Alwaz
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,099
- 10,794
Ikiwa hali ndizo hizi,chaguzi za nini?.
Hivi tunavyoandika chaguzi zenye mizozo ziko Haiti,Misri na Ivory Coast.
Unajua haya mambo ya uchaguzi yana gharama mno,kuanzia mali mpaka muda na afya.
Ikiwa kila siku tunaingia gharama hizo mwishowe matokeo huamuliwa mezani.Ni afadhali tutafute utaratibu mwengine wa kupata viongozi.
Utaratibu ninaopendelea mimi ni:
1. Kuwepo tume maalum inayopokea maoni ya raia na kuyaweka kwenye mtandao kila siku.Raia watasema mtu anayefaa kuongoza baada ya miaka mitano ni fulani na sifa zake ni hizi......Raia wakileta kasoro za mtu huyo tume ambayo itakuwa chini ya taasisi ya bunge itakuwa na taratibu za kufuatilia na hatimaye kuja na jawabu ambayo inaweza kukatiwa rufaa na raia au mhusika mwenyewe ili kusafisha heshima yake.
2.Kiongozi aliyeko madarakani kwa utaratibu huu,iwapo raia wataendelea kuridhika naye hakutokuwa na ukomo wa uongozi.
3.Demokrasia hii ambayo inaweza kuitwa Ami's Democracy (ADE) itakuwa Iko kati na kati baina ya ufalme na demokrasia ya nchi za magharibi inayotesa sasa hivi.
Faida ya ADE ni kuwa gharama za kuendesha nchi zitakuwa chini sana.Fedha na muda vitatumika kwenye mambo ya mendeleo kiuhalisia.
Hasara ya utaratibu wa sasa kwanza ni fedha zinatumika nyingi kwa vipindi vifupi vifupi.Wanaofaidika ni waasisi wa demokrasia kwa kuuza karatasi,wino,masanduku na kadhalika.Raia wa nchi nyingi wanagombana pasi na ulazima.Wanapoteza muda na afya zao bure
Kauli mbiu ya demokrasia yangu ni UCHAGUZI DAIMA!.
Hivi tunavyoandika chaguzi zenye mizozo ziko Haiti,Misri na Ivory Coast.
Unajua haya mambo ya uchaguzi yana gharama mno,kuanzia mali mpaka muda na afya.
Ikiwa kila siku tunaingia gharama hizo mwishowe matokeo huamuliwa mezani.Ni afadhali tutafute utaratibu mwengine wa kupata viongozi.
Utaratibu ninaopendelea mimi ni:
1. Kuwepo tume maalum inayopokea maoni ya raia na kuyaweka kwenye mtandao kila siku.Raia watasema mtu anayefaa kuongoza baada ya miaka mitano ni fulani na sifa zake ni hizi......Raia wakileta kasoro za mtu huyo tume ambayo itakuwa chini ya taasisi ya bunge itakuwa na taratibu za kufuatilia na hatimaye kuja na jawabu ambayo inaweza kukatiwa rufaa na raia au mhusika mwenyewe ili kusafisha heshima yake.
2.Kiongozi aliyeko madarakani kwa utaratibu huu,iwapo raia wataendelea kuridhika naye hakutokuwa na ukomo wa uongozi.
3.Demokrasia hii ambayo inaweza kuitwa Ami's Democracy (ADE) itakuwa Iko kati na kati baina ya ufalme na demokrasia ya nchi za magharibi inayotesa sasa hivi.
Faida ya ADE ni kuwa gharama za kuendesha nchi zitakuwa chini sana.Fedha na muda vitatumika kwenye mambo ya mendeleo kiuhalisia.
Hasara ya utaratibu wa sasa kwanza ni fedha zinatumika nyingi kwa vipindi vifupi vifupi.Wanaofaidika ni waasisi wa demokrasia kwa kuuza karatasi,wino,masanduku na kadhalika.Raia wa nchi nyingi wanagombana pasi na ulazima.Wanapoteza muda na afya zao bure
Kauli mbiu ya demokrasia yangu ni UCHAGUZI DAIMA!.