Demokrasia ina gharama zake ikiwemo marudio ya chaguzi ndogo. Je, zisifanyike?

thetallest

JF-Expert Member
Oct 21, 2017
8,256
9,085
Kupanga ni kuchagua.marudio ya chaguzi ndogo zinazoendelea nchini ni halali kwa mujibu wa katiba ,kanuni na taratibu tulizojiwekekea kama nchi,na wabunge waliopitisha mswaada huu walikua ni wa vyama vyote vya siasa vilivyokua na wabunge wakati huo.

Inashangaza sasa kuona baadhi yetu tunalaumu utaratibu huu wa kisheria.

Naamini kwa wanaolaumu wako sawa kwa sababu nguvu yao inapungua kwa kasi sana. Ingekuwa wabunge na madiwani hao wa chama X wangekua wanahama toka chama Y kuja chama X ingekua ni shangwe sana kwa chama X, wakijinasibu kwamba wahamaji hao wamejitambua na sifa kedekede kuwamwagia.

Nionavyo mimi ni kwamba kuna tatizo ndani ya vyama vyenyewe vya siasa ,ni ngumu kunielewe kwa mwenye itikadi ,ushabiki,na mtanguliza maslahi binafisi. Pamba walizoweka masikioni watazitoa wakati muda umewatupa mkono.

Tusipokubali kusikia maoni tofauti, kuhojiwa, tukaamua kuhodhi vyama vya siasa kama mali binafsi, tunaviua vyama vyetu kwa kiburi cha kusingizia wanachama wananunuliwa.

Ifike mahala demokrasia itawale ndani ya vyama vya siasa ili kuondoa hii sintofahamu ya wimbi la hamahama.

Niwapongeze wabunge na madiwani wanaotumia demokrasia kufanya maamuzi sahihi kwa wakati sahihi.

Mwisho kabisa, naomba mchanganuo toka kwa yeyote yule ambae ana data kamili za gharama za uchaguzi walau za jimbo moja tu la uchaguzi wa marudio,kwa maana ya shilingi kwa shilingi, ili sisi wadau tuone kisha tulipeleke suala hili bungeni kufanyiwa amendments
 
Hizi siasa za mabavu, fitna, uongo, ulaghai, wizi, utapeli, hila, udanganyifu, ghilba, dhulma, utekaji, uonevu, unyanyasaji, ufisadi na mengine kama hayo ndo hupelekea kuibuka kwa yale tunayosikia huko kwingine.. Tujirekebishe
 
Bora zisifanyike endapo hatupo tayari kuheshimu sheria na kanuni zetu. Kwa afya na ustawi wa umoja taifa letu.
 
Hizi siasa za mabavu, fitna, uongo, ulaghai, wizi, utapeli, hila, udanganyifu, ghilba, dhulma, utekaji, uonevu, unyanyasaji, ufisadi na mengine kama hayo ndo hupelekea kuibuka kwa yale tunayosikia huko kwingine.. Tujirekebishe
Yametamalaki sana ndani ya vyama vya siasa ,ni kweli
 
Bora zisifanyike endapo hatupo tayari kuheshimu sheria na kanuni zetu. Kwa afya na ustawi wa umoja taifa letu.
Kuepuka hizi chaguzi, ukitoa sababu za vifo, ni vyama vyenyewe kuheshimu taratibu kanuni,walizojiwekea,umungu mtu ndani ya vyama ukiendelea hatuwezi epuka chaguzi hizi
 
Kupanga ni kuchagua.marudio ya chaguzi ndogo zinazoendelea nchini ni halali kwa mujibu wa katiba ,kanuni na taratibu tulizojiwekekea kama nchi,na wabunge waliopitisha mswaada huu walikua ni wa vyama vyote vya siasa vilivyokua na wabunge wakati huo.

Tunaweza kupunguza gharama kwa kuondoa huu utaratibu wa kurudia chaguzi bila kubomoa demokrasia. Angalia Afrika Kusini kwa mfano, nadhani mbunge akihama chama anahama na ubunge wake. Na pia tunaweza kusema Wabunge hawaruhusiwi kuhama Chama wakshachaguliwa Ubunge, kwa sababu ni demokrasia ilisababisha wawe wbunge kupitia chama fulani.
 
Tunaweza kupunguza gharama kwa kuondoa huu utaratibu wa kurudia chaguzi bila kubomoa demokrasia. Angalia Afrika Kusini kwa mfano, nadhani mbunge akihama chama anahama na ubunge wake. Na pia tunaweza kusema Wabunge hawaruhusiwi kuhama Chama wakshachaguliwa Ubunge, kwa sababu ni demokrasia ilisababisha wawe wbunge kupitia chama fulani.
Wazo jema,sasa basi,badala ya kuwatukana,kuwadhihaki,kuwakejeri kwa wao kutumia demokrasi ni bora tukashinikiza sheria au taratibu hizi bunge lizifanyie marekebisho
 
Wazo jema,sasa basi,badala ya kuwatukana,kuwadhihaki,kuwakejeri kwa wao kutumia demokrasi ni bora tukashinikiza sheria au taratibu hizi bunge lizifanyie marekebisho
Nape alishasema hayo, watu wake wa CCM kutia na kina Makonda wakamzomea
 
Kupanga ni kuchagua.marudio ya chaguzi ndogo zinazoendelea nchini ni halali kwa mujibu wa katiba ,kanuni na taratibu tulizojiwekekea kama nchi,na wabunge waliopitisha mswaada huu walikua ni wa vyama vyote vya siasa vilivyokua na wabunge wakati huo.

Inashangaza sasa kuona baadhi yetu tunalaumu utaratibu huu wa kisheria.
Naamini kwa wanaolaumu wako sawa kwa sababu nguvu yao inapungua kwa kasi sana .
Ingekua wabunge na madiwani hao wa chama X wangekua wanahama toka chama Y kuja chama X ingekua ni shangwe sana kwa chama X,wakijinasibu kwamba wahamaji hao wamejitambua na sifa kedekede kuwamwagia.

Nionavyo mimi ni kwamba kuna tatizo ndani ya vyama vyenyewe vya siasa ,ni ngumu kunielewe kwa mwenye itikadi ,ushabiki,na mtanguliza maslahi binafisi.,pamba walizoweka masikioni watazitoa wakati muda umewatupa mkono.
Tusipokubali kusikia maoni tofauti ,kuhojiwa,tukaamua kuhodhi vyama vya siasa kama mali binafsi ,tunaviua vyama vyetu kwa kiburi cha kusingizia wanachama wananunuliwa.
Ifike mahala demokrasia itawale ndani ya vyama vya siasa ili kuondoa hii sintofahamu ya wimbi la hamahama.
Niwapongeze wabunge na madiwani wanaotumia demokrasia kufanya maamuzi sahihi kwa wakati sahihi.

Mwisho kabisa,naomba mchanganuo toka kwa yoyote yule ambae ana data kamili za gharama za uchaguzi walau za jimbo moja tu la uchaguzi wa marudio,kwa maana ya shilingi kwa shilingi,ili sisi wadau tuone. kisha tulipeleke suala hili bungeni kufanyiwa amendments
Ulichozumngumza ni sahihi,ndani ya vyama kuna matatizo ya uungu mtu
 
Kupanga ni kuchagua.marudio ya chaguzi ndogo zinazoendelea nchini ni halali kwa mujibu wa katiba ,kanuni na taratibu tulizojiwekekea kama nchi,na wabunge waliopitisha mswaada huu walikua ni wa vyama vyote vya siasa vilivyokua na wabunge wakati huo.

Inashangaza sasa kuona baadhi yetu tunalaumu utaratibu huu wa kisheria.
Naamini kwa wanaolaumu wako sawa kwa sababu nguvu yao inapungua kwa kasi sana .
Ingekua wabunge na madiwani hao wa chama X wangekua wanahama toka chama Y kuja chama X ingekua ni shangwe sana kwa chama X,wakijinasibu kwamba wahamaji hao wamejitambua na sifa kedekede kuwamwagia.

Nionavyo mimi ni kwamba kuna tatizo ndani ya vyama vyenyewe vya siasa ,ni ngumu kunielewe kwa mwenye itikadi ,ushabiki,na mtanguliza maslahi binafisi.,pamba walizoweka masikioni watazitoa wakati muda umewatupa mkono.
Tusipokubali kusikia maoni tofauti ,kuhojiwa,tukaamua kuhodhi vyama vya siasa kama mali binafsi ,tunaviua vyama vyetu kwa kiburi cha kusingizia wanachama wananunuliwa.
Ifike mahala demokrasia itawale ndani ya vyama vya siasa ili kuondoa hii sintofahamu ya wimbi la hamahama.
Niwapongeze wabunge na madiwani wanaotumia demokrasia kufanya maamuzi sahihi kwa wakati sahihi.

Mwisho kabisa,naomba mchanganuo toka kwa yoyote yule ambae ana data kamili za gharama za uchaguzi walau za jimbo moja tu la uchaguzi wa marudio,kwa maana ya shilingi kwa shilingi,ili sisi wadau tuone. kisha tulipeleke suala hili bungeni kufanyiwa amendments
Kata moja inakadiriwa kuwa mil 200-300 kulingana na idadi ya watu!Kuna majimbo yana kata mpaka 15,so ukipiga hesabu hapo ni kama bil 3-6 kwa jimbo!!!!!

Nways,hata mikutano ya kisiasa na maandamano ipo kikatiba!Nchi hii shida sio sheria,shida watawala wanachagua sheria zipi zifanye kazi na zipi wazipuuzie kulingana na maslahi yao!!!!!
 
Kata moja inakadiriwa kuwa mil 200-300 kulingana na idadi ya watu!Kuna majimbo yana kata mpaka 15,so ukipiga hesabu hapo ni kama bil 3-6 kwa jimbo!!!!!

Nways,hata mikutano ya kisiasa na maandamano ipo kikatiba!Nchi hii shida sio sheria,shida watawala wanachagua sheria zipi zifanye kazi na zipi wazipuuzie kulingana na maslahi yao!!!!!
Makadirio yako ni batili,lete uhalisia kamili
 
Kupanga ni kuchagua.marudio ya chaguzi ndogo zinazoendelea nchini ni halali kwa mujibu wa katiba ,kanuni na taratibu tulizojiwekekea kama nchi,na wabunge waliopitisha mswaada huu walikua ni wa vyama vyote vya siasa vilivyokua na wabunge wakati huo.

Inashangaza sasa kuona baadhi yetu tunalaumu utaratibu huu wa kisheria.
Naamini kwa wanaolaumu wako sawa kwa sababu nguvu yao inapungua kwa kasi sana .
Ingekua wabunge na madiwani hao wa chama X wangekua wanahama toka chama Y kuja chama X ingekua ni shangwe sana kwa chama X,wakijinasibu kwamba wahamaji hao wamejitambua na sifa kedekede kuwamwagia.

Nionavyo mimi ni kwamba kuna tatizo ndani ya vyama vyenyewe vya siasa ,ni ngumu kunielewe kwa mwenye itikadi ,ushabiki,na mtanguliza maslahi binafisi.,pamba walizoweka masikioni watazitoa wakati muda umewatupa mkono.
Tusipokubali kusikia maoni tofauti ,kuhojiwa,tukaamua kuhodhi vyama vya siasa kama mali binafsi ,tunaviua vyama vyetu kwa kiburi cha kusingizia wanachama wananunuliwa.
Ifike mahala demokrasia itawale ndani ya vyama vya siasa ili kuondoa hii sintofahamu ya wimbi la hamahama.
Niwapongeze wabunge na madiwani wanaotumia demokrasia kufanya maamuzi sahihi kwa wakati sahihi.

Mwisho kabisa,naomba mchanganuo toka kwa yoyote yule ambae ana data kamili za gharama za uchaguzi walau za jimbo moja tu la uchaguzi wa marudio,kwa maana ya shilingi kwa shilingi,ili sisi wadau tuone. kisha tulipeleke suala hili bungeni kufanyiwa amendments
Chaguzi ndogo zimekisa sifa.Si za huru tena.Ni mawili ama NEC isukwe upya au chaguz za marudio zifutwe
 
Chaguzi ndogo zimekisa sifa.Si za huru tena.Ni mawili ama NEC isukwe upya au chaguz za marudio zifutwe
Bunge ndo lenye mamlaka hayo,tulishinikize liondoe utaratibu huu,kuwatukana wanaohama hakubadilishi utaratibu
 
Back
Top Bottom