Dereva huyu wa gari la mwendokasi aonywe!

Tanzania Mpya

JF-Expert Member
Apr 11, 2012
253
144
Nilipanda basi la Mwendo Kasi kutoka Kariakoo kwenda Ubungo asubuhi hii kwenye saa 2 na robo hivi.

Nimemshangaa Dereva wa basi namba T144DGW anavyoendesha kwa speed kubwa na kutoacha nafasi ya kutosha kati yake na mwenzake aliye mbele yake! Anafanya michezo kama dereva wa daladala, anamfuata mwenzake kwa karibu mno na kusababisha kufunga breki za ghafla pale mwenzake wa mbele anapopunguza mwendo au kusimama.

Kuna wakati nilihisi kwamba atamgonga yule wa mbele! Hata aliposimama kituo changu cha Shekilango, jamaa anaingia kituoni kwa speed na nafasi aliyoicha kati yake na sakafu ya kituo ni sentimita chache tu tofauti na wenzake wanavyosimama.

Naomba Mamlaka ya husika imuonye Dereva huyo ajirekebishe la sivyo ataisababishia hasara Serikali muda si mrefu. Hawa madereva wakumbuke kwamba haya magari pamoja na miundombinu yake vimegharimu fedha zetu nyingi, kwa hiyo wawe waangalifu.

Nashauri pia wapimwe kama wamelewa kabla ya kukabidhiwa magari hayo.

Mungu ibariki Tanzania.
 
acha uzushi na kulalamika mwendo kasi zinatembea hazi kimbii gari hazifiki hata speed 60 unasema zinakimbia??

ukipanda gari na ikafika speed 100 siutasema inapaaa??

Hana sababu ya kushindana utadhani anawahi kugombania abiria ili afikishe mahesabu ya jioni. Any way, una haki ya kuwa na mtazamo wako tofauti.
 
Bila shaka ulinyang'anywa hiyo gari akapewa au kakuchukulia mke? Sounds like majungu
Nilipanda basi la Mwendo Kasi kutoka Kariakoo kwenda Ubungo asubuhi hii kwenye saa 2 na robo hivi. Nimemshangaa Dereva wa basi namba T144DGW anavyoendesha kwa speed kubwa na kutoacha nafasi ya kutosha kati yake na mwenzake aliye mbele yake! Anafanya michezo kama dereva wa daladala, anamfuata mwenzake kwa karibu mno na kusababisha kufunga breki za ghafla pale mwenzake wa mbele anapopunguza mwendo au kusimama. Kuna wakatinilihisi kwamba atamgonga yule wa mbele! Hata aliposimama kituo changu cha Shekilango, jamaa anaingia kituoni kwa speed na nafasi aliyoicha kati yake na sakafu ya kituo ni sentimita chache tu tofauti na wenzake wanavyosimama.

Naomba Mamlaka ya husika imuonye Dereva huyo ajirekebishe la sivyo ataisababishia hasara Serikali muda si mrefu. Hawa madereva wakumbuke kwamba haya magari pamoja na miundombinu yake vimegharimu fedha zetu nyingi, kwa hiyo wawe waangalifu. Nashauri pia wapimwe kama wamelewa kabla ya kukabidhiwa magari hayo.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Mleta mada ana hoja. Dereva huyu hafai Kwa mabasi haya jana nusura agonge pedestrians Tip top manzese. Mabasi haya hayatakiwi kwenda zaidi ya 60km per hour. Yana style yake ya uendeshaji kwa waliobahatika kufika kule yalipozoeleka. Huyu dereva nadhani alikuwa wake Ngorika.
 
Back
Top Bottom