Elections 2010 Demokrasia Matatani

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,930
Kwa miaka tumeambiwa wao ndio waasisi wa demokrasia nchini na ya kuwa wao ndio walinzi wa demokrasia hiyo. Leo hii Taifa letu linaenda kupitia kipindi cha majaribu na tusipoangalia tunaweza kupita kipindi cha giza totoro. Wananchi wetu wamepiga kura vizuri jana na kutulia wakisubiri matokeo yatoke wenye kushinda wawe wameshinda na walioshindwa wawe wameshindwa.

Hata hivyo hali hadi hivi sasa ni tete na kama nilivyoasa masaa kadhaa huko nyuma hali hii ya kutokujua na mambo ambayo yanaonekana kama kulazimisha uongozi uliokatliwa juu ya nchi kana kwamba ni urithi wa watu fulani itapelekea mgongano wa wazi kati ya watawala na watawaliwa.

Demokrasia yetu iko matatani. Ninawasihi vijana kutulia na kuwa na uvumilivu lakini wakati huo huo Tume ya Uchaguzi iwatendee haki Watanzania na kufanya kile walichoapishwa kufanya. Vyombo vya usalama vikae nje sana katika hili na wasiwe wabebaji wa maagizo ambayo yana athari kwa wananchi wa taifa lao. Tutumie hekima kila inapostahili vinginevyo yale tuliyoyahofia kweli yatatokea na tutajikuta tunashindwa hata kumlaumu mtu.

Hadi hivi sasa hata hivyo ni watu wa Tume ya Uchaguzi ndio watasababisha matatizo kwani wanashindwa kufanya kitu kidogo sana kama kutangaza matokeo. Hadi hivi sasa kuna dalili matokeo wanayotaka kutolewa yale ni yale ya CCM kushinda lakini maeneo mengine wanabania. Jamani hii si haki, tunapolilia utaalamu na usomi basi tunatarajia tuone kweli watu wanafanya kazi kisomi na kwa weledi. j

Liacheni litakalokuwepo liwe, Tanzania itakuwepo tu. Heshima ya CCM inaegemea kabisa kwenye matukiio yanayoendelea kutokea sasa hivi nchini. NI katika haya CCM itahukumiwa na historia. Ni katika haya Rais ambaye amependwa na wananchi licha ya tofauti za kisiasa atajikuta anahukumiwa. Naomba tena tusilazimishe ushindi wa kishindo.

Demokrasia yetu ni kubwa zaidi kuliko furaha na hisia za kikundi kimoja cha watu. Kama hawakutaka kuwa tayari kusimama mbele ya hukumu ya Watanzania wasingeitisha uchaguzi jamani ili tuwe na utawala wa kudumu tu. Demokrasia bila uwezekano wa kushindwa siyo demokrasia. Sauti ya wananchi isikike.
 
tatizo vijana wetu hawakupata mbinu za kulina uraia wala elimu yake, ni serikali ya CCM ambayo huwa haipendi wa chini wajue rights zao.... sasa wale vijana hawajui even how to demand their rights

Tuombee amnai na utulivu na mlio mwanza na arusha, jitahidini sana kuwatuliza vijana

nijuavyo mimi vurugu zinachochewa na ccm ili kuharibu uchaguzi kwani wameshindwa vibaya sana
 
ktk kuhitimisha kampeni zao uwanja wa jangwani, mkapa alisisitiza kuwa ccm ni lazima ishinde na mapinduzi daima!!!!!!!
 
Hii ndio watu wanasema mkuki kwa nguruwe, double standard ya hali ya juu, Shimbo where are you? Mwema? enyi mliojidai kuwa watu wakubali matokeo mko wapi pale CCM wanapokataa matokeo na kusababisha fujo?
Ingekuwa ni vyama vingine mngekuwa tayari kuwa crucify!!
Lakini hakuna marefu yasiyo na ncha, iko siku mtalipia unafiki huu!!! :A S angry:
 
Wewe mwanakijiji ulisema matokeo yote ya ubunge tutayajua leo na ya uraisi yatatoka kesho. Nina shaka! Huku bongo siku ndo imekaribia kuisha na hata nusu ya hayo matokeo ya ubunge hakuna
 
Ni kweli nipo Arusha lakini siamini ninacho kiona...ccm wanataka watu wafe ili wapate sababu.
 
Tatizo ni kwamba walio na mamlaka ya kulinda na kutangaza demokrasia kwao inafanywa kinadharia zaidi.Hawana hata mawazo ya kuitekeleza kwa vitendo.Na mbaya zaidi wanachukulia kama wao wakipata ni demokrasia wenzao wakipata hiyo sio demokrasia na ndipo ninapoungana na Mwanakijiji kuwa kweli Demokrasia ipo mashakani.
 
Hadi hivi sasa hata hivyo ni watu wa Tume ya Uchaguzi ndio watasababisha matatizo kwani wanashindwa kufanya kitu kidogo sana kama kutangaza matokeo. Hadi hivi sasa kuna dalili matokeo wanayotaka kutolewa yale ni yale ya CCM kushinda lakini maeneo mengine wanabania. Jamani hii si haki, tunapolilia utaalamu na usomi basi tunatarajia tuone kweli watu wanafanya kazi kisomi na kwa MWANAKIJIJI INASIKITISHA HAPA TATIZO SIO TUME YA UCHAGUZI.TUME YA UCHAGUZI NDIO CCM NA CCM NDIO TUME YA UCHAGUZI,KAMA WALIVYODHANI CCM YA KUA CCM NDIO TANZANIA NA TANZANIA NDIO CCM NI MAKOSA MAKUBWA "CCM HAIKUJIAADA KUSHINDWA HAPA NDIO TATIZO LINAPOAANZIA"HALI HII NI HATARI NA NITISHIO KWA AMANI YA NCHI.NINANI ASIEJUA YA KUA MKUSANYIKO MKUBWA WA WATU WAKISUBIRI HAKI YAO YA KUJUA HAKI YAO YA UCHAGUZI PASIPOKUA NA MAJIBU YA KULIDHISHA NIA HATARI? CCM UMSITUPELEKE HUKOMUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Kwa kweli CCM imejiandaa kulipeleka Taifa hili sehemu ambayo haikujiandaa kwenda. Ni jambo la kukatisha tamaa sana kuhusu demokrasia ya nchi hii. Tunaimba kwenye majukwaa kuwa tunadumisha demokrasia kumbe ni double standards. Inashangaza kuona matokeo yanayotangazwa ni kutoka maeneo yale ambayo CCM imeshinda na maeneo ambayo mapambanaji wameshindwa hawataki wananchi wayajue. Ni demokrasia gani hiyo? Nchi inaelekea pabaya maana vijana hawa hawako tayari kuona haki zao zinaporwa. Mungu wahukumu wote wanaoiba haki hizi za watanzania
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom