.

Mwananchi
The citizen
Raia Mwema
MwanaHalisi
Guardian
Daily News ( kama sio wakati wa kampeni za uchaguzi )
Kulikoni
Tanzania Daima
Nipashe.
 
Rai na Mtanzania ni magaezeti yake JK na Mshikaji wake Rostam Aziz. Halafu Uhuru na Mzalendo ni magazeti dada.
 
Mwananchi
The citizen
Raia Mwema
MwanaHalisi
Guardian
Daily News ( kama sio wakati wa kampeni za uchaguzi )
Kulikoni
Tanzania Daima
Nipashe.

Hapo umenena! Ila hayo yenye Red siyaamini amini vile? Raia Mwema sijawahi hata kulisoma. Daily News sidhani maana linamilikiwa na Serikali ya Mafisadi haliwezi kututendea haki wa-TZ ila unaweza kulinunua na kukimbilia kwenye ukurasa wa matangazo ya nafasi za kazi tu basi!

Zamani nilikuwa mpenzi sana wa magazeti ya Habari Corporation lakini tangu yameuzwa sina hamu nayo kabisa wala sikumbuki kama huwa najishughulisha hata kusoma vichwa vya habari kwa wauza magazeti!!!

Nafikiri hayo magazeti ya Fisadi Mkuu tukiyasusia atafunga kampuni ya magazeti. Tunaomba siku moja apatikane mtu wa kutuhamasisha kufanya mgomo.
 
Hapo umenena! Ila hayo yenye Red siyaamini amini vile? Raia Mwema sijawahi hata kulisoma. Daily News sidhani maana linamilikiwa na Serikali ya Mafisadi haliwezi kututendea haki wa-TZ ila unaweza kulinunua na kukimbilia kwenye ukurasa wa matangazo ya nafasi za kazi tu basi!

Zamani nilikuwa mpenzi sana wa magazeti ya Habari Corporation lakini tangu yameuzwa sina hamu nayo kabisa wala sikumbuki kama huwa najishughulisha hata kusoma vichwa vya habari kwa wauza magazeti!!!

Nafikiri hayo magazeti ya Fisadi Mkuu tukiyasusia atafunga kampuni ya magazeti. Tunaomba siku moja apatikane mtu wa kutuhamasisha kufanya mgomo.
Kama wewe ni mpenda mabadiliko chanya ya kweli, anza Jumatano ijayo kusoma gazeti la Raia Mwema. Lina uchambuzi wa upeo mkubwa wa masuala katika kupigania mabadfiliko chanya kupitia kwa waandishi wenye weledi mkubwa wa fani.Katika misingi ya kimabadiliko chanya naweza nikasema bila kusita sita kwamba kwa sasa gazeti hilo la kina Jenerali Ulimwengu, Johnson Mbwambo,John Bwire, Francis Chirwa na wengine liko juu mno positively kimabadiliko.Prove that yourself.
 
Jenerali hakua na njia alichomwa kisu cha mgongoni na Salva asijue kumbe mwenzake anajikomba kwa Rostam na kumueleza siri zote za matatizo ya kampuni yetu tuliyoipenda, RA akatumia nafasi yake kuwachongea TRA wakawabana wasijali kama kampuni ya wazawa, kodi juu salva kama ME halipi hata stuatuatory anachofanya ni ku transfer hela za kampuni kumhonga mkewe aliyekua anaishi uingereza kwa jasho letu, mwisho jenerali na wenzie wakaachia ngazi, Salva akahongwa ukurugenzi ikulu baada ya kusota mtaani na kumuandikia RA barua ya kumsimanga tuliyoisoma humu JF. kauma kampuni aliyokua mkurugenzi kwenda kuajiriwa kwa kazi ya dola ngapi vile? hebu tuambieni mshahara wake na DSA za safari ndio maana wanazigombani
 
Mtoa mada unatakiwa kupewa semina ili ujuwe jinsi ya kuyatambuwa magazeti huru, hivi wewe na akili zako timamu Habari corpotion ndio inayomiliki gazeti la Mtanzania, na hiyo kampuni ni mali Fisadi Rostam Aziz, wewe unategemea habari gani yenye maslahi ya Taifa kutoka kwenye media hiyo? na ni kwa nini unaendelea kununuwa magazet hayo ili hali huku ukijuwa unazidi kumtajirisha huyu Jambazi Rostam Aziz?

Umemaliza kila kitu mkuu wangu! Ni ufisadi kujadili magazeti haya uchwara na yasiyo na maadili. Bora hata magazeti ya Shigongo.
 
Nilimjua Balile kupitia makala zake akiwa gazeti la Mwananchi wakati huo,alikuwa mwandishi mahiri kweli kweli akisimamia ukweli.Baadae alichukuliwa na Hansbert Ngurumo kuanzisha gazeti la Tanzania Daima kabla ya kuelekea Hull university kaufanya masters sikumbuki ilikuwa ni ya nini,akiwa Hull alikuwa bado akiliandikia Tanzania Daima,nilikuwa bado mpenzi wa makala zake.

Ngoma ni aliporudi toka huko na kujiunga na Habari Corporation ndipo alipoanza kula matapishi yake,huo utumbo plus bla bla bla anazoziimba mpaka leo huwa najiuliza huyu jamaa ni mzima kweli?

Nasikia yeye na Muhingo Rweyemamu(mtaalamu wa siasa za matope-issue ya Hizbu kama mwaikumbuka) ndio waliomuondoa Tagalile kwenye uhariri mtendaji baada ya kuwa kikwazo kwao na habari zao za kupika.Balile ndiye aliyekuwa akipika habari za ndoa ya Dr.Slaa na Josephine mpaka ikawa kichefuchefu....kweli njaa mbaya sana.
 
Huyo huyo n a uraia karejeshewa.Mambo burudaaaanii,papai kwa kujiti na kule CCM anapeta tu.
 
Back
Top Bottom