Denis Urio, msiri wa Kingai, kwanini hajaletwa kizimbani wakati yeye ndiye source ya kesi ya Ugaidi?

K
Kingai atajuta kuanzisha kesi za kishamba kama hizi hata kama kapewa ahadi na ccm ya kuwa igp ajae,hii kesi ni ya kubumba KILA Mtza anajua hilo.
Kingai ana umri gani?
Ili uwe RPC nivigezo gani huzingatiwa?
Nani huwa anawateua Ma RPC?
 
K

Kingai ana umri gani?
Ili uwe RPC nivigezo gani huzingatiwa?
Nani huwa anawateua Ma RPC?
Uwezo wako binafsi tu wa kuwashughulikia wapinzani na kuipa ccm ushindi ni cv tosha, mengine ni chachandu tu
 
Huyu mtu wa ndani wa CDM anaye tajwa kama shahidi wa jamhuri ni nani??
 
Acha uongo lijenje yupo mtaani na mahakama imeshaambiwa

USSR
Mtaani tena?Mtuhumiwa wa ugaidi anaachwa mtaani azurure wakati ndo miongoni mwa waliokuwa wakitafutwa.
 
Utetezi wasifunge sehemu yao ya ushahidi hadi pamoja na mambo mengine, Dennis Urio aletwe mahakamani.
Mtetezi wa mbowe gaidi, dalali wa chanjo.yote umejuvisha ww......sikupendi ww basi tu.Nakuchukia sana tangu kipindi unadalalia chanjo.sijui ulikula milioni ngapi!!
 
Kwa taarifa za uhakika Denis urio yupo Sudan eneo la Darfur kama peacekeeper

USSR
Uko uko alipopelekwa kimkakati maana yeye ndiyo aliyepanga jinsi ya kutengeneza ugaidi feki kwa kutumwa atapata malipo yake. Peacekeeper gani mshenzi Kama huyo.
 
Kingai ndio alikuwa kiongozi wa lile kundi la Magufuli la watu wasiojulikana. Kundi hili ndio liliondesha unyama kwa wote waliokuwa wapingaji wa utawala wa Magufuli.

Wasiojulikana wamejulikana kabisaaa
 
Kingai ndio alikuwa kiongozi wa lile kundi la Magufuli la watu wasiojulikana. Kundi hili ndio liliondesha unyama kwa wote waliokuwa wapingaji wa utawala wa Magufuli.
Mzee hii ni kama inaukweli kaka
 
Na ukweli huu ulikuwa unaleta maswali mengi kuhusu ukaribu wa Cardinal Pengo na huyu mtu ambaye kwa kipimo chochote, uovu wake ulikuwa wa kutiaha.

Au ukaribu wa Pengo kwa Magufuli ilikuwa ni kutii lile andiko lisemalo tabibu hayupo kwaajili ya wazima, bali wagonjwa? Uharamia wa marehemu ulivuka utu wa kawaida wa mwanadamu mwenye Roho wa Mungu.
Lakini "utabibu"wa tabibu na mgonjwa wake una mipaka yake tofauti kabisa na mahusiano aliyokuwa nayo Pengo na huyo mtu. Hawa viongozi wengi wa dini wamejiharibia sana sifa zao na dini zao kwa mahusiano ya namna hii.
 
Wakuu, story ya kesi ya Ugaidi, kama jinsi ilivyoelekezwa na Bwana Kingai, chanzo chake ni msiri wa Kingai ambaye ni Denis Urio!

Hii case ya ugaidi, kwa 100% inamuhusu sana huyu Denis Urio, ambapo Bwana Kingai alisema alipata taarifa hizo kutoka kwake!

Cha kushangaza, mpaka sasa mashahidi wa Jamuhuri wanatumia neno "Msiri" huku wakijisahaulisha kuwa mwanzoni mwa case hii Bwana Kingai alieleza information zote zilitoka kwa Denis Urio.

Pamoja na hayo, ulimwengu unastaajabu kuwa source wa hayo mambo (Denis Urio), anatajwa juu juu tu Mahakamani huku hakuna dalili ya kuitwa kwake kuja kutoa confirmation kuwa info alizitoa yeye, na yeye aliambiwa na watu gani?

Upande wa jamhuri wamepozi as if sio muhusika kabisaa kwenye kesi hii, na kubadili lugha eti msiri wa Kingai!

Nashauri wakili wa utetezi kuiomba mahakama ilazimishe kuletwa kwa huyu Denis Urio ili tujue mbivu na mbichi!
Hii kesi inazua maswali mengi sana. Watuhumiwa wanadai hawakufikishwa Police Central Dar es Salaam, bali Kituo cha Polisi Tazara na kisha kupelekwa Mbweni. Mashahidi wa Jamhuri wanadai walifikishwa Police Central Dar es Salaam na kisha kupelekwa Mbweni. Nani anayesema ukweli?
 
ninachoshangaa mimi taarifa amewapa yeye ya kuwapa kazi hao akina Adamoo,Sasa tena uyouyo Urio anakuja kukamatwa na kupewa kipigo kama watuhumiwa walivyokamatwa,Inakuwaje hapo
Mkuu hujui kama kulikuwa na Mambo ya udukuzi chini ya yule Msepazake.
Nazani Simu zote za kupiga na kupokea za Mbowe zilikuwa zikifuatiliwa kujua majadiliano. Ndio yakaja huko yalipo fikia Sasa..
 
Back
Top Bottom