Demokrasia inavyohujumiwa CCM. Mwenyekiti hana mshindani

CCM wanatumia dola kuikalia Tanzania kimabavu..
Marehemu wetu huyu kama kweli Mungu yupo na zile amri 10 alizompa Mussa bado zinafanya kazi zotee...aisee kama si kuni muda muda huu basi ni sufuria.
 
UNajua Katiba yao inasema nini juu ya hilo? Unawalaumu wafuate ya kwako wakati wao wana utaratibu uliopitishwa? Naona kama kuna kuwashwa washwa!
Katiba inaweza kuwa ya kidikteta!
 
Hakuna cha kusema pamoja na kuwa mwenyekiti wa muda mrefu ....... Mbowe naye hovyo tu! mambo ya kuharibu maendeleo ya chama kwa kudanganya unapigiwa kura. Kura gani ya kijinga hiyo. Mbowe aondoke awaachie wengine nao wawaze kivingine. Tusitake kumpamba kwa matendo ya kijinga-jinga!

Ukiamua kusema ukweli, sema kwa kila chama badala ya kupuliza udhaifu wa CHADEMA uonekane ni mdogo. Udhaifu wao ni mkubwa na hauwafikishi kokote, kwa enzi yoyote!
Kinachojalisha ni kufanyika kwa uchaguzi huru na haki na siyo usimikaji kama wa kichifu!
 
Unataka Mwenyekiti Wa chama amfokee Rais wa Nchi.
Chama ni taasisi inayojitegemea ikiwa na wanachama wake na uraisi pia ni taasisi inayojitegemea pia ikiongoza taifa kwa ujumla wake kupitia chama Fulani its better mwenyekiti wa chama awe mwngne tofauti na Raisi.
 
Kiti cha mwenyekiti wa CCM Taifa kiko wazi baada ya kifo cha Rais Magufuli. Kinachofuata hivi sasa ni kumsimika Mama Samia Suluhu kuwa mwenyekiti mpya baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Tanzania. Hii si sawa kabisa na wala hakuna demokrasia hapo!

Kwanini kusifanyike uchaguzi ili wanachama wenye sifa washindanishwe kwa kupigiwa kura? Iko wapi demokrasia ambayo CCM inajitapa nayo? Makundi ndani ya CCM yanazaliwa kwa sababu hii. Kwani CCM isingeshinda kiti cha Urais utaratibu upi ungefuatwa kumpata mwenyekiti mpya?

Mbowe pamoja na kuwa mwenyekiti wa muda mrefu CHADEMA lakini anapigiwa kura. Hii ndiyo demokrasia.

Kitu cha ajabu kuna viongozi ndani ya CCM wakiongozwa na Polepole wameanza kujipendekeza na kujibebisha kwa Mama Samia ili waendeleze ulaji wao. Pity!
Umetumwa?
 
Kuwa na hekima... Umeleta hoja..na hakuna aliyekutusi... Ukitumia muda wako kujibu kama Mwanaume ulifunzwa kwenu unakuwa unapungukiwa na nini!?

Ikiwa rais wa atatoka ADA TADEA ila asiwe mwenyekiti wa chama chake... Akirudi chamani anakuwa na mwenyekiti wake..

Kwa sheria za vyama mbalimbali... chama kinaweza kumfuta mtu uanachama...na anakosa nafasi ya kuendelea kuwa kiongozi katika.nafasi aliyogombea. Wakimfuata Rais... Au wakitumia.power hiyo kujinufaisha!?

Yaani umekaa hapo umeshashiba basi unaona wote wanaokaa kuja na hizi taratibu hayawani na vichwa maji!?
Maana nzima ya ccm kufanya rais ndo awe mwenyekiti wa chama kwanza ni hulka yao ya kutaka kutumia resources za nchi vibaya au kwa manufaa ya chama Chao na pili kurahisisha wizi wa kura kupitia vyonbo vya serikali na tatu chama kutotambua wajibu wake kwa serikali basi
 
Mbona hukuyajadili hayo wakati wa mwenyekiti aliyeaga dunia?
Hiki ni kitu kipya kwa Tanzania Rais aliye madarakani kufariki dunia na kuacha ombwe la uongozi kwa muda mfupi. Lakini pia ni wakati muafaka kuwakumbusha CCM kuangalia namna bora ya kuboresha demokrasia ndani ya chama chao na kuwapa nafasi na uhuru wanachama wao kushiriki katika kupata kiongozi wao mkuu.
 
Soma Katiba Kiongozi.... Soma. Ni muhimu sana.. kabla hujaungumza juu ya kitu uwe unakijua atleast mara tatu zaidi ya Mtu wa kawaida..

Na tusiwe watu wa kulalamika tuuu..kila wakati.. its unhealthy.. ukiona shida sema utatuzi..sio wakutoa hewani.. soma uone uvunjifu wa taratibu kwa Mujibu wa sheria zinazoongoza swala hilo.. tupe alternative... Unatoka umefaidika kwa kujua na sisi tunasoma bandiko lako tunakuwa tumejua kupitia kwako.

Tusome au tuulize ..tusije kuandika tu for the sake of writing.
Hadithi nyingiiiii mwishoe jibu hakuna. Du, mlalamishi huyuuuu.

Ngoja nisubiri wanaoijua katiba ya CCM waje wadadafue kiutaalam wa political science.
 
Maana nzima ya ccm kufanya rais ndo awe mwenyekiti wa chama kwanza ni hulka yao ya kutaka kutumia resources za nchi vibaya au kwa manufaa ya chama Chao na pili kurahisisha wizi wa kura kupitia vyonbo vya serikali na tatu chama kutotambua wajibu wake kwa serikali basi
Mbaya zaidi wamewalazimisha wakuu wa vyombo vya usalama kuwa wana CCM ili kurahisisha hujuma!
 
Kiti cha mwenyekiti wa CCM Taifa kiko wazi baada ya kifo cha Rais Magufuli. Kinachofuata hivi sasa ni kumsimika Mama Samia Suluhu kuwa mwenyekiti mpya baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Tanzania. Hii si sawa kabisa na wala hakuna demokrasia hapo!

Kwanini kusifanyike uchaguzi ili wanachama wenye sifa washindanishwe kwa kupigiwa kura? Iko wapi demokrasia ambayo CCM inajitapa nayo? Makundi ndani ya CCM yanazaliwa kwa sababu hii. Kwani CCM isingeshinda kiti cha Urais utaratibu upi ungefuatwa kumpata mwenyekiti mpya?

Mbowe pamoja na kuwa mwenyekiti wa muda mrefu CHADEMA lakini anapigiwa kura. Hii ndiyo demokrasia.

Kitu cha ajabu kuna viongozi ndani ya CCM wakiongozwa na Polepole wameanza kujipendekeza na kujibebisha kwa Mama Samia ili waendeleze ulaji wao. Pity!
Kwani NJEMBA hana kadi ili awe Mwenyekiti?
 
Aina hii ya fikra ndio imetufikisha pabaya. Tanzania sio kisiwa, nasema tena sio kisiwa!! Tuna mambo ya ujumla katika dunia hii. Ulichokisema ndio “chama kushika hatamu”. Utakubali kuwa hata hapa nyumbani, Lissu na marehemu Seif hawakuwa viongozi wa juu kabisa katika vyama vyao. Hii ni ishahidi kuwa kinachofanyika CCM sio utaratibu wa ki-nchi bali ki-CCM. Na Mwinyi wa Zanzibar anawezaje kuongoza Zanzibar na wakati sio hata Mwenyekiti upande wa Zanzibar? Au unasema hapa kuwa anaamliwa na Mwenyekiti/Rais wa Jamhuri mambo ya kufanya? Ikiwa ni hivo, uko wapi uhuru wa mamlaka hiyo yenye bunge na mahakama zake??

Kiazi ni kiazi tu!! Ujuaji mwingiii kumbe hakuna kitu!

Hayo mamlaka ya kiserikali kwa Zanzibar uko na hakika ni ya one hundred percent?

And how about Britain? How do they do it?
 
Back
Top Bottom