Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,371
- 39,186
Habari Leo
Serikali hadi sasa imekwisha kutoa udhamini kwa mashirika mbalimbali wenye thamani wa zaidi ya Sh bilioni 350, imeelezwa.Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremiah Sumari alikuwa akimjibu Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa (Chadema), aliyeuliza athari za udhamini huo kwa serikali ambao umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka.
Mashirika hayo na fedha ambazo serikali imeyadhamini katika mabano ni Shirika la Umeme Tanznaia (Tanesco) Sh 139,314,978,184, ATC Ltd (Sh bilioni 72) na Shirika la magari la Taifa (SMC) (Sh 2,898,840,716).Mengine ni Mamlaka ya Mkonge Tanzania (TSA) Sh 1,024,933,969, Shirika la Uchumi la CCM SUKITA ambalo limekwisha kufilisika na liko chini ya mfilisi (Sh 10,139,494,513) na Chama cha Ushirika Mara (Sh 8,502,977,181).
Naibu Waziri aliyataja mashirika mengine kuwa Kiwanda cha Nguo Urafiki (Sh 25,781,394,288.75), Kampuni ya General Tyre East Africa (Sh 12,530,800,000) na Chama cha Ushirika Nyanza (Sh 1,370,509,071.27).Alisema serikali inayo Kamati ya taifa ya Madeni kwa mujibu wa Sheria ya Mikopo, Dhamana na Misaada ya Serikali ya mwaka 1974 iliyorekebishwa mwaka 2004.
Wajumbe wa kamati hiyo ni makatibu wakuu wa wizara mbalimbali, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na Mhasibu Mkuu wa Serikali.Kazi kubwa ya kamati hii ni kutathmini kwa kina shirika au kampuni inayoomba udhamini wa serikali na hatimaye kumshauri Waziri wa Fedha na Uchumi ipasavyo, alisema.
Alisema athari za udhamini ni wakati shirika au kampuni inaposhindwa kulipa deni lililotokana na dhamama iliyotolewa ni kwa serikali kutakiwa kulilipa deni husika. Akijibu swali la nyongeza la Dk. Slaa, alisema ufutaji wa deni lililodhaminiwa na serikali una utaratibu na hufanywa inapoonekana ni busara.
Alitoa maelezo hayo baada ya Mbunge huyo kutaka deni la Tanesco lililodhaminiwa na serikali la zaidi ya Sh bilioni 139 lifutwe ili kusaidia shirika hilo lipunguze gharama za umeme kwa watumiaji.Dk. Slaa pia alitaka watu wanaohusika na deni la Sukita lililotokana na ununuzi wa pombe kali na matairi katika miaka ya 1985 hadi 1990 na ambao alisema wanajulikana washitakiwe.
My Take:
Mimi nilidhani kuwa serikali inadhamini mashirika ambayo ina hisa TU. Kama wameweza kutoa udhamini wa bilioni 10 kwa Sukita kweli wameshindwa kutoa udhamini kiduchu kwa THI ili iweze kupata misaada inayohitaji na kuweza kujikita na kuwa taasisi?
Serikali hadi sasa imekwisha kutoa udhamini kwa mashirika mbalimbali wenye thamani wa zaidi ya Sh bilioni 350, imeelezwa.Naibu Waziri wa Fedha na Uchumi, Jeremiah Sumari alikuwa akimjibu Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa (Chadema), aliyeuliza athari za udhamini huo kwa serikali ambao umekuwa ukiongezeka mwaka hadi mwaka.
Mashirika hayo na fedha ambazo serikali imeyadhamini katika mabano ni Shirika la Umeme Tanznaia (Tanesco) Sh 139,314,978,184, ATC Ltd (Sh bilioni 72) na Shirika la magari la Taifa (SMC) (Sh 2,898,840,716).Mengine ni Mamlaka ya Mkonge Tanzania (TSA) Sh 1,024,933,969, Shirika la Uchumi la CCM SUKITA ambalo limekwisha kufilisika na liko chini ya mfilisi (Sh 10,139,494,513) na Chama cha Ushirika Mara (Sh 8,502,977,181).
Naibu Waziri aliyataja mashirika mengine kuwa Kiwanda cha Nguo Urafiki (Sh 25,781,394,288.75), Kampuni ya General Tyre East Africa (Sh 12,530,800,000) na Chama cha Ushirika Nyanza (Sh 1,370,509,071.27).Alisema serikali inayo Kamati ya taifa ya Madeni kwa mujibu wa Sheria ya Mikopo, Dhamana na Misaada ya Serikali ya mwaka 1974 iliyorekebishwa mwaka 2004.
Wajumbe wa kamati hiyo ni makatibu wakuu wa wizara mbalimbali, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na Mhasibu Mkuu wa Serikali.Kazi kubwa ya kamati hii ni kutathmini kwa kina shirika au kampuni inayoomba udhamini wa serikali na hatimaye kumshauri Waziri wa Fedha na Uchumi ipasavyo, alisema.
Alisema athari za udhamini ni wakati shirika au kampuni inaposhindwa kulipa deni lililotokana na dhamama iliyotolewa ni kwa serikali kutakiwa kulilipa deni husika. Akijibu swali la nyongeza la Dk. Slaa, alisema ufutaji wa deni lililodhaminiwa na serikali una utaratibu na hufanywa inapoonekana ni busara.
Alitoa maelezo hayo baada ya Mbunge huyo kutaka deni la Tanesco lililodhaminiwa na serikali la zaidi ya Sh bilioni 139 lifutwe ili kusaidia shirika hilo lipunguze gharama za umeme kwa watumiaji.Dk. Slaa pia alitaka watu wanaohusika na deni la Sukita lililotokana na ununuzi wa pombe kali na matairi katika miaka ya 1985 hadi 1990 na ambao alisema wanajulikana washitakiwe.
My Take:
Mimi nilidhani kuwa serikali inadhamini mashirika ambayo ina hisa TU. Kama wameweza kutoa udhamini wa bilioni 10 kwa Sukita kweli wameshindwa kutoa udhamini kiduchu kwa THI ili iweze kupata misaada inayohitaji na kuweza kujikita na kuwa taasisi?