Raia Fulani
JF-Expert Member
- Mar 12, 2009
- 10,771
- 2,544
Tunapokizungumzia Chadema tunazungumzia mambo mawili makuu; Demokrasia na Maendeleo. Ni imani yangu kuwa waasisi wa chama hawakukurupuka katika kutafuta hayo maneno mawili ili yawe mwongozo katika kile viongozi, wanachama na wananchi kwa ujumla wanaanimi. Ni vyema basi kujua kwa muhtasari nini maana ya maneno haya.
Demokrasia
Neno Demokrasia linatumika kijamii pamoja na kisiasa. Linatumika katika nyanja nyingi za maisha kama katika kazi, ndoa, dini, elimu, kiuchumi n.k. Ila neon hili linatumika zaidi katika siasa.
Demokrasia inaweza kutafsiriwa katika misingi yake toka lugha ya Kigiriki. Demos = the people, Kratos = power. Hivyo basi demokrasia ni mfumo wa kiutawala ambapo nguvu ya kisiasa inatoka kwa wananchi. Au ni mfumo wa kisiasa ambampo nguvu za kiutawala zinatoka kwa wananchi.
Kadhalika demokrasia inaweza kuwa ya moja kwa moja ama ya uwakilishi. Katika mazingira yetu hatuwezi wote wananchi mil 40 kufanya maamuzi kwa niaba na kwa ajili yetu. Hivyo umuhimu wa demokrasia ya uwakilishi ndipo inapohusika. Demokrasia ya uwakilishai ni pale ambapo watu wachache wamechaguliwa ama kuteuliwa kuwakilisha mawazo ya wengi, na kwa usawa na haki katika vyombo vya maamuzi kama serikali, bunge na mahakama.
Maendeleo
Umoja wa mataifa kitengo cha maendeleo kinafafanua maendeleo kuwa ni kuwa na maisha marefu nay a afya, kuwa na ufahamu, kuwa na uwezo wa kuzifikia rasilimali zinazohitajika kwa maisha bora na kuweza kushiriki katika maisha ya kijamii kwa ujumla. Kwa lugha nyingine maendeleo ni kuwajengea watu uwezo katika nyanja zote za kimaisha kama siasa, uchumi, kijamii, kiutamaduni ili watu waweze kudhibiti maisha yao, kuelezea mahitaji yao na kutafuta ufumbuzi kwa matatizo yao.
Demokrasia na Maendeleo ni dhana mbili zinazoelekea kufanana na wakati huo huo kutofautiana. Zinafanana kwa misingi kuwa dhana zote mbili ni hitimisho la maisha bora kwa wananchi husika. Zinatofautiana kwa misingi kuwa kipi kianze na kipi kifuate . wakati mwingine ili pawepo na maendeleo, nguvu ya ziada inabidi kutumika. Tuliona hili katika utekelezaji wa Azimio la Arusha. Tunaona hili kwa wenzetu kama ilivyokuwa kwa Ujerumani, USSR na mataifa mengine. Demokrasia kwa upande wake inataka maridhiano na maamuzi ya wengi ama uwakilishi wa hayo maamuzi, kitu ambacho kinaweza kuchelewesha utekelezaji kisa tu mawazo ya mtu/watu Fulani yaheshimiwe.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA
Tunapoangalia katika ngazi ya chama tunaona kuwa Chadema kikiwa na dhana zake mbili kinashindwa aidha kuwa na kauli moja ni dhana gani ifuatwe kwanza, ama mawazo ya nani yapewe kipaumbele. Inawezekana mambo kuwa shwari ndani ya Chadema ila ni media na Dola kutaka kuchafua tu hali ya hewa ya chama. Inawezekana pia kuwa ndani ya chama hali si shwari hivyo kusababisha mivutano ya utekelezaji wa dhana hizo mbili-kwamba nani anatekeleza demokrasia na nani anatekeleza maendeleo.
Labda tujadili kuanzia hapa. Ndani ya Chadema kuna wanaoamini katika demokrasia na kuna wanaoamini katika maendeleo ila mwisho wa siku wana kauli ya kikasuku ya People's Power! Kuna uwezekano wa kubeba dhana hizi mbili kwa wakati mmoja? Kuna haja ya kuchelewesha moja ili iliyobaki ifanye kazi ili mwisho wa siku lengo litimie? Tuyajadili haya kwa manufaa ya chama chenyewe, pamoja na imani na matumaini ambayo tumeyaweka juu ya chama kwa mustakabali wa maisha bora kwa kila mtanzania
Yajue pia ya CCM kwa ufupi hapa
Soma uchambuzi wa wengine hapa
Demokrasia
Neno Demokrasia linatumika kijamii pamoja na kisiasa. Linatumika katika nyanja nyingi za maisha kama katika kazi, ndoa, dini, elimu, kiuchumi n.k. Ila neon hili linatumika zaidi katika siasa.
Demokrasia inaweza kutafsiriwa katika misingi yake toka lugha ya Kigiriki. Demos = the people, Kratos = power. Hivyo basi demokrasia ni mfumo wa kiutawala ambapo nguvu ya kisiasa inatoka kwa wananchi. Au ni mfumo wa kisiasa ambampo nguvu za kiutawala zinatoka kwa wananchi.
Kadhalika demokrasia inaweza kuwa ya moja kwa moja ama ya uwakilishi. Katika mazingira yetu hatuwezi wote wananchi mil 40 kufanya maamuzi kwa niaba na kwa ajili yetu. Hivyo umuhimu wa demokrasia ya uwakilishi ndipo inapohusika. Demokrasia ya uwakilishai ni pale ambapo watu wachache wamechaguliwa ama kuteuliwa kuwakilisha mawazo ya wengi, na kwa usawa na haki katika vyombo vya maamuzi kama serikali, bunge na mahakama.
Maendeleo
Umoja wa mataifa kitengo cha maendeleo kinafafanua maendeleo kuwa ni kuwa na maisha marefu nay a afya, kuwa na ufahamu, kuwa na uwezo wa kuzifikia rasilimali zinazohitajika kwa maisha bora na kuweza kushiriki katika maisha ya kijamii kwa ujumla. Kwa lugha nyingine maendeleo ni kuwajengea watu uwezo katika nyanja zote za kimaisha kama siasa, uchumi, kijamii, kiutamaduni ili watu waweze kudhibiti maisha yao, kuelezea mahitaji yao na kutafuta ufumbuzi kwa matatizo yao.
Demokrasia na Maendeleo ni dhana mbili zinazoelekea kufanana na wakati huo huo kutofautiana. Zinafanana kwa misingi kuwa dhana zote mbili ni hitimisho la maisha bora kwa wananchi husika. Zinatofautiana kwa misingi kuwa kipi kianze na kipi kifuate . wakati mwingine ili pawepo na maendeleo, nguvu ya ziada inabidi kutumika. Tuliona hili katika utekelezaji wa Azimio la Arusha. Tunaona hili kwa wenzetu kama ilivyokuwa kwa Ujerumani, USSR na mataifa mengine. Demokrasia kwa upande wake inataka maridhiano na maamuzi ya wengi ama uwakilishi wa hayo maamuzi, kitu ambacho kinaweza kuchelewesha utekelezaji kisa tu mawazo ya mtu/watu Fulani yaheshimiwe.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA
Tunapoangalia katika ngazi ya chama tunaona kuwa Chadema kikiwa na dhana zake mbili kinashindwa aidha kuwa na kauli moja ni dhana gani ifuatwe kwanza, ama mawazo ya nani yapewe kipaumbele. Inawezekana mambo kuwa shwari ndani ya Chadema ila ni media na Dola kutaka kuchafua tu hali ya hewa ya chama. Inawezekana pia kuwa ndani ya chama hali si shwari hivyo kusababisha mivutano ya utekelezaji wa dhana hizo mbili-kwamba nani anatekeleza demokrasia na nani anatekeleza maendeleo.
Labda tujadili kuanzia hapa. Ndani ya Chadema kuna wanaoamini katika demokrasia na kuna wanaoamini katika maendeleo ila mwisho wa siku wana kauli ya kikasuku ya People's Power! Kuna uwezekano wa kubeba dhana hizi mbili kwa wakati mmoja? Kuna haja ya kuchelewesha moja ili iliyobaki ifanye kazi ili mwisho wa siku lengo litimie? Tuyajadili haya kwa manufaa ya chama chenyewe, pamoja na imani na matumaini ambayo tumeyaweka juu ya chama kwa mustakabali wa maisha bora kwa kila mtanzania
Yajue pia ya CCM kwa ufupi hapa
Soma uchambuzi wa wengine hapa