Deo Filikunjombe: Mbunge anayefanya makubwa jimboni mwake

Mbona wabunge wengi tu wa CDM wamefanya hivyo lakini hawajajitangaza. Amefuata nyayo za CMD lakini hata hivyo bado anahali ngumu jimboni kwake.
 
Du kumbe kwa muda mfupi namna hii posho kwa mbunge mmoja yaweza kuwa zaidi ya tsh. milioni 90!, kweli kuna haja ya posho kufutwa
 
Kama rushwa ndio hivi, basi sioni tatizo lake, maana kila jimbo lingekuwa na ambulance, au visima vya maji.
Milioni tisini ni madawati mangapi? Solar panels ngapi?

Naunga mkono hoja.

Tunahitaji rushwa nyingi zaidi za aina hii ili kupunguza idadi ya Wamama Wajawazito wanaohatarishiwa maisha yao kutokana na kuwa mbali na vituo vya afya, tunahitaji rushwa ya namna hii ili kupunguza idadi ya wanaokufa kwa kuchelewa kupata matibabu.

Hivyo kama Wabunge wote wangetumia zile Million 90 kutoa rushwa za mtindo huu, naamini tungekuwa tumepiga hatua kubwa sana kukabiliana na tatizo hili, Deo endelea kutoa rushwa za namna hii...
 
Nampongeza filikunjombe ila maoni yangu ni hapo kwenye kanisani ivi angekuwa ni mbunge wa chadema ingekuwaje?wanasiasa upenda sana kutumia siasa ya udini kama mtaji wao wa kisiasa,CCM wasifanye ivo kila mtu ana uhuru wa kuabudu.
 
Sina ugomvi na yeye kukabidhi gari ila ugomvi wangu ni pale viongozi wetu wanapotumia misaada ikakwa ajili ya faida za kisiasa?...kama gari ni kwa ajili ya matumizi ya hospitali ya wilaya kwann asingemkabidhi mkuu wa wilaya au daktari wa wilaya??

.....kazi ya mbunge sidhani kama ndo hii, anatakiwa kuzunguka huko na huko kumobilize wadau wa kiuchumi na kusimamia vema matumizi ya hela za halmashauri, ila kwa staili hii ya kutumia hela zao kutoa misaaada sidhani kama tutafika
 
Sina ugomvi na yeye kukabidhi gari ila ugomvi wangu ni pale viongozi wetu wanapotumia misaada ikakwa ajili ya faida za kisiasa?...kama gari ni kwa ajili ya matumizi ya hospitali ya wilaya kwann asingemkabidhi mkuu wa wilaya au daktari wa wilaya??

.....kazi ya mbunge sidhani kama ndo hii, anatakiwa kuzunguka huko na huko kumobilize wadau wa kiuchumi na kusimamia vema matumizi ya hela za halmashauri, ila kwa staili hii ya kutumia hela zao kutoa misaaada sidhani kama tutafika
Pamoja na majukumu yoote ya Kibunge anayopaswa kuyafanya, tukumbuke pia kuwa alipewa Tsh. Million 90 za walipa kodi kwa ajili ya matumizi yake binafsi, kama Regia Mtema alivyowahi kukiri kuwa hiyo ni pesa ndoogo sana isiyotosha ata kwa matumizi ya wiki mbili.

Sasa kwa Deo kujinyima hicho kidogo, na kuamua kuwanunulia wapiga kura wake ambulance kuna tatizo gani? faida zozote za kisiasa zinazosaidia kuokoa maisha ya watu maskini zinapaswa ziungwe mkono...
 
Kna sehemu umemfananisha Deo na Godbless lema kuwa wanafanya vitu vya maendeleo. Mkuu nilikua naomba nijue mambo ambayo mhe.mbunge wa Arusha, amefanikiwa kuyafanya mpk mwez huu wa kumi? Nawasilisha.
 
Nilikutana naye maeneo ya mwenge pale anabandika sticker hiyo hice natumaini atakumbuka mambo tuliyoöngea.
Hongera sana Deo.
 
Hii nchi tutaendelea kuwa masikini mpaka tutakapojuwa mipaka ya kimajukumu

Sasa kama mbunge ananunua ambulance hii maana yake ni kuwaambia wananchi "nimeshindwa kuisimamia serikali" sasa inabidi posho zangu ndio niwanunulie nyie............sasa mbunge kama huyu wa nini

Hii ni hulka mbaya ambayo imekaa kwa wanasiasa wote na inabidi tufike mahali wananchi tuwasaidie kufahamu tunataka wabunge wakuisimamia serikali na mambo ya kuletea ambulance iwe ni serikali (labda atoe kama mtu binafsi na sio kama mbunge kisha aje kutuambia kanunua ambulance kama mafanikio).

Lets not think ndani ya box
 
Tanzania tunahulka ya kuchagua chama na rangi yake bila kuangalia uwezo wa mtu. Mbunge kijana Deo Filikunjombe Haule wa Ludewa anafanya makubwa jimboni mwake na hivyo kuwafunika wabunge wote waliomtangulia na wamekiri hivyo. Hayo ndiyo maendeleo tunayotaka kama alivyofanya Godbless Lema wa Arusha. Kama posho wanazolilia wabunge zingekuwa zinafanya kazi kama hiyo ingeeleweka.



DSCF7201.JPG

Hata hivyo Mbunge huyo amesema kuwa ,katika kulipa fidia kwa wananchi wake amelazimika kuzitumia kiasi cha shilingi milioni 90 alizopata bungeni kununua gari ya wagonjwa katika jimbo hilo.

Alisema kuwa hadi sasa amepata kukabidhi gari la wagonnjwa katika kata ya manda ,Rupingu na sasa katikata ya Mlangali ambako pia rais Jakaya Kikwete amepata kuahidi gari katika kata hiyo ya Mlangali .

Filikujombe alisema kuwa Rais Kikwete alipata kuahidi gari katika kata hiyo na kuwa iwapo itafika gari hilo la Rais basi wao wataangalia matumizi ya gari hii ya sasa.

Kweli you guys you are great thinkers. Kuna milioni 90 kwenye hiyo Hiace chakavu hapo kweli?? Kama mdau ninayehusika na biashara ya magari, mapya na used hilo hapo si gari. What I just see is Tetanus hapo.
NB: Hebu wadau mliopo huko ludewa rusheni registration number ya huo mkangafu tuwape actual cost zake mara moja.
 
Kwanza kabisa lazma ujue kuwa rushwa ni adui wa haki na haijawahi kuwa nzuri kwa jamii yoyote ile isipokuwa mtoaji na mpokeaji rushwa. Pili naona kunadhana potofu ambayo imejengenga kuwa mbunge ni mfadhili. Hii si sawa kabisa. Mbunge makini ni yule anayefundisha watu wake namna ya kujikwamua kiuchumi na kuhamasisha maendeleo ya jamii yake etc. Tanzania haitaki mbunge anayewapa watu samaki e.g kugawa mahindi, bali anayewafundisha watu kuvua e.g kufundisha kanuni za kilimo bora/kuwapa elimu ya biashara ili wawe na maendeleo endelevu na sio maendeleo yanayomtegemea fulani, hivyo huyo fulani asipokuwepo basi hakuna maendeleo. So afanyecho Filikunjombe so far anajitahid ila aende beyond ili maendeleo ya wana Ludewa yawe endelevu na sio yategemee uwepo wa Filikunjombe ie. kugawiwa magari, kutoa sadaka kubwa, kulisha makutano wengi, etc
Mbunge ananufaika na wanajimbo wananufaika. hii ikifanywa majimbo yote tanzania itakuwa ahueni.Kuhusu kilimo na afya bora,nadhani wengi wanajua ila tatizo ni fedha.Hata wilaya yao ikiwa na madini, wachina ndio wanafaidi, amelalamikia makaa ya mawe angalau.... hao wengine wanakariri vifungu vya vkanuni za bunge na kulamba posho.
 
Hii nchi tutaendelea kuwa masikini mpaka tutakapojuwa mipaka ya kimajukumu

Sasa kama mbunge ananunua ambulance hii maana yake ni kuwaambia wananchi "nimeshindwa kuisimamia serikali" sasa inabidi posho zangu ndio niwanunulie nyie............sasa mbunge kama huyu wa nini

Hii ni hulka mbaya ambayo imekaa kwa wanasiasa wote na inabidi tufike mahali wananchi tuwasaidie kufahamu tunataka wabunge wakuisimamia serikali na mambo ya kuletea ambulance iwe ni serikali (labda atoe kama mtu binafsi na sio kama mbunge kisha aje kutuambia kanunua ambulance kama mafanikio).

Lets not think ndani ya box
Kodi yote ya tanzania haiwezi hata kulipa mishahara ya watumishi. Wameomba ambulance wakaletewa bajaji kila wilaya. Watanzania hatuko productive na hatuko innovative, tunaishi kwa misaada ya wafadhili.
Watanzania wachache sana wanafanya kazi masaa 12 mpaka 16 kwa siku. Wachache sana wana kazi mbili, halafu tunapiga kelele huku tunakunywa ulabu.
 
Watanzania thamani yetu ni ndogo sana. Kagari ka wagonjwa. Iwe ni mbunge wa CCM au chama kingine chochote, si kazi yake kununuwa gari la wagonjwa na kutangaza, ili iweje?

Rushwa ni za aina nyingi sana, hii ni mojawapo.

Nilitegemea wabunge wasimamie mambo mazito ya kubadilisha maisha ya watu.

Dah,yaani nilikua nadhani na wewe una akili.Kumbe hakuna kitu.Sasa,hili la mbunga kufanya jambo la maana kama hili unaliona sio ishu.Yaani CCM Wengine bana,ahaaa au ndo ile staili ya wabunge wa ccm kupiga makofi tuuuuuuuuuu
 
Mzee, hii ni siasa siyo kazi ya kitume..lazima atangaze ijulikane kuwa kafanya ili apate support ya watu.
1. Majukumu ya mbunge ni yapi?
2. Kuna umuhimu gani wa kujitangaza anapotoa msaada?. Hilo gari ni msaada, wala sio sehemu ya majukumu yake.
Hii nayo ni Rushwa!
 
hongera sana mbunge kwa msaada uliotoa kwa wana jimbo lako! lakini kulikuwa hakuna haja ya kusema gharama za hiyo gari. sipendi tabia ya mtu kusaidia na kusema nimetumia kiasi hichi cha pesa, saidia na anza inatosha.
 
Watanzania thamani yetu ni ndogo sana. Kagari ka wagonjwa. Iwe ni mbunge wa CCM au chama kingine chochote, si kazi yake kununuwa gari la wagonjwa na kutangaza, ili iweje?

Rushwa ni za aina nyingi sana, hii ni mojawapo.

Nilitegemea wabunge wasimamie mambo mazito ya kubadilisha maisha ya watu.

Nilisema huko nyuma kwamba elimu ya uraia inahitajika sana nchi hii na inatakiwa ianze humu JF. Yaani mbunge kutekeleza majukumu aliyoomba kuyafanya kwa miaka mitano na ambayo ndiyo yanampa mshahara na marupurupu kutoka katika hazina ya nchi ndoa aonekane ameota msaada au amefanya kitu cha ajabu? Sasa majukumu ya kawaida ya mbunge ni nini? Kagari kenyewe ni ka milioni 10 - 12, halafu mnadai katumia milioni 90 za mkopo wake! Huu ni upotoshaji. Haya na huyo Lema kafanya nini?
 
Mhhhhhhhhhhhhh! Mbona hii gari aliitoa kabla ya uchaguzi wa mwaka jana mkuu. Au ndo propaganda? Acha uzushi mkuu, huyu mswis namjua kaka tangu pale kasita. Alituharibia CDM kwa kumtuma mamluki kuchukua fomu ya kugombea ubunge kwa tiketi ya CDM ili apite bila kupingwa.

Wakuu hili gari lilitolewa kabla ya uchaguzi wa 2015, hapa jamaa anajaribu kumpigia debe kwa ajili ya uchaguzi wa 2015.
 
Kwa nini wanaume wa maeneo anayaotoka Deo huwa hawatahiriwi? Pale kasita ilikuwa huwezi kuoga na jamaa bathroom moja na akifanya hivyo basi lazima aoge na chupi!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom