Demokrasia ya Afrika matatani kufuatia Mapinduzi ya Katiba

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
IMG_20210330_175343_707.jpg

Demokrasia katika nchi nyingi za Afrika imekuwa ikilegalega kutokana na Sheria ambazo Bunge linatakiwa kumtii Rais hali inayopelekea Marais kutengua Katiba na kujiongezea muda wa kukaa madarakani.

Suala hilo la kubadilisha Katiba kwa kuondoa ukomo wa muda au umri wa Urais linafahamika kama Mapinduzi ya Katiba (Constitutional coup) na ni maarufu sana kwenye nchi za Afrika huku likiwa kikwazo kikubwa cha Demokrasia.

Marais ambao wamebadilisha Katiba za nchi zao kuondoa kikomo cha mihula miwili baadhi yao ni pamoja na Gnassingbé (Togo), Museveni (Uganda), Déby (Chad), Biya (Cameroon), Kagame (Rwanda), Hayati Nkurunziza (Burundi), el-Sisi (Misri) na Sassou (Brazavelle).
 
Kama wananchi inafikia kusema mtu fulani ni mungu kwanini wasijawe na kiburi cha majivuno ya kubadili katiba?
 
Mambo yameanza ili wapigaji waingie kati...

Kaangalia mataifa ya Russia,N.Korea,China....etc etc + nguvu zao za kiuchumi zilivyo imara + nguvu za Kitaifa

Siku zote akipatikana mtu sahihi ni muhimu aendeleze Gurudumu ili Taifa lisonge..


Mstaafu Mwinyi aliwahi kusema Katiba sio Msaafu.


Yote kwa yote lakini sio kwa umuhimu niwapongeza watu wa Urusi kwa kumuongezea muda mrefu zaidi Raisi Putin
 
Back
Top Bottom