Ha haaa, we ndugu yangu Rutunga kweli story yako inaendana na jina lako ni ya kutunga! sasa nakuweka sawa,usisikie poroja za kihuni za wafama maji au wenye wivu wanaokaribia kujinyonga,Huyu jamaa (mbunge mteule) ni mwadilifu kupita maelezo, ni mchapa kazi wa kuigwa ,ana uzalendo kwa nchi hii na record yako inathibitisha hivyo,now what happened is siku chache kable cam[paign kuanza alipata ajali jumapili moja akitoa kanisani kumcha Mungu kama ilivyo desturi yake.ajali ilitokea pale mlalakuwa alikuwa akiendeshwa na mwanae mmoja wa kiume, alipata mshituko sehemu ya shingo kwa sababu alikuwa anasoma gazeti wakati ajali hiyo inatokea,mimi binafsi ni kati ya watu wa kwanza kabis kuifka eneo la ajali,ambayo haikuwa ya kutisha sana,tulimpeleka hopitali akapimwa akapewa matibabu na kuruhusiwa siku hiyo hiyo ya jumapili, lakini maumivu yalipomzidia alishauriana na familia yake na chama chake na kwa kuwa hana mzaha na afya yake aliamua kwenda India kupata matibabu ya uhakika ambako alikaa for ten days na kurudi ngangari kuwahi kuelekea Ngara kuendelea na kampeni ambako amewabwaga wapinzani kwa kishindo plus wabaya wake wote .sasa unaposema hatembei hasimami una maana watu wangara wote ni wapumbavu kumpeleka mjengoni mgonjwa? alifanya je kampeni majimbo yote 20 ya ngara na kumpatia ushindi wa kishindo JK wa 84%? wewe ungeijua jiografia ya ngara ilivyo iusingeandika upuuzi kama huo,kule lazima uwe ngagari kinoma, the weakest fell by the way!! anayetaka kumuona mheshimiwa huyu anijulishe nimpangie mihadi ajionee alivyo mzima wa afya yupo nyumbani kwake mbezi beach akisubiria kuapishwa aingie mjengoni kuwatumikia wa Tanzania wenzake,Mungu mbariki mtumishi wako Deo Ntukamazina,Mungu ibariki Tanzania,JK mchapakazi muadilifu huyo wanangari wamekupa mtumie kadri uwezavyo, nasi tuko nanyi kwa maendeleo ya nchi tuachane na porojo, za wanafiki wafamaji.
Poleeeeeeeeeee kwa kuudanganya umma ndugu yangu naufahamu ukwel wa Ngara na Siasa zeke na ukwel wa Maisha ya Ntukamazina kwasababu ni mtu wa karibu sana na huyu mzee wetu
1. Mzee ana matatizo ya mgongo, fuvu la kichwa pia anatatizo la shingo. Kwa wale walioshiriki kwenye kampeni za kura za maoni watathibitisha hilo. Anavaa bandeji kiuononi na lilifunguka kipindi cha kura za maoni wagombea wenzake walimfunga kwani kiuno chake ni kibovu.
2. Huyu mzee sio muadilifu kivile ni mtu wa visasi sana na ni mbinafsi sanaaaaaaaaaa.
3. Ametumia fedha nyingi sana kipindi cha kampeni kwa kuwahonga wapiga kura waliokuwa kambi yake kipindi cha kura za maoni wanasema Mzee alitumia zaidi ya Milion 400 kupata ubunge.
4.Huko India alipelekwa na raisi Kikwete kwa kodi za Wananch kwa ajir ya matibabu.Rejea kampeni ya Raisi alivyokuwa Ngara mji mdogo wa Rulenge Kikwete alitamka kwa kinywa chake kua Serikali itampeleka India kwa ajir ya Matibabu
5. Huyu Mzee ni mgonjwa tena sana mpaka sasa yuko kitandani hali sio nzuri anatembelea magongo
6.Kampeni amefanyiwa na Mwenyekt wa Chama (W) Mke wa Ntukamazina, Mshindi wa pili wa Kura za Maoni na bwana mdogo anaitwa Bahati (Amepewa milion 10 kwa kufanya kazi hii)
8. Nikumabie ukwel huyu mzee hakubarik kabisaa ila sema si unajua tena wapiga kura wetu wana njaa kwa ajil ya pesa ndo maana amechaguliwa.
Siasa za Ngara sio kama unavyozania zimegawanyka sehem 2 za kikabira. Upande wa Ushubi na Ungaza. Upande wa Uangaza huyu mzee ndo hawataki hata kumuona hata ukingaria kura nyingi alizopata Sam Ruhuza (NCCR Mageuzi) zimetoka huko na huyu mzee kapata kura nyingi upande wa Uanga
Kuna kashfa nyingi zinazomuandama huyu mzee ikiwa matumizi mabaya ya ofisi na rushwa
Mwisho wanachi wa Ngara walichagua picha kwani ameonekana mala 2 tu siku za mwisho yani Ijumaa na Jumamosi kipindi cha kampeni zake.Ruhuza (NCCR) aliwaambia kuwa wananchi acheni kuchagua picha na mtu kilema aliyekitandani mda wote.
Tafadhari ndugu yangu Namaki acha kudanganya wana JF hapa