Deni la Taifa laongezeka kwa asilimia 7.6 ndani ya mwaka. Chanzo ni ukopaji wa fedha kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,500
9,279
DENI la Taifa limefikia Sh. trilioni 59 hadi kufikia Disemba mwaka jana, ikilinganishwa na Sh. trilioni 54.8 kwa kipindi kama hicho mwaka 2019, sawa na ongezeko la asilimia 7.6, huku Bunge likitoa ushauri liwe himilivu.

Kati ya kiasi hicho, deni la ndani limefikia Sh. trilioni 16.2 na deni la nje Sh. trilioni 42.8. Ongezeko la deni limetokana na ukopaji kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo.

Pamoja na kwamba deni hilo ni himilivu kwa viashiria vyote muhimu, serikali imeshauriwa ione haja ya kujipima uhimilivu wake, kwa kutumia kiashiria cha makusanyo ya mapato ya ndani, kwa pato la Taifa ambacho kwenye mpango hakijaripotiwa.

Hayo yalibainishwa na Sillo Baran, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti, alipokuwa akiwasilisha taarifa kuhusu tathmini ya utekelezaji wa mpango wa maendeleo wa miaka mitano (2016/17-2020/21), mapendekezo ya Mpango wa tatu wa Maendeleo wa Taifa wa miaka mitano (2021/22-2025/26) na Mwongozo wa maandalizi ya Mpango na bajeti ya serikali na mpango wa maendeleo wa taifa kwa mwaka wa fedha 2021/22, na kusema wanashauri hilo kwa sababu deni la taifa uhudumiwa na makusanyo ya ndani na ni malipo ya lazima katika matumizi ya serikali.

“Vilevile kamati inaishauri serikali kukamilisha haraka mchakato wa nchi yetu kufanyiwa credit rating (kiwango cha mkopo) ili kuiwezesha serikali kupata mikopo nafuu na kwa urahisi,” alisema mwenyekiti huyo.

Alisema Bunge kwamba kwa mujibu wa tathmini ya uhimilivu wa deni iliyofanywa Disemba 2020, deni, ni himilivu kwa vigezo vyote vya kimataifa na hivyo, nchi ina uwezo wa kukopa ndani na nje, na kulipa mikopo hiyo bila kuwa na athari hasi kwenye ukuaji wa uchumi.

Katika maoni ya jumla ya kamati hiyo ya bajeti, serikali imeshauriwa kutafuta njia ya kupunguza kukopa katika soko la fedha la ndani ili kuziba nakisi ya bajeti kwa kupitia dhamana ya serikali na hati fungani.

Badala yake, serikali ijikite zaidi katika kuongeza udhamini wa wakopaji wadogo (credit gurantee schemes) pamoja na kuongeza matumizi ya mikopo inayojidhamini yenyewe (lease finance).

Vilevile, serikali iangalie uwezekano wa kufungua zaidi soko la mitaji (liberization of capital market) ili kupunguza athari za serikali kukopa kwenye soko la ndani.

Chanzo: Nipashe
 
Miradi yote ya kimkakati inaendeshwa kwa pesa zetu wenyewe
Sio Mitano tena ni milele kabisa.
Uchumi wa kati.
Nchi hii ni tajiri sana hatuhitaji pesa za mabeberu.

Au nasema uongo ndugu zanguuuuu.

Unaijua vieite wewe!!!!
Sisi tunatembelea mavieitee!!!!
IMG_20210127_125033.jpg
 
Kitu kinachotia shaka kwenye hii chanjo ya covid-19 ni kwamba hata mara baada ya kupatiwa chanjo mtu hulazimika bado kujilinda kwa barakoa na taratibu zote kama zile zilizopaswa kutumika kabla chanjo haijatengenezwa sasa hapa chanjo inaumaana gani?

Je, chanjo hii ambayo mara nyingi huwa ni aina virus itakapofail nini kitatokea?kwa vyovyote wadudu watakuwa sugu zaidi may be 10 times hivyo RAIS wetu anaposema tusiwe na haraka juu ya chanjo hizi tumuelewe>

Chanjo zozote duniani zilipita stage mbali mbali ya kwanza ni watu wa kuwajaribia chanjo husika pili kuipa chanjo hiyo muda kuona jinsi gani ina fanya kazi [it should take even 3-5 years] baada ya hapo ndipo chanjo hiyo huthibitishwa rasmi na mamlaka husika za kimataifa zenye wajumbe labstechs toka nchi mbali mbali.

Nampa heko mkemia magufuli lets wait no hurry acha wengine wajaribiwe kwanza
 
Back
Top Bottom