Elections 2010 Deogratias Ntukamazina, nuru mpya ya wana Ngara!!

ngara

Member
Nov 4, 2010
11
0
Napenda kuwapongeza wana Ngara kwa kutumia vizuri haki yao ya msingi kumchagua mzee wetu mpendwa ndugu Deogratias Ntukamazina. Tuna uhakika mzee huyu atatumika vizuri kuleta maendeleo ya Ngara na taifa kwa ujumla.

Mungu ibariki Tanzania.
 
Aminia huyu ni moja ya wazee ambao mi mwenyewe namjua ufanisi wake na uwezo wake kikazi.
tumwombee mungu asije akaungana tena na hao mafisadi.

TUNATAKA MTU ANAYEJUA SHIDA ZA MTANZANIA:
 
Dotto ni CCM, ni kweli ndugu mwana ukweli, lakini ninavyomfahamu mimi ni mtu anayelaani ufisadi na alikuwepo serikalini pia lakini hakujihusisha na ufisadi. Hivyo cha muhimu ni kumuombea asaidie kuleta maendeleo ya Ngara ili na wana Ngara waweze kufarahia matunda ya watoto wao kama wilaya nyingine zinavyofurahia.
 
Ndugu Dreamer, usikariri, angalia mtu binafsi usiangalie chama, je kina Mwakyembe si wako CCM au na wao unawaita mafisadi?
 
Jamani msikariri chagueni watu msichague Chama, je kina Mwakyembe ni mafisadi? si wako CCM, chagueni watu na wapimeni sio mnapima Chama
 
Ndugu Dreamer, usikariri, angalia mtu binafsi usiangalie chama, je kina Mwakyembe si wako CCM au na wao unawaita mafisadi?


Heshima kwako ngara,

Ni kweli wapo wanaCCM wapiganaji kama wanavyopenda kujiita umemtaja Mwakyembe na mimi naongeza Ole Sendeka,Anna kilango na nk.Mkuu wapiganaji ndani ya CCM hawana nguvu kama unavyodhani wanapigwa vita kweli mtaji wanoutegemea ni wananchi wa kawaida.Nitajie mpiganaji mmoja mwenye wadhifa wa naibu waziri,waziri au mkuu wa mkoa jibu ni hakuna chama cha mapinduzi hakiwataki.

Nina wasiwasi na Ntukamazima kama atakubali kufikishwa mahali alipofikishwa Lucas Seleli,Anna Kilango au Ole Sendeka.Kwa mujibu wa maelezo yako umesema Ntukamazima ni mzee mara nyingi wazee hawapendi purukushani.
 
hivi ndugu mwakyembe hawezi kuitwa mzee, au what is your definition ya mzee? naona ume misquote maana ya mzee, mimi nina maana mzee ni mtu mzima yeyote
 
Chama gani??

Kama ni mtu safi ambaye anapingana na mafisadi hata kama ni ssm anafaa tu kama vile ambavyo nimefurahia kina Anne Kilango, Mwakyembe, Sitta, Magufuli, Beatrice Shelukindo, na wale ambao unawafahamu kuwa walikuwa wachapazazi wa ssm kurudi jimboni.

 
hivi ndugu mwakyembe hawezi kuitwa mzee, au what is your definition ya mzee? naona ume misquote maana ya mzee, mimi nina maana mzee ni mtu mzima yeyote

Mkuu Ngara ebu tupe umri wa Ntukamazina.Hili jina nimeshawahi kulisikia mahali ila sikumbuki vizuri uzoefu wangu unaonyesha mara nyingi wastaafu serekalini [makatibu wakuu,makamishna,wakurugenzi] wanapenda kukimbilia mjengoni kuendeleza urasimu wao.
 
Napenda kuwapongeza wana Ngara kwa kutumia vizuri haki yao ya msingi kumchagua mzee wetu mpendwa ndugu Deogratias Ntukamazina. Tuna uhakika mzee huyu atatumika vizuri kuleta maendeleo ya Ngara na taifa kwa ujumla.

Mungu ibariki Tanzania.

Ebu jibu Ndiyo au Hapana kwa haya1.Ntukamazina hakuwahi kufanya kamepeini kwa kuwa aliugua kiharusi2.Kwenye mikutano yake ya kampeini CCM walikuwa wakitumia picha yake kumnadi3.Ametanagzwa mshindi kupitia CCM kwa kura nyingi.4.Mpaka sasa amelazwa nyumbani baada ya kutoka India kwenye matibabu.5.Ntukamazina hawezi kusimama,wala kutembea6.Hataweza kwenda bungeni kutokana na ugonjwa wa kiharusi unaomsumbua.7.Wana Ngara wamepata mbunge makini LAKINI hatawawakilisha BungeniMengine yatafuata baada ya kujibiwa hayo
 
Ebu jibu Ndiyo au Hapana kwa haya1.Ntukamazina hakuwahi kufanya kamepeini kwa kuwa aliugua kiharusi2.Kwenye mikutano yake ya kampeini CCM walikuwa wakitumia picha yake kumnadi3.Ametanagzwa mshindi kupitia CCM kwa kura nyingi.4.Mpaka sasa amelazwa nyumbani baada ya kutoka India kwenye matibabu.5.Ntukamazina hawezi kusimama,wala kutembea6.Hataweza kwenda bungeni kutokana na ugonjwa wa kiharusi unaomsumbua.7.Wana Ngara wamepata mbunge makini LAKINI hatawawakilisha BungeniMengine yatafuata baada ya kujibiwa hayo

Heshima kwako Rutunga M.

Sasa naanza kupata mwanga kwanini Tanzania ni nchi masikini sana dunia pamoja na kuwa na rasilimali kibao.Inawezekana mtu kuchaguliwa akiwa amelezwa hospital.Iko siku Tanzania itaweka rekodi ya kumchagua marehemu sitashangaa sana kila mara jambo jipya linaaza Tanzania.
 
kiongozi mzuri hata siku moja hatoki CCM, Kwanini? mana kiongozi yeyote akiwa ccm ataongoza kama ccm watakavomuagiza, kwa hiyo huyo jamaa ni fisadi tu kama alivo LOWASA,CHENGE,MRAMBA,MSABAHA,KIKWETE,MAKAMBA, KINANA
 
Ana asili ya Rwanda au Burundi? Amewaingiza serikalini watu wengi sana wa aina hiyo. Hawa ni kati ya wazee ambao wananalishusha hadhi Bunge letu kwa kulifanya sehemu ya kustafia wakati wengi wetu tunatarajia makubwa kutoka Bunge hili. Nadhani itungwe sheria kuwazuia wazee kama hawa ambao wamechoka kwenda kumalizia maisha yao Bungeni. Kuna kamtindo ka MAkatibu wakuu wastaafu, wakurugenzi wa Taasisi za UMMA wastaafu, wakuu wa vyombo vya DOLA wastaafu( Mboma, Tibaigana,......) kuingia CCM haraka wakishastafu halafu wanaibukia majimboni.
 
Ha haaa, we ndugu yangu Rutunga kweli story yako inaendana na jina lako ni ya kutunga! sasa nakuweka sawa,usisikie poroja za kihuni za wafama maji au wenye wivu wanaokaribia kujinyonga,Huyu jamaa (mbunge mteule) ni mwadilifu kupita maelezo, ni mchapa kazi wa kuigwa ,ana uzalendo kwa nchi hii na record yako inathibitisha hivyo,now what happened is siku chache kable cam[paign kuanza alipata ajali jumapili moja akitoa kanisani kumcha Mungu kama ilivyo desturi yake.ajali ilitokea pale mlalakuwa alikuwa akiendeshwa na mwanae mmoja wa kiume, alipata mshituko sehemu ya shingo kwa sababu alikuwa anasoma gazeti wakati ajali hiyo inatokea,mimi binafsi ni kati ya watu wa kwanza kabis kuifka eneo la ajali,ambayo haikuwa ya kutisha sana,tulimpeleka hopitali akapimwa akapewa matibabu na kuruhusiwa siku hiyo hiyo ya jumapili, lakini maumivu yalipomzidia alishauriana na familia yake na chama chake na kwa kuwa hana mzaha na afya yake aliamua kwenda India kupata matibabu ya uhakika ambako alikaa for ten days na kurudi ngangari kuwahi kuelekea Ngara kuendelea na kampeni ambako amewabwaga wapinzani kwa kishindo plus wabaya wake wote .sasa unaposema hatembei hasimami una maana watu wangara wote ni wapumbavu kumpeleka mjengoni mgonjwa? alifanya je kampeni majimbo yote 20 ya ngara na kumpatia ushindi wa kishindo JK wa 84%? wewe ungeijua jiografia ya ngara ilivyo iusingeandika upuuzi kama huo,kule lazima uwe ngagari kinoma, the weakest fell by the way!! anayetaka kumuona mheshimiwa huyu anijulishe nimpangie mihadi ajionee alivyo mzima wa afya yupo nyumbani kwake mbezi beach akisubiria kuapishwa aingie mjengoni kuwatumikia wa Tanzania wenzake,Mungu mbariki mtumishi wako Deo Ntukamazina,Mungu ibariki Tanzania,JK mchapakazi muadilifu huyo wanangari wamekupa mtumie kadri uwezavyo, nasi tuko nanyi kwa maendeleo ya nchi tuachane na porojo, za wanafiki wafamaji.
 
Ndugu Ngongo mbunge wetu Ngara aliwahi kuwa Katibu mkuu wa utumishi, Ndugu Rutanga aisee kweli wewe umenisikitisha sana hivi wewe pole kwa kuwa na chuki moyoni kiasi hiko kwa mbunge wetu, hivi hiko kiharusi ulimpa wewe? pleease hizo sala zako za kumuombea mbunge wetu zishindwe katika jina la YESU mbunge wetu haumi ni mzima na nakuomba usikose kukodolea macho wabunge watakapokuwa wanaapishwa huko Dodoma ili uweze kumuona mbunge wetu wa Ngara na nitaleta picha huku akiwa anaapishwa ili uzomewe na uongo wako wa duu!! duniani kuna mambo!!
 
Back
Top Bottom