dosama
JF-Expert Member
- Dec 25, 2010
- 912
- 957
Ni mchango wake bungeni
Mh.Deo Filikunjombe baada ya kuchangia mjadala wa bajeti hajaonyesha kuunga mkono hoja na badala yake "indirect "kupinga bajeti ameituhumu serikali kwa kutoweza kutimiza ahadi zake kwa wananchi.
Kasisitiza kuandaa bajeti inayotekelezeka kwasababu bajeti zilizopita zinaisuta serikali leo kwa kutotekelezwa. Mikopo haionyeshi impact kwa lolote hapa Tanzania na Raisi Kikwete amekuwa akienda nje kuomba misaada na hali serikali si makini katika kusimamia matumizi ya fedha.
Inatakiwa ifike kupindi Kikwete aambiwe sasa baki ndani ya nchi tutumie hiki kidogo tulichonacho. Haya ni maneno ya Deo Fnjombe.
Mbunge wa Ludewa, Deo Haule Filikunjombe awe mfano wa kuigwa na wabunge wa CCM, kwa kutokuunga mkono hoja ya bajeti na ameonyesha kuthubutu na kukomaa kisiasa.. Kwa kuionya serikali kwamba imezidi kutumia hela nyingi na kukosa nidhamu ya fedha na kufuja rasilimali tulizo nazo..
Na amesema kuwa deni la taifa limeongezeka kutoka tirilion 5, 14 mpaka 22tsh..na kuwa ukali na ugum wa maisha umeongezeka kwa watanzania nchini kote na kuwa hii bajeti imeondoa matumaini ya watanzania kuiamini serikali kwa sehem kubwa.. Na kuwa mipango na fedha huwa zinatolewa na hazifikishi maeneo husika kwa muda muafaka na kama zitafika ..fedha hizo zitafika chache.. Ambapo ametoa mfano jimboni kwake ludewa kuwa kuna fedha nyingi za miradi na shughuli za maendeleo..
Ziliahidiwa kupelekwa na serikali pale bungeni mwaka jana lakini hazijafika mpaka leo.. Na zilizofika ni chache.. Hivyo ameionya serikali na kuwakanya baadhi ya watumishi wasio na nidham ya fedha..
Source: bunge live on tbc1
My take:
Namuunga mkono na anapaswa kuwa mfano wa kuigwa kwa kusema ukweli kuwa serikali na viongozi kwa ujumla waongo..kwa kuwa utekelezaji wa ahadi mipango ya maendeleo ni DUNI..!